< Ezekieli 17 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahvé me fut adressée, en ces mots:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo.
Fils d'homme, raconte une énigme, et dis une parabole à la maison d'Israël.
3 Waambie hivi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi,
Tu diras: « Le Seigneur Yahvé dit: Un grand aigle aux grandes ailes et aux longues plumes, plein de plumes de diverses couleurs, vint au Liban et prit la cime du cèdre.
4 akakwanyua ncha yake na kuichukua mpaka nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.
Il coupa le plus haut de ses jeunes rameaux, et le transporta dans un pays de trafic. Il le planta dans une ville de marchands.
5 “‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi,
"''Il prit aussi une partie de la semence du pays et la planta dans une terre fertile. Il la plaça près de nombreuses eaux. Il la plaça comme un saule.
6 nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.
Il grandit et devint une vigne étalée, de petite taille, dont les branches étaient tournées vers lui, et dont les racines étaient sous lui. Elle devint donc une vigne, produisit des branches et poussa des rameaux.
7 “‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa na kutanda matawi yake kumwelekea kwa ajili ya kupata maji.
"''Il y avait aussi un autre grand aigle, avec de grandes ailes et beaucoup de plumes. Voici, cette vigne a plié ses racines vers lui, et elle a poussé ses rameaux vers lui, depuis le sol où elle était plantée, afin qu'il l'arrose.
8 Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’
Elle était plantée dans un bon sol, près de beaucoup d'eaux, afin qu'elle produise des branches et qu'elle porte du fruit, pour être une bonne vigne. »''
9 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, utastawi? Je, hautangʼolewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuungʼoa na mizizi yake.
Dis: « Le Seigneur Yahvé dit: « Prospère-t-il? N'arrachera-t-il pas ses racines et ne coupera-t-il pas ses fruits, pour qu'il se dessèche, pour que toutes ses feuilles fraîches et printanières se flétrissent? Ce n'est pas par un bras fort ou par un grand nombre de personnes qu'elle pourra être relevée de ses racines.
10 Hata kama utapandwa pengine, Je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani, hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’”
Oui, voici, étant plantée, prospérera-t-elle? Ne se desséchera-t-elle pas quand le vent d'orient la touchera? Elle se flétrira dans le sol où elle a poussé. »'"
11 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahvé me fut adressée en ces termes:
12 “Waambie nyumba hii ya kuasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alikwenda Yerusalemu na kumchukua mfalme na watu maarufu, akarudi nao na kuwaleta mpaka Babeli.
« Dis maintenant à la maison rebelle: « Ne savez-vous pas ce que signifient ces choses? ». Dis-leur: Voici, le roi de Babylone est venu à Jérusalem, il a pris son roi et ses chefs, et les a emmenés avec lui à Babylone.
13 Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi,
Il prit l'un des descendants royaux, et fit alliance avec lui. Il le fit aussi jurer, et il enleva les puissants du pays,
14 ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake.
afin d'abaisser le royaume, de l'empêcher de se relever, et de le faire subsister en respectant son alliance.
15 Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?
Mais il s'est rebellé contre lui en envoyant ses ambassadeurs en Égypte, pour qu'ils lui donnent des chevaux et un peuple nombreux. Prospérera-t-il? Celui qui fait de telles choses échappera-t-il? Viendra-t-il à bout de l'alliance, et échappera-t-il quand même?
16 “‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha katika kiti cha enzi, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake.
« Je suis vivant, dit le Seigneur Yahvé, dans le lieu où habite le roi qui l'a fait roi, dont il a méprisé le serment et rompu l'alliance, il mourra avec lui au milieu de Babylone.
17 Farao na jeshi lake kubwa, na wingi wake wa watu hawataweza kusaidia chochote katika vita, wakati watakapozungukwa na jeshi ili kukatilia mbali maisha ya watu wengi.
Pharaon, avec sa puissante armée et sa grande troupe, ne l'aidera pas dans la guerre, quand on élèvera des monticules et qu'on construira des forts pour exterminer de nombreuses personnes.
18 Alidharau kiapo kwa kuvunja Agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.
Car il a méprisé le serment en rompant l'alliance; et voici, il avait donné sa main, et pourtant il a fait toutes ces choses. Il ne s'échappera pas.
19 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, nitaleta juu ya kichwa chake kiapo changu, alichokidharau na Agano langu lile alilolivunja.
C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: 'Je suis vivant! Je ferai retomber sur sa tête mon serment qu'il a méprisé et mon alliance qu'il a rompue.
20 Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta mpaka Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu.
J'étendrai mon filet sur lui, et il sera pris dans mon piège. Je l'emmènerai à Babylone, et là j'entrerai en jugement avec lui pour la faute qu'il a commise envers moi.
21 Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesema.
Tous ses fugitifs, dans toutes ses bandes, tomberont par l'épée, et ceux qui resteront seront dispersés à tout vent. Alors vous saurez que c'est moi, Yahvé, qui l'ai dit ».
22 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kwenye kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana.
« Le Seigneur Yahvé dit: 'Je prendrai aussi une partie de la cime du cèdre et je la planterai. J'arracherai de la cime de ses jeunes rameaux un rameau tendre, et je le planterai sur une montagne élevée et haute.
23 Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina wataweka viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake.
Je le planterai sur la montagne élevée d'Israël; il produira des rameaux, il portera du fruit, et il sera un bon cèdre. Des oiseaux de toute espèce habiteront à l'ombre de ses branches.
24 Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Bwana ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi. “‘Mimi Bwana nimesema, nami nitatenda.’”
Tous les arbres des champs sauront que moi, Yahvé, j'ai fait tomber le grand arbre, j'ai élevé le petit arbre, j'ai desséché l'arbre vert, et j'ai fait prospérer l'arbre sec. "'Moi, Yahvé, j'ai parlé et je l'ai fait.'"