< Ezekieli 12 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
2 “Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
O son of humankind in [the] midst of [the] house of rebellion you [are] dwelling whom eyes [belong] to them to see and not they see ears [belong] to them to hear and not they hear for [are] a house of rebellion they.
3 “Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.
And you O son of humankind prepare for yourself baggage of exile and go into exile by day to eyes their and you will go into exile from place your to a place another to eyes their perhaps they will see for [are] a house of rebellion they.
4 Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.
And you will bring out baggage your like baggage of exile by day to eyes their and you you will go out in the evening to eyes their like goings out of exile.
5 Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
To eyes their dig yourself in the wall and you will bring out in it.
6 Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
To eyes their on a shoulder you will lift [it] up in the darkness you will bring [it] out face your you will cover and not you will see the land for a sign I have made you to [the] house of Israel.
7 Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
And I did so just as I was commanded baggage my I brought out like baggage of exile by day and in the evening I dug myself in the wall by hand in the darkness I brought [it] out on a shoulder I lifted [it] up to eyes their.
8 Asubuhi neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me in the morning saying.
9 “Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
O son of humankind ¿ not have they said to you [the] house of Israel [the] house of rebellion what? [are] you doing.
10 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’
Say to them thus he says [the] Lord Yahweh [is] the prince the oracle this in Jerusalem and all [the] house of Israel who they [are] in midst of them.
11 Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka.
Say I [am] sign your just as I have done so it will be done to them in exile in captivity they will go.
12 “Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi.
And the prince who [is] in midst of them to a shoulder he will lift up in the darkness so he may go out in the wall they will dig to bring out in it face his he will cover because that not he will see to the eye he the land.
13 Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
And I will spread net my over him and he will be caught in hunting net my and I will bring him Babylon towards [the] land of [the] Chaldeans and it not he will see and there he will die.
14 Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa.
And all [those] who [are] around him (help his *Q(K)*) and all troops his I will disperse to every wind and a sword I will draw after them.
15 “Wao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
And they will know that I [am] Yahweh when scatter I them among the nations and I will disperse them among the lands.
16 Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
And I will leave over some of them people of number from [the] sword from [the] famine and from [the] pestilence so that they may recount all abominations their among the nations where they have gone there and they will know that I [am] Yahweh.
17 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
18 “Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako.
O son of humankind food your in quaking you will eat and water your in trembling and in anxiety you will drink.
19 Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
And you will say to [the] people of the land thus he says [the] Lord Yahweh of [the] inhabitants of Jerusalem concerning [the] land of Israel food their in anxiety they will eat and water their in horror they will drink so that it may be desolate land its from fullness its from [the] violence of all the inhabitants in it.
20 Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.’”
And the cities inhabited they will be waste and the land a desolation it will become and you will know that I [am] Yahweh.
21 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
22 “Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’
O son of humankind what? [is] the proverb this to you on [the] land of Israel saying they are long the days and it perishes every vision.
23 Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa.
Therefore say to them thus he says [the] Lord Yahweh I will make to cease the proverb this and not people will use as a proverb it again in Israel that except speak to them they have drawn near the days and [the] matter of every vision.
24 Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli.
For not it will be again any vision of worthlessness and divination of flattery in [the] midst of [the] house of Israel.
25 Lakini Mimi Bwana nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mwenyezi.’”
For - I Yahweh I will speak which I will speak a word so it may be done not it will be postponed again for in days your O house of rebellion I will speak a word and I will do it [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
26 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
27 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
O son of humankind there! [the] house of Israel [are] saying the vision which he [is] seeing [is] of days many and of times distant he [is] prophesying.
28 “Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mwenyezi.’”
Therefore say to them thus he says [the] Lord Yahweh not it will be postponed again all words my [that] which I will speak a word so it may be done [the] utterance of [the] Lord Yahweh.

< Ezekieli 12 >