< Ezekieli 3 >
1 Naye akaniambia, “Mwanadamu, kula kile kilichoko mbele yako, kula huu ukurasa wa kitabu, kisha uende ukaseme na nyumba ya Israeli.”
He said to me, “Son of man, what you have found, eat. Eat this scroll, then go speak to the house of Israel.”
2 Ndipo nikafungua kinywa changu, naye akanilisha ule ukurasa wa kitabu.
So I opened my mouth, and he fed me that scroll.
3 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, kula ukurasa huu wa kitabu ninaokupa ujaze tumbo lako.” Kwa hiyo nikaula, ulikuwa mtamu kama asali kinywani mwangu.
He said to me, “Son of man, feed your belly and fill your stomach with this scroll that I have given to you!” So I ate it, and it was as sweet as honey in my mouth.
4 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, sasa nenda katika nyumba ya Israeli ukaseme nao maneno yangu.
Then he said to me, “Son of man, go to the house of Israel and speak my words to them.
5 Hukutumwa kwa taifa lenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu, bali kwa nyumba ya Israeli.
For you are not being sent to a people of strange speech or difficult language, but to the house of Israel—
6 Sikukutuma kwa mataifa mengi yenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu ambao maneno yao hutayaelewa. Hakika ningekutuma kwa watu hao, wangekusikiliza.
not to many peoples of strange speech or a difficult language, whose words you cannot understand. Surely if I sent you to them, they would have listened to you.
7 Lakini nyumba ya Israeli haitakusikiliza kwa kuwa hawako radhi kunisikiliza mimi, kwa kuwa nyumba yote ya Israeli ni wenye vipaji vya nyuso vigumu na mioyo ya ukaidi.
But the house of Israel will not be willing to listen to you, for they are not willing to listen to me. So all the house of Israel is strong browed and hard hearted.
8 Tazama nimefanya uso wako mgumu dhidi ya nyuso zao na kipaji cha uso wako kigumu dhidi ya vipaji vya nyuso zao.
Behold! I have made your face as stubborn as their faces and your brow as hard as their brows.
9 Kama vile almasi ilivyo ngumu kuliko gumegume, ndivyo nilivyokifanya kipaji cha uso wako. Usiwaogope wala usiwahofu, ijapokuwa ni nyumba ya kuasi.”
I have made your brow like a diamond, harder than flint! Do not fear them or be discouraged by their faces, since they are a rebellious house.”
10 Naye akaniambia, “Mwanadamu, sikiliza kwa makini na uyatie moyoni mwako maneno yote nitakayosema nawe.
Then he said to me, “Son of man, all the words that I announce to you—take them into your heart and hear them with your ears!
11 Kisha nenda kwa watu wa taifa lako walio uhamishoni, ukaseme nao. Waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenyezi asemavyo,’ kwamba watasikiliza au hawatasikiliza.”
Then go to the captives, to your people, and speak to them. Say to them, 'This is what the Lord Yahweh says,' whether they will listen or not.”
12 Ndipo Roho akaniinua, nikasikia sauti kubwa nyuma yangu ya ngurumo. (Utukufu wa Bwana na utukuzwe katika mahali pa makao yake!)
Then the Spirit lifted me up, and I heard behind me the sound of a great earthquake: “Blessed be the glory of Yahweh from his place!”
13 Ilikuwa ni sauti ya mabawa ya wale viumbe hai yakisuguana moja kwa jingine, sauti kama ya ngurumo.
It was the sound of the wings of the living creatures as they touched one another, and the sound of the wheels that were with them, and the sound of a great earthquake.
14 Ndipo Roho aliponiinua na kunipeleka mbali. Nikaenda nikiwa na uchungu na hasira moyoni mwangu, nao mkono wa Bwana ukiwa juu yangu.
The Spirit lifted me up and took me away, and I went with bitterness in my spirit's rage, for the hand of Yahweh was powerfully pressing on me!
15 Nikafika kwa wale watu waliokuwa uhamishoni huko Tel-Abibu karibu na Mto Kebari. Nikakaa miongoni mwao kwa muda wa siku saba, nikiwa nimejawa na mshangao.
So I went to the captives at Tel Aviv who lived along the Kebar Canal, and I stayed there among them for seven days, overwhelmed in amazement.
16 Mwishoni mwa hizo siku saba neno la Bwana likanijia kusema:
Then it happened after seven days that the word of Yahweh came to me, saying,
17 “Mwanadamu, nimekufanya uwe mlinzi wa nyumba ya Israeli, kwa hiyo sikia neno nisemalo, ukawape onyo litokalo kwangu.
“Son of man, I have made you a watchman for the house of Israel, so listen to the word from my mouth, and give them my warning.
18 Nimwambiapo mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ na wewe usipomwonya mtu huyo au kumshauri aache njia zake mbaya ili kuokoa maisha yake, huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake na damu yake nitaidai mkononi mwako.
When I say to the wicked, 'You will surely die' and you do not warn him or speak a warning to the wicked about his evil deeds so he might live—the wicked one will die for his sin, but I will require his blood from your hand.
19 Lakini ukimwonya mtu mwovu naye akakataa kuacha uovu wake na njia zake mbaya, atakufa katika dhambi yake, lakini wewe utakuwa umejiokoa nafsi yako.
But if you warn the wicked, and he does not turn from his wickedness or from his wicked deeds, then he will die for his sin, but you will have rescued your own life.
20 “Tena, mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda maovu, nami nikaweka kikwazo mbele yake mtu huyo atakufa. Kwa kuwa hukumwonya, atakufa katika dhambi yake. Mambo ya haki aliyotenda, hayatakumbukwa, damu yake nitaidai mkononi mwako.
If a righteous man turns from his righteousness and acts unjustly, and I set a stumbling block before him, he will die. Because you did not warn him, he will die in his sin, and I will not call to mind the righteous deeds that he performed, but I will require his blood from your hand.
21 Lakini ukimwonya mwenye haki asitende dhambi na akaacha kutenda dhambi, hakika ataishi kwa sababu alipokea maonyo na utakuwa umejiokoa nafsi yako.”
But if you warn the righteous man to stop sinning so that he no longer sins, he will surely live since he was warned; and you will have rescued your own life.”
22 Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu huko, naye akaniambia, “Simama uende mpaka sehemu tambarare, nami nitasema nawe huko.”
So the hand of Yahweh was on me there, and he said to me, “Arise! Go out into the plain, and I will speak with you there!”
23 Kwa hiyo niliinuka nikaenda mpaka mahali pa tambarare. Utukufu wa Bwana ulikuwa umesimama huko, kama utukufu ule niliouona kando ya Mto Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
I arose and went out into the plain, and there the glory of Yahweh was staying, like the glory that I had seen beside the Kebar Canal; so I fell on my face.
24 Ndipo Roho akaja ndani yangu akanisimamisha kwa miguu yangu. Akasema nami akaniambia: “Nenda ukajifungie ndani ya nyumba yako.
The Spirit came to me and stood me up on my feet; and he spoke with me, and said to me, “Go and shut yourself up within your house,
25 Nawe, ee mwanadamu, watakufunga kwa kamba, watakufunga ili usiweze kutoka na kuwaendea watu.
for now, son of man, they will place ropes upon you and tie you so you cannot go out among them.
26 Nitaufanya ulimi wako ushikamane kwenye kaa la kinywa chako, ili uwe kimya usiweze kuwakemea, wajapokuwa ni nyumba ya kuasi.
I will make your tongue stick to the roof of your mouth, so you will be mute, and you will not be able to rebuke them, since they are a rebellious house.
27 Lakini nitakaposema nawe, nitafungua kinywa chako nawe utawaambia, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo.’ Yeyote atakayesikiliza na asikilize, na yeyote atakayekataa na akatae; kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi.
But when I speak with you, I will open your mouth so you will say to them, 'This is what the Lord Yahweh says.' The one who will hear will hear; the one who will not listen will not listen, for they are a rebellious house!”