< Ezekieli 21 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
2 “Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
O son of humankind set face your against Jerusalem and prophesy against sanctuaries and prophesy against [the] land of Israel.
3 uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
And you will say to [the] land of Israel thus he says Yahweh here I [am] against you and I will bring out sword my from sheath its and I will cut off from you [the] righteous and [the] wicked.
4 Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
Because that I have cut off from you [the] righteous and [the] wicked therefore it will go forth sword my from sheath its against all flesh from [the] south [the] north.
5 Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
And they will know all flesh that I Yahweh I have brought out sword my from sheath its not it will go back again.
6 “Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
And you O son of humankind groan with breaking of loins and with bitterness you will groan to eyes their.
7 Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
And it will be that they will say to you concerning what? [are] you groaning and you will say because of a report that [it is] coming and it will melt every heart and they will hang limp every pair of hands and it will grow faint every spirit and all knees they will go water there! [it is] coming and it will happen [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
8 Neno la Bwana likanijia, kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
9 “Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
O son of humankind prophesy and you will say thus he says [the] Lord say a sword a sword it has been sharpened and also [is] polished.
10 umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
So as to slaughter a slaughter it has been sharpened so as be for it lightning it has been polished or we will rejoice [the] scepter of son my [is] rejecting every tree.
11 “‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
And someone gave it to polish [it] to grasp [it] in the palm it it has been sharpened a sword and it it has been polished to put it in [the] hand of [one who] slays.
12 Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
Cry out and wail O son of humankind for it it has come on people my it [is] on all [the] princes of Israel thrown to [the] sword they have been with people my therefore slap a thigh.
13 “‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
For it has been tested and what? if also a scepter rejecting not it will be [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
14 “Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
And you O son of humankind prophesy and strike palm to palm so it may be doubled a sword a third a sword of [those] slain it [is] a sword of [the] slain great which surrounds them.
15 Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
So as - to melt a heart and [may be] many the stumblings at all gates their I have set a slaughter of a sword alas! made for lightning wrapped for slaughtering.
16 Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
Be sharp go to [the] right cause to set go to [the] left where? [is] face your set.
17 Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
And also I I will strike palm my to palm my and I will give rest to rage my I Yahweh I have spoken.
18 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
19 “Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
And you O son of humankind make for yourself - two roads to come [the] sword of [the] king of Babylon from a land one they will go out both of them and a monument make at [the] beginning of [the] road of a city make [it].
20 Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
A road you will make to come a sword Rabbah of [the] people of Ammon and Judah in Jerusalem fortified.
21 Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
For he has stopped [the] king of Babylon to [the] mother of the road at [the] beginning of [the] two the roads to divine divination he has shaken the arrows he has enquired by the teraphim he has looked at the liver.
22 Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
In right [hand] his it was - the divination Jerusalem to set up battering-rams to open a mouth for shattering to raise a sound with a war cry to set up battering-rams on [the] gates to pour out a mound to build a siege-wall.
23 Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
And it will be to them (as divines *Q(k)*) falsehood in view their oaths of oaths [belong] to them and it [will] bring to remembrance iniquity to be seized.
24 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
Therefore thus he says [the] Lord Yahweh because brought to remembrance you iniquity your because were uncovered transgressions your to be seen sins your in all practices your because have been remembered you by the hand you will be seized.
25 “‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
And you O profane [one] wicked prince of Israel whom it has come day his at a time of punishment of [the] end.
26 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
Thus he says [the] Lord Yahweh to remove the turban and to lift off the crown this not this the lowly exalt and the exalted to bring low.
27 Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
A ruin a ruin a ruin I will make it also this not it will be until comes [the one] whom [belongs] to him the judgment and I will give it.
28 “Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
And you O son of humankind prophesy and you will say thus he says [the] Lord Yahweh concerning [the] people of Ammon and concerning reproach their and you will say a sword a sword [is] drawn for slaughter [is] polished to contain on account of lightning.
29 Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
When see for you falsehood when divine for you falsehood to give you to [the] necks of [those] profaned of wicked [people] whom it has come day their at a time of punishment of [the] end.
30 Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
Put back into sheath its in [the] place where you were created in [the] land of origins your I will judge you.
31 Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
And I will pour out on you indignation my with [the] fire of wrath my I will blow on you and I will give you in [the] hand of men brutish craftsmen of destruction.
32 Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”
For the fire you will become fuel blood your it will be in [the] midst of the land not you will be remembered for I Yahweh I have spoken.

< Ezekieli 21 >