< Ezekieli 31 >
1 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa tatu, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
La onzième année, au troisième mois, le premier jour du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée, en ces termes:
2 “Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri na makundi yake ya wajeuri: “‘Je, ni nani awezaye kulinganishwa na wewe katika fahari.
« Fils d'homme, dis à Pharaon, roi d'Égypte, et à sa multitude: A qui ressembles-tu dans ta grandeur?
3 Angalia Ashuru, wakati fulani ilikuwa mwerezi huko Lebanoni, ukiwa na matawi mazuri ukitia msitu kivuli; ulikuwa mrefu sana, kilele chake kilipita majani ya miti yote.
Voici, l'Assyrien était un cèdre au Liban. avec de belles branches, et avec une ombre semblable à celle de la forêt, de haute stature; et son sommet était parmi les branches épaisses.
4 Maji mengi yaliustawisha, chemchemi zenye maji mengi ziliufanya urefuke; vijito vyake vilitiririka pale ulipoota pande zote na kupeleka mifereji yake kwenye miti yote ya shambani.
Les eaux l'ont nourri. La profondeur l'a fait grandir. Ses rivières coulaient tout autour de sa plantation. Il a envoyé ses canaux à tous les arbres des champs.
5 Hivyo ukarefuka kupita miti yote ya shambani; vitawi vyake viliongezeka na matawi yake yakawa marefu, yakitanda kwa sababu ya wingi wa maji.
C'est pourquoi sa stature était plus élevée que celle de tous les arbres des champs; et ses rameaux se sont multipliés. Ses branches sont devenues longues à cause des nombreuses eaux, quand il les a étalés.
6 Ndege wote wa angani wakaweka viota kwenye vitawi vyake, wanyama wote wa shambani wakazaana chini ya matawi yake, mataifa makubwa yote yaliishi chini ya kivuli chake.
Tous les oiseaux du ciel ont fait leur nid dans ses branches. Sous ses branches, tous les animaux des champs donnaient naissance à leurs petits. Toutes les grandes nations ont vécu dans son ombre.
7 Ulikuwa na fahari katika uzuri, ukiwa na matawi yaliyotanda, kwa kuwa mizizi yake ilikwenda chini mpaka kwenye maji mengi.
Ainsi, elle était belle dans sa grandeur, dans la longueur de ses branches; car sa racine était près de nombreuses eaux.
8 Mierezi katika bustani ya Mungu haikuweza kushindana nao, wala misunobari haikuweza kulingana na vitawi vyake, wala miaramoni haikulinganishwa na matawi yake, wala hakukuwa na mti katika bustani ya Mungu wa kulinganisha na uzuri wake.
Les cèdres du jardin de Dieu n'ont pu le cacher. Les cyprès n'étaient pas comme ses branches. Les pins n'étaient pas comme ses branches; et aucun arbre du jardin de Dieu ne lui ressemblait dans sa beauté.
9 Niliufanya kuwa mzuri ukiwa na matawi mengi, ulionewa wivu na miti yote ya Edeni katika bustani ya Mungu.
Je l'ai embelli par la multitude de ses branches, de sorte que tous les arbres de l'Eden, qui étaient dans le jardin de Dieu, l'enviaient.
10 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulikuwa mrefu sana, kilele chake kikiwa juu ya majani manene ya miti na kwa sababu ulikuwa na kiburi cha urefu wake,
C'est pourquoi, ainsi parle le Seigneur Yahvé Parce qu'il s'est élevé dans sa stature, qu'il a placé son sommet parmi les branches épaisses, et que son cœur s'est élevé dans sa hauteur,
11 niliutia mikononi mwa mtawala wa mataifa, ili yeye aushughulikie sawasawa na uovu wake. Nikaukatilia mbali,
je le livrerai entre les mains du puissant des nations. Il lui fera du mal. Je l'ai chassé à cause de sa méchanceté.
12 nayo mataifa mageni yaliyo makatili sana yaliukata huo mti na kuuacha. Matawi yake yalianguka juu ya milima na kwenye mabonde yote, vitawi vyake vikavunjika na kusambaa katika makorongo yote ya nchi. Mataifa yote ya duniani yakaondoka kutoka kwenye kivuli chake na kuuacha.
Les étrangers, les tyrans des nations, l'ont retranché et abandonné. Ses branches sont tombées sur les montagnes et dans toutes les vallées, et ses rameaux sont brisés par tous les cours d'eau du pays. Tous les peuples de la terre sont descendus de son ombre et l'ont abandonné.
13 Ndege wote wa angani wakakaa kwenye ule mti ulioanguka na wanyama pori wote wakakaa katikati ya vitawi vyake.
Tous les oiseaux du ciel habiteront sur sa ruine, et tous les animaux des champs se tiendront sur ses branches,
14 Kamwe hakutakuwa na miti mingine kando ya hayo maji itakayorefuka zaidi ya huo, vilele vyake vikiwa juu ya majani yote ya miti. Hakuna miti mingine, hata kama imekunywa maji vizuri namna gani, itakayofikia urefu huo. Yote mwisho wake ni kifo, na kuingia ardhini, kama vile ilivyo kwa wanadamu, pamoja na wale waendao shimoni.
si bien qu'aucun de tous les arbres qui sont près des eaux ne s'élève dans sa stature, et ne pose sa cime parmi les rameaux épais. Leurs puissants ne se dressent pas sur leur hauteur, même tous ceux qui boivent de l'eau; car ils sont tous livrés à la mort, dans les parties inférieures de la terre, parmi les enfants des hommes, avec ceux qui descendent dans la fosse.''
15 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mwerezi uliposhushwa chini kaburini nilizifunika chemchemi zenye maji mengi kwa maombolezo: Nilivizuia vijito vyake na wingi wa maji yake nikauzuia. Kwa sababu yake niliivika Lebanoni huzuni, nayo miti yote ya shambani ikanyauka. (Sheol )
« Le Seigneur Yahvé dit: « Le jour où il est descendu au séjour des morts, j'ai provoqué un deuil. J'ai couvert l'abîme pour lui, et j'ai retenu ses fleuves. Les grandes eaux ont été arrêtées. J'ai fait pleurer le Liban à cause de lui, et tous les arbres des champs se sont évanouis à cause de lui. (Sheol )
16 Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa kishindo cha kuanguka kwake wakati nilipoushusha chini kaburini pamoja na wale washukao shimoni. Ndipo miti yote ya Edeni, miti iliyo bora kuliko yote na iliyo mizuri sana ya Lebanoni, miti yote ile iliyokunywa maji vizuri, ilifarijika hapa duniani. (Sheol )
J'ai fait trembler les nations au bruit de sa chute, quand je l'ai précipité dans le séjour des morts avec ceux qui descendent dans la fosse. Tous les arbres d'Éden, les meilleurs et les plus beaux du Liban, tous ceux qui boivent de l'eau, ont été consolés dans les parties inférieures de la terre. (Sheol )
17 Wale walioishi katika kivuli chake, wale walioungana naye miongoni mwa mataifa, nao pia walikuwa wamezikwa pamoja naye, wakiungana na wale waliouawa kwa upanga. (Sheol )
Ils sont aussi descendus au séjour des morts avec lui, vers ceux qui sont tués par l'épée; oui, ceux qui étaient son bras, qui vivaient sous son ombre au milieu des nations. (Sheol )
18 “‘Ni miti ipi ya Edeni inayoweza kulinganishwa nawe kwa fahari na utukufu? Hata hivyo, wewe pia, utashushwa chini pamoja na miti ya Edeni mpaka kuzimu, utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga. “‘Huyu ni Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri, asema Bwana Mwenyezi.’” ()
"'A qui ressembles-tu ainsi, en gloire et en grandeur, parmi les arbres d'Eden? Mais tu seras descendu avec les arbres d'Eden dans les régions inférieures de la terre. Tu seras couché au milieu des incirconcis, avec ceux qui sont tués par l'épée. "'Voici Pharaon et toute sa multitude,' dit le Seigneur Yahvé. »