< Mwanzo 24 >

1 Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
Now Abraham was very old and Yahweh had blessed Abraham in all things.
2 Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
Abraham said to his servant, the one who was the oldest of his household and who was in charge of all that he had, “Put your hand under my thigh
3 Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
and I will make you swear by Yahweh, the God of heaven and the God of the earth, that you will not get a wife for my son from the daughters of the Canaanites, among whom I make my home.
4 bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
But you will go to my country, and to my relatives, and get a wife for my son Isaac.”
5 Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
The servant said to him, “What if the woman will not be willing to follow me to this land? Must I take your son back to the land from which you came?”
6 Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
Abraham said to him, “Make sure that you do not take my son back there!
7 Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
Yahweh, the God of heaven, who took me from my father's house and from the land of my relatives, and who promised me with a solemn oath saying, 'To your offspring I will give this land,' he will send his angel before you, and you will get a wife for my son from there.
8 Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
But if the woman is not willing to follow you, then you will be free from this oath of mine. Only you are not to take my son back there.”
9 Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
So the servant put his hand under the thigh of Abraham his master, and swore to him concerning this matter.
10 Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
The servant took ten of his master's camels and departed. He also took with him all kinds of gifts from his master. He departed and went to the region of Aram Naharaim, to the city of Nahor.
11 Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
He made the camels kneel down outside the city by the well of water. It was evening, the time that women go out to draw water.
12 Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
Then he said, “Yahweh, God of my master Abraham, grant me success today and show covenant faithfulness to my master Abraham.
13 Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
Look, here I am standing by the spring of water, and the daughters of the men of the city are coming out to draw water.
14 Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
Let it happen like this. When I say to a young woman, 'Please lower your pitcher so that I may drink,' and she says to me, 'Drink, and I will water your camels too,' then let her be the one that you have appointed for your servant Isaac. By this I will know that you have shown covenant faithfulness to my master.”
15 Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
It came about that even before he had finished speaking, behold, Rebekah came out with her water pitcher on her shoulder. Rebekah was born to Bethuel son of Milkah, the wife of Nahor, Abraham's brother.
16 Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
The young woman was very beautiful and a virgin. No man had slept with her. She went down to the spring and filled her pitcher, and came up.
17 Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
Then the servant ran to meet her and said, “Please give me a little drink of water from your pitcher.”
18 Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
She said, “Drink, my master,” and she quickly let down her pitcher on her hand, and gave him a drink.
19 Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
When she had finished giving him a drink, she said, “I will draw water for your camels also, until they have finished drinking.”
20 Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
So she hurried and emptied her pitcher into the trough, then ran again to the well to draw water, and drew water for all his camels.
21 Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
The man watched her in silence to see whether Yahweh had prospered his journey or not.
22 Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
As the camels finished drinking, the man brought out a gold nose ring weighing half a shekel, and two gold bracelets for her arms weighing ten shekels,
23 Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
and asked, “Whose daughter are you? Tell me please, is there room in your father's house for us to spend the night?”
24 Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
She said to him, “I am the daughter of Bethuel son of Milkah, whom she bore to Nahor.”
25 Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
She also said to him, “We have plenty of both straw and feed, and also room for you to spend the night.”
26 Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
Then the man bowed down and worshiped Yahweh.
27 akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
He said, “Blessed be Yahweh, the God of my master Abraham, who has not forsaken his covenant faithfulness and his trustworthiness toward my master. As for me, Yahweh has led me directly to the house of my master's relatives.”
28 Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
Then the young woman ran and told her mother's household about all of these things.
29 Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
Now Rebekah had a brother, and his name was Laban. Laban ran to the man who was out at the road by the spring.
30 Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
When he had seen the nose ring and the bracelets on his sister's arms, and when he had heard the words of Rebekah his sister, “This is what the man said to me,” he went to the man, and, behold, he was standing by the camels at the spring.
31 Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
Then Laban said, “Come, you blessed of Yahweh. Why are you standing outside? I have prepared the house, and a place for the camels.”
32 Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
So the man came to the house and he unloaded the camels. The camels were given straw and feed, and water was provided to wash his feet and the feet of the men who were with him.
33 Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
They set food before him to eat, but he said, “I will not eat until I have said what I have to say.” So Laban said, “Speak on.”
34 Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
He said, “I am Abraham's servant.
35 Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
Yahweh has blessed my master very much and he has become great. He has given him flocks and herds, silver and gold, male servants and female servants, and camels and donkeys.
36 Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
Sarah, my master's wife, bore a son to my master when she was old, and he has given everything that he owns to him.
37 Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
My master made me swear, saying, 'You must not get a wife for my son from the daughters of the Canaanites, in whose land I make my home.
38 ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
Instead, you must go to my father's family, and to my relatives, and get a wife for my son.'
39 “Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
I said to my master, 'Perhaps the woman will not follow me.'
40 “Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
But he said to me, 'Yahweh, before whom I walk, will send his angel with you and he will prosper your way, so that you will get a wife for my son from among my relatives and from my father's family line.
41 Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
But you will be free from my oath if you come to my relatives and they will not give her to you. Then you will be free from my oath.'
42 “Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
So I arrived today at the spring, and said, 'O Yahweh, God of my master Abraham, please, if you do indeed intend to make my journey successful—
43 Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
here I am, standing by the spring of water—let the young woman who comes out to draw water, the woman to whom I say, “Please give me a little water from your pitcher to drink,”
44 naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
the woman who says to me, “Drink, and I will also draw water for your camels”—let her be the woman whom you, Yahweh, have chosen for my master's son.'
45 “Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
Even before I had finished speaking in my heart, behold, Rebekah came out with her pitcher on her shoulder and she went down to the spring and drew water. So I said to her, 'Please give me a drink.'
46 “Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
She quickly lowered her pitcher from her shoulder and said, 'Drink, and I will give your camels water also.' So I drank, and she watered the camels also.
47 “Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
I asked her and said, 'Whose daughter are you?' She said, 'The daughter of Bethuel, Nahor's son, whom Milkah bore to him.' Then I put the ring in her nose and the bracelets on her arms.
48 nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
Then I bowed down and worshiped Yahweh, and blessed Yahweh, the God of my master Abraham, who had led me by the right way to find the daughter of my master's relative for his son.
49 Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
Now therefore, if you are prepared to show covenant faithfulness and trustworthiness to my master, tell me. But if not, tell me, so that I may turn to the right hand or to the left.”
50 Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
Then Laban and Bethuel answered and said, “The thing has come from Yahweh; we cannot speak to you either bad or good.
51 Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
Look, Rebekah is before you. Take her and go, so she may be the wife of your master's son, as Yahweh has spoken.”
52 Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
When Abraham's servant heard their words, he bowed himself down to the ground to Yahweh.
53 Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
The servant brought out articles of silver and articles of gold, and clothing, and gave them to Rebekah. He also gave precious gifts to her brother and to her mother.
54 Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
Then he and the men who were with him ate and drank. They stayed there overnight, and when they arose in the morning, he said, “Send me away to my master.”
55 Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
Her brother and her mother said, “Let the young woman stay with us for a few more days, at least ten. After that she may go.”
56 Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
But he said to them, “Do not hinder me, since Yahweh has prospered my way. Send me on my way so that I may go to my master.”
57 Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
They said, “We will call the young woman and ask her.”
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
So they called Rebekah and asked her, “Will you go with this man?” She replied, “I will go.”
59 Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
So they sent their sister Rebekah, along with her female servant, on her journey with Abraham's servant and his men.
60 Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
They blessed Rebekah, and said to her, “Our sister, may you be the mother of thousands of ten thousands, and may your descendants possess the gate of those who hate them.”
61 Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
Then Rebekah arose, and she and her servant girls mounted the camels, and followed the man. Thus the servant took Rebekah, and went his way.
62 Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
Now Isaac was living in the Negev, and had just returned from Beer Lahai Roi.
63 Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
Isaac went out to meditate in the field in the evening. When he looked up and saw, behold, there were camels coming!
64 Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
Rebekah looked, and when she saw Isaac, she jumped down from the camel.
65 na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
She said to the servant, “Who is that man who is walking in the field to meet us?” The servant said, “It is my master.” So she took her veil, and covered herself.
66 Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
The servant recounted to Isaac all the things that he had done.
67 Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
Then Isaac brought her into his mother Sarah's tent and took Rebekah, and she became his wife, and he loved her. So Isaac was comforted after his mother's death.

< Mwanzo 24 >