< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
Potem mię przywiódł ku drzwiom domu, a oto wody wychodziły z pod progu domu na wschód słońca; bo przednia strona domu była na wschód słońca, a wody one schodziły spodkiem po prawej stronie domu po stronie południowej ołtarza.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
Stamtąd mię wywiódł drogą bramy północnej, i obwiódł mię drogą zewnętrzną do bramy zewnętrznej, drogą, która patrzy na wschód słońca; a oto wody wynikły po prawej stronie.
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
A gdy wychodził on mąż na wschód słońca, w którego ręku była miara, i wymierzył tysiąc łokci, i przewiódł mię przez wodę, przez wodę aż do kostek;
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
Potem wymierzył drugi tysiąc, a przewiódł mię przez wodę, przez wodę aż do kolan; i zaś wymierzył trzeci tysiąc, i przewiódł mię przez wodę aż do biódr.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
A gdy zaś wymierzył tysiąc, był potok, któregom nie mógł przebrnąć; bo były wezbrały wody, wody, które trzeba było przepłynąć, potok, któregom nie mógł przebrnąć.
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
Tedy rzekł do mnie: Widziałżeś, synu człowieczy? I wywiódł mię, i obrócił mię na brzeg onego potoku.
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
A gdym się obrócił, oto na brzegu onego potoku było drzewo bardzo wielkie po obu stronach;
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
I rzekł do mnie: Te wody wychodzą od Galilei pierwszej, a schodzą po równinie, i wchodzą w morze; a gdy do morza wpadną, uzdrowione bywają wody.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
I stanie się, że każda dusza żyjąca, która się płaza, gdziekolwiek przyjdą potoki, żyć będzie, i będzie ryb bardzo wiele, przeto, że gdy przyjdą tam one wody, oczerstwieją, i żyć będą wszędy, kędykolwiek przyjdzie ten potok.
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
Stanie się i to, że staną podle niego rybitwi od Engaddy aż do zdroju Eglaim, tam będą rozciągać sieci; ryb będzie bardzo wiele rozmaitego rodzaju, jako ryb morza wielkiego.
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
Błota jego i kałuże jego nie będą uzdrowine, ale soli oddane będą.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
A nad potokiem wyrośnie na brzegu jego po obu stronach wszelkie drzewo owoce przynoszące, którego liść nie opada, ani owoc jego ustaje, w miesiącach swoich przynosi pierwociny; bo wody jego z świątnicy wychodzą, przetoż owoc jego jest na pokarm, a liście jego na lekarstwo.
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
Tak mówi panujący Pan: Tać jest granica, w której sobie dziedzicznie przywłaszczycie ziemię według dwunastu pokoleń Izraelskich; Józefowi się dostaną dwa sznury.
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
Dziedzicznie, mówię, posiądziecie ją, równie jeden jako drugi, o którą podniosłem rękę moję, że ją dam ojcom waszym; i przypadnie wam ta ziemia w dziedzictwo.
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
Tać jest tedy granica tej ziemi ku stronie północnej, od morza wielkiego, drogą do Hetlonu, kędy wchodzą do Sedad.
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
Emat, Berota, Sybraim, które są między granicą Damaszku i między granicą Emat, wsi pośrednie, które są przy granicy Hawran.
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
A tak będzie granica od morza Chatzar Enon, będzie granica Damaszek, a północna strona na północy, i granica Emat; a toć jest strona północna.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
A strona wschodnia między Hawran i między Damaszkiem i między Galaad i między ziemią Izraelską przy Jordanie; od tej granicy przy morzu wschodniem mierzyć będziecie; a toć jest strona wschodnia.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
A strona południowa na południe od Tamar aż do wód poswarków w Kades, od potoku aż do morza wielkiego; a toć jest strona południwoa na południe.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
Strona zaś zachodnia morze wielkie od granicy aż przeciwko kędy się wchodzi do Emat, tać jest strona zachodnia.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
A tak rozmierzycie sobie tę ziemię, według pokoleń Izraelskich.
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
A gdy ją rozmierzycie, będzie wam w dziedzictwo, i przychodniom, którzyby mieszkali między wami, którzyby spłodzili synów między wami, bo wam będą jako tu zrodzeni między synami Izraelskimi; z wami dziedziczyć będą między pokoleniami Izraelskiemi.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
A w któremkolwiek pokoleniu przychodzień przychodniem będzie, tam mu dacie dziedzictwo jego, mówi panujący Pan.

< Ezekieli 47 >