< Ezekieli 11 >

1 Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
And it lifted up me a spirit and it brought me to [the] gate of [the] house of Yahweh eastern which faces east-ward and there! [were] at [the] entrance of the gate twenty and five man and I saw in midst of them Jaazaniah [the] son of Azzur and Pelatiah [the] son of Benaiah [the] leaders of the people.
2 Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
And he said to me O son of humankind these [are] the people who plan wickedness and who counsel counsel of evil in the city this.
3 Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
Who say not [is] in [the] near [future] to build houses it [is] the pot and we [are] the meat.
4 Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
Therefore prophesy on them prophesy O son of humankind.
5 Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
And it fell on me [the] spirit of Yahweh and he said to me say thus he says Yahweh thus you have said O house of Israel and [the] thoughts of spirit your I I know it.
6 Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
You have multiplied slain [ones] your in the city this and you have filled streets its [the] slain.
7 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
Therefore thus he says [the] Lord Yahweh slain [ones] your which you have put in [the] midst of it they [are] the meat and it [is] the pot and you he will bring out from [the] midst of it.
8 Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
A sword you have feared and a sword I will bring on you [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
9 Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
And I will bring out you from [the] midst of it and I will give you in [the] hand of strangers and I will bring about on you judgments.
10 Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
By the sword you will fall on [the] territory of Israel I will judge you and you will know that I [am] Yahweh.
11 Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
It not it will become for you a pot and you you will become in [the] midst of it meat to [the] border of Israel I will judge you.
12 Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
And you will know that I [am] Yahweh whom in statutes my not you have walked and judgments my not you have done and according to [the] judgments of the nations which [are] around you you have done.
13 Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
And it was when prophesied I and Pelatiah [the] son of Benaiah he died and I fell on face my and I cried out a voice great and I said alas! O Lord Yahweh complete destruction [are] you? making with [the] remnant of Israel.
14 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
15 “Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
O son of humankind brothers your brothers your [the] people of redemption your and all [the] house of Israel all of it whom they said to them [the] inhabitants of Jerusalem be distant from with Yahweh to us it it has been given the land to a possession.
16 “Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
Therefore say thus he says [the] Lord Yahweh that I have removed far away them among the nations and that I have scattered them among the lands and I have become for them a sanctuary a little in the lands where they have gone there.
17 “Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
Therefore say thus he says [the] Lord Yahweh and I will gather you from the peoples and I will gather you from the lands which you have been scattered among them and I will give to you [the] land of Israel.
18 “Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
And they will come there towards and they will remove all detestable things its and all abominations its from it.
19 Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
And I will give to them a heart one and a spirit new I will put in inner being your and I will remove [the] heart of stone from flesh their and I will give to them a heart of flesh.
20 Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
So that in statutes my they may walk and judgments my they may keep and they will do them and they will become for me a people and I I will become for them God.
21 Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
And to [the] heart of detestable things their and abominations their heart their [is] going conduct their on own head their I will requite [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
22 Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
And they lifted up the cherubim wings their and the wheels [were] close by them and [the] glory of [the] God of Israel [was] above them from to above.
23 Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
And it went up [the] glory of Yahweh from over [the] middle of the city and it stood still over the mountain which [was] from [the] east of the city.
24 Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
And a spirit it lifted up me and it brought me Chaldea towards to the exile[s] in the vision by [the] spirit of God and it went up from on me the vision which I had seen.
25 nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.
And I spoke to the exile[s] all [the] words of Yahweh which he had shown me.

< Ezekieli 11 >