< Mwanzo 48 >

1 Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
And it was after the things these and someone said to Joseph there! father your [is] sick and he took [the] two sons his with him Manasseh and Ephraim.
2 Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
And someone told to Jacob and he said here! son your Joseph he has come to you and he strengthened himself Israel and he sat on the bed.
3 Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
And he said Jacob to Joseph God Almighty he appeared to me at Luz in [the] land of Canaan and he blessed me.
4 naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
And he said to me here I [am] about to make fruitful you and I will multiply you and I will make you a company of peoples and I will give the land this to offspring your after you a possession of perpetuity.
5 “Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
And now [the] two sons your who were born to you in [the] land of Egypt until came I to you Egypt towards [belong] to me they Ephraim and Manasseh like Reuben and Simeon they will be[long] to me.
6 Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
And offspring your whom you have fathered after them to you they will be[long] on [the] name of brothers their they will be called in inheritance their.
7 Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
And I - when came I from Paddan she died on me Rachel in [the] land of Canaan on the journey at yet a distance of land to go Ephrathah and I buried her there on [the] journey of Ephrath that [is] Beth-lehem.
8 Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
And he saw Israel [the] sons of Joseph and he said who? [are] these.
9 Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
And he said Joseph to father his [are] sons my they whom he has given to me God in this [place] and he said fetch them please to me so I may bless them.
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
And [the] eyes of Israel they were heavy from old age not he was able to see and he brought near them to him and he kissed them and he embraced them.
11 Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
And he said Israel to Joseph to see face your not I judged and here! he has shown me God also offspring your.
12 Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
And he took Joseph them from with knees his and he bowed down to face his [the] ground towards.
13 Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
And he took Joseph [the] two of them Ephraim at right [hand] his from [the] left of Israel and Manasseh at left [hand] his from [the] right of Israel and he brought [them] near to him.
14 Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
And he stretched out Israel right [hand] his and he put [it] on [the] head of Ephraim and he [was] the young and left [hand] his on [the] head of Manasseh he laid cross-wise hands his for Manasseh [was] the firstborn.
15 Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
And he blessed Joseph and he said God whom they walked about fathers my before him Abraham and Isaac God who shepherded me from duration my until the day this.
16 Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
The angel who has redeemed me from all harm may he bless the lads and may it be called in them name my and [the] name of fathers my Abraham and Isaac and may they multiply to abundance in [the] midst of the earth.
17 Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
And he saw Joseph that he will put father his [the] hand of right his on [the] head of Ephraim and it was displeasing in view his and he grasped [the] hand of father his to remove it from on [the] head of Ephraim on [the] head of Manasseh.
18 Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
And he said Joseph to father his not thus O father my for this [is] the firstborn put right [hand] your on head his.
19 Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
And he refused father his and he said I know O son my I know also he he will become a people and also he he will become great and but brother his young he will become great more than him and offspring his it will be [the] fullness of the nations.
20 Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
And he blessed them on the day that saying by you it will bless Israel saying may he make you God like Ephraim and like Manasseh and he put Ephraim before Manasseh.
21 Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
And he said Israel to Joseph here! I [am] about to die and he will be God with you and he will bring back you to [the] land of fathers your.
22 Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
And I I give to you a shoulder one over brothers your which I took from [the] hand of the Amorite[s] by sword my and by bow my.

< Mwanzo 48 >