< Mwanzo 18 >

1 Bwana akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri.
Yahvé lui apparut près des chênes de Mamré, comme il était assis à l'entrée de la tente, dans la chaleur du jour.
2 Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.
Il leva les yeux et regarda, et il vit que trois hommes se tenaient près de lui. Il courut à leur rencontre depuis l'entrée de la tente, se prosterna à terre
3 Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako.
etdit: « Seigneur, si j'ai trouvé grâce à tes yeux, ne te sépare pas de ton serviteur.
4 Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu.
Allez maintenant chercher un peu d'eau, lavez vos pieds, et reposez-vous sous l'arbre.
5 Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.”
Je vais chercher un morceau de pain pour que vous puissiez vous rafraîchir le cœur. Après cela, vous pourrez vous en aller, maintenant que vous êtes venus vers votre serviteur. » Ils ont dit: « Très bien, faites ce que vous avez dit. »
6 Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara, akamwambia, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”
Abraham se précipita dans la tente vers Sara, et dit: « Prépare vite trois seahs de fleur de farine, pétris-la et fais des gâteaux. »
7 Kisha Abrahamu akakimbia kwenda kwenye kundi, akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha.
Abraham courut au troupeau, prit un veau tendre et bon, et le donna au serviteur. Celui-ci s'empressa de le panser.
8 Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.
Il prit du beurre, du lait et le veau qu'il avait habillé, et il le mit devant eux. Il se tint près d'eux sous l'arbre, et ils mangèrent.
9 Wakamuuliza, “Yuko wapi Sara mkeo?” Akasema, “Yuko huko, ndani ya hema.”
Ils lui demandèrent: « Où est Sarah, ta femme? » Il a dit: « Là, dans la tente. »
10 Kisha Bwana akasema, “Hakika nitakurudia tena majira kama haya mwakani na Sara mkeo atakuwa ana mwana.” Sara alikuwa akiwasikiliza kwenye ingilio la hema, lililokuwa nyuma yake.
Il dit: « Je reviendrai certainement chez toi l'année prochaine à peu près à la même époque; et voici que Sarah, ta femme, aura un fils. » Sara entendit à la porte de la tente, qui était derrière lui.
11 Abrahamu na Sara walikuwa wazee tena waliosogea miaka, naye Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake.
Or Abraham et Sara étaient vieux, d'un âge avancé. Sara avait dépassé l'âge de procréer.
12 Hivyo Sara akacheka kimoyomoyo alipokuwa akiwaza, “Baada ya mimi kuwa mkongwe hivi na bwana wangu amezeeka, je, nitaweza kufurahia jambo hili?”
Sara riait en elle-même, disant: « Quand je serai vieille, aurai-je du plaisir, mon seigneur étant vieux aussi? »
13 Ndipo Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, ‘Kweli nitazaa mtoto nami sasa ni mzee?’
Yahvé dit à Abraham: « Pourquoi Sarah a-t-elle ri en disant: « Aurai-je vraiment un enfant quand je serai vieille?
14 Je, kuna jambo lolote gumu lisilowezekana kwa Bwana? Nitakurudia mwakani majira kama haya, naye Sara atakuwa na mwana.”
Y a-t-il quelque chose de trop difficile pour Yahvé? Au temps fixé, je reviendrai vers toi, à la saison qui vient, et Sara aura un fils. »
15 Sara akaogopa kwa kuwa alidanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Bwana akasema, “Ndiyo, ulicheka!”
Alors Sarah le nia, disant: « Je n'ai pas ri », car elle avait peur. Il a dit: « Non, mais vous avez ri. »
16 Wakati watu hao waliposimama ili waondoke, walielekeza nyuso zao Sodoma, Abrahamu akawatoa kitambo kidogo ili awasindikize.
Les hommes se levèrent de là et regardèrent vers Sodome. Abraham alla avec eux pour les voir en chemin.
17 Ndipo Bwana akasema, “Je, nimfiche Abrahamu jambo ninalokusudia kufanya?
Yahvé dit: « Est-ce que je cacherai à Abraham ce que je fais,
18 Hakika Abrahamu atakuwa taifa kubwa na lenye nguvu, kupitia kwake mataifa yote ya dunia yatabarikiwa.
puisque Abraham deviendra une nation grande et puissante, et que toutes les nations de la terre seront bénies en lui?
19 Kwa maana nimemchagua yeye, ili awaongoze watoto wake na jamaa yake kufuata njia ya Bwana, kwa kuwa waadilifu na kutenda haki, ili Bwana atimize ahadi yake kwa Abrahamu.”
Car je l'ai connu, afin qu'il commande à ses enfants et à sa famille après lui, pour qu'ils gardent la voie de l'Éternel, en pratiquant la justice et l'équité, afin que l'Éternel fasse venir sur Abraham ce qu'il a dit de lui. »
20 Basi Bwana akasema, “Kilio dhidi ya Sodoma na Gomora ni kikubwa sana na dhambi yao inasikitisha sana,
Yahvé dit: « Puisque le cri de Sodome et de Gomorrhe est grand, et que leur péché est très grave,
21 kwamba nitashuka nione kama waliyoyatenda ni mabaya kiasi cha kilio kilichonifikia. Kama sivyo, nitajua.”
je descendrai maintenant, et je verrai si leurs actes sont aussi mauvais que les rapports qui me sont parvenus. Si ce n'est pas le cas, je le saurai. »
22 Basi wale watu wakageuka wakaenda kuelekea Sodoma, lakini Abrahamu akabaki amesimama mbele za Bwana.
Les hommes se détournèrent de là et allèrent vers Sodome, mais Abraham se tenait encore devant Yahvé.
23 Ndipo Abrahamu akamsogelea akasema: “Je, utawaangamiza wenye haki na waovu?
Abraham s'approcha, et dit: Veux-tu consumer les justes avec les méchants?
24 Je, ikiwa watakuwepo watu wenye haki hamsini katika mji huo, hivi kweli utauangamiza na wala hutauacha kwa ajili ya hao watu hamsini wenye haki waliomo ndani yake?
Et s'il y a cinquante justes dans la ville? Vas-tu consumer et ne pas épargner la place pour les cinquante justes qui s'y trouvent?
25 Hilo na liwe mbali nawe, kufanya jambo kama hilo, kuwaua wenye haki pamoja na waovu, kuwatendea wenye haki sawasawa na waovu. Iwe mbali nawe! Je, Mwamuzi wa dunia yote hatafanya lililo sawa?”
Qu'il soit loin de toi de faire de telles choses, de tuer les justes avec les méchants, afin que les justes soient comme les méchants. Que cela soit loin de vous. Le Juge de toute la terre ne devrait-il pas faire ce qui est juste? »
26 Bwana akasema, “Kama nikipata watu hamsini wenye haki katika mji wa Sodoma, nitausamehe huo mji wote kwa ajili yao.”
Yahvé dit: « Si je trouve à Sodome cinquante justes dans la ville, j'épargnerai tout le lieu à cause d'eux. »
27 Kisha Abrahamu akasema tena: “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri wa kuzungumza na Bwana, ingawa mimi si kitu bali ni mavumbi na majivu;
Abraham répondit: « Voici, j'ai pris sur moi de parler au Seigneur, bien que je sois poussière et cendre.
28 je, kama hesabu ya wenye haki imepungua watano katika hamsini, utauangamiza huo mji wote kwa ajili ya hao watano waliopungua?” Bwana akamwambia, “Kama nikiwakuta huko watu arobaini na watano, sitauangamiza.”
Et s'il manque cinq des cinquante justes? Détruiras-tu toute la ville par manque de cinq? » Il a dit: « Je ne la détruirai pas si j'y trouve quarante-cinq personnes. »
29 Abrahamu akazungumza naye kwa mara nyingine, “Je, kama huko watapatikana watu arobaini tu?” Akamjibu, “Kwa ajili ya hao arobaini, sitauangamiza.”
Il lui parla encore, et dit: « Et s'il y en a quarante qui se trouvent là? » Il a dit: « Je ne le ferai pas pour l'amour des quarante. »
30 Ndipo akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze. Je, kama huko watakuwepo thelathini tu?” Akajibu, “Sitapaangamiza ikiwa nitawakuta huko watu thelathini.”
Il dit: « Oh, ne laissez pas le Seigneur se mettre en colère, et je parlerai. Et s'il y en a trente trouvés là? » Il a dit: « Je ne le ferai pas si j'en trouve trente là-bas. »
31 Abrahamu akasema, “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri sana kuzungumza na Bwana, je, kama wakipatikana huko watu ishirini tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao ishirini, sitauangamiza.”
Il dit: « Voici, j'ai pris sur moi de parler au Seigneur. Et s'il y en a vingt qui se trouvent là? » Il a dit: « Je ne la détruirai pas à cause des vingt. »
32 Abrahamu akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze tena mara moja tu. Itakuwaje kama watapatikana huko watu kumi tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao kumi, sitauangamiza.”
Il dit: « Oh, que le Seigneur ne se mette pas en colère, et je ne parlerai qu'une fois de plus. Et si l'on en trouve dix là-bas? » Il a dit: « Je ne la détruirai pas à cause des dix. »
33 Bwana alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, akaondoka, naye Abrahamu akarudi nyumbani kwake.
Yahvé s'en alla dès qu'il eut fini de s'entretenir avec Abraham, et Abraham retourna à sa place.

< Mwanzo 18 >