< Mwanzo 12 >

1 Bwana akawa amemwambia Abramu, “Ondoka kutoka nchi yako, uache jamii yako na nyumba ya baba yako, uende hadi nchi nitakayokuonyesha.
And he said Yahweh to Abram go for yourself from land your and from kindred your and from [the] household of father your to the land which I will show you.
2 “Mimi nitakufanya taifa kubwa na nitakubariki, Nitalikuza jina lako, nawe utakuwa baraka.
So I may make you into a nation great and I will bless you and I will make great name your and you be a blessing.
3 Nitawabariki wale wanaokubariki, na yeyote akulaaniye nitamlaani; na kupitia kwako mataifa yote duniani yatabarikiwa.”
So let me bless [those who] bless you and [one who] disdains you I will curse and they will be blessed by you all [the] clans of the earth.
4 Hivyo Abramu akaondoka kama Bwana alivyokuwa amemwambia; naye Loti akaondoka pamoja naye. Wakati Abramu alipoitwa aondoke Harani, alikuwa na miaka sabini na mitano.
And he went Abram just as he had said to him Yahweh and he went with him Lot and Abram [was] a son of five years and seventy year[s] when came out he from Haran.
5 Abramu akamchukua Sarai mkewe pamoja na Loti mwana wa ndugu yake, mali zote walizokuwa nazo pamoja na watu aliokuwa amewapata huko Harani, wakasafiri mpaka nchi ya Kanaani, wakafika huko.
And he took Abram Sarai wife his and Lot [the] son of brother his and all possession[s] their which they had accumulated and the person[s] whom they had acquired in Haran and they went out to go [the] land of towards Canaan and they came [the] land of towards Canaan.
6 Abramu akasafiri katika nchi hiyo akafika huko Shekemu, mahali penye mti wa mwaloni ulioko More. Wakati huo Wakanaani walikuwa wanaishi katika nchi hiyo.
And he passed Abram in the land to [the] place of Shechem to [the] great tree of Moreh and the Canaanite[s] then [was] in the land.
7 Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Hivyo hapa akamjengea madhabahu Bwana aliyekuwa amemtokea.
And he appeared Yahweh to Abram and he said to offspring your I will give the land this and he built there an altar to Yahweh who had appeared to him.
8 Kutoka huko Abramu akasafiri kuelekea kwenye vilima mashariki ya Betheli, naye akapiga hema huko, Betheli ikiwa upande wa magharibi na Ai upande wa mashariki. Huko alimjengea Bwana madhabahu na akaliitia jina la Bwana.
And he moved on from there the hill country towards from [the] east of Beth-el and he pitched (tent his *Q(K)*) Beth-el [was] from [the] west and Ai [was] from [the] east and he built there an altar to Yahweh and he called on [the] name of Yahweh.
9 Kisha Abramu akasafiri kuelekea upande wa Negebu.
And he journeyed Abram going and journeying the south towards.
10 Basi kulikuwako na njaa katika nchi, naye Abramu akashuka kwenda Misri kukaa huko kwa muda, kwa maana njaa ilikuwa kali.
And it was a famine in the land and he went down Abram Egypt towards to sojourn there for [was] heavy the famine in the land.
11 Alipokuwa karibu kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “Ninajua ya kwamba wewe ni mwanamke mzuri wa sura.
And it was just as he drew near to enter Egypt and he said to Sarai wife his here! please I know that [are] a woman beautiful of appearance you.
12 Wakati Wamisri watakapokuona, watasema, ‘Huyu ni mke wake.’ Ndipo wataniua, lakini wewe watakuacha hai.
And it will be that they will see you the Egyptians and they will say [is] wife his this and they will kill me and you they will let live.
13 Sema wewe ni dada yangu, ili nitendewe mema kwa ajili yako, na maisha yangu yatahifadhiwa kwa sababu yako.”
Say please [are] sister my you so that it may go well for me for sake of you and it will live life my on account of you.
14 Abramu alipoingia Misri, Wamisri wakamwona Sarai kuwa ni mwanamke mzuri sana wa sura.
And it was when entered Abram Egypt and they saw the Egyptians the woman that [was] beautiful she very.
15 Maafisa wa Farao walipomwona, wakamsifia kwa Farao; ndipo Sarai akapelekwa kwa nyumba ya mfalme.
And they saw her [the] officials of Pharaoh and they praised her to Pharaoh and she was taken the woman [the] house of Pharaoh.
16 Kwa ajili ya Sarai, Farao akamtendea Abramu mema, naye Abramu akapata kondoo, ngʼombe, punda, ngamia na watumishi wa kiume na wa kike.
And to Abram he did good for sake of her and it be[longed] to him sheep and cattle and [male] donkeys and [male] servants and female servants and female donkeys and camels.
17 Lakini Bwana akamwadhibu Farao na nyumba yake kwa maradhi ya kufisha kwa sababu ya kumchukua Sarai, mke wa Abramu.
And he struck Yahweh - Pharaoh plagues great and house his on [the] matter of Sarai [the] wife of Abram.
18 Ndipo Farao akamwita Abramu, akamuuliza, “Umenifanyia nini? Kwa nini hukuniambia ni mke wako?
And he summoned Pharaoh Abram and he said what? this have you done to me why? not did you tell to me that [was] wife your she.
19 Kwa nini ulisema, ‘Yeye ni dada yangu,’ hata nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa basi, mke wako huyu hapa. Mchukue uende zako!”
Why? did you say [is] sister my she and I took her for myself to a wife and now here! wife your take [her] and go.
20 Kisha Farao akawapa watu wake amri kuhusu Abramu, wakamsindikiza pamoja na mke wake na kila alichokuwa nacho.
And he commanded on him Pharaoh men and they sent away him and wife his and all that [belonged] to him.

< Mwanzo 12 >