< Ezekieli 10 >

1 Nikatazama, nikaona juu ya ile nafasi iliyokuwa juu ya vichwa vya wale makerubi kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi.
I widziałem; a oto na rozpostarciu, które było nad głową Cherubinów, jakoby kamień szafirowy, na wejrzeniu jako podobieństwo stolicy, ukazało się nad nimi.
2 Bwana akamwambia mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, “Ingia katikati ya yale Magurudumu yaliyo chini ya makerubi. Ukaijaze mikono yako makaa ya mawe ya moto kutoka katikati ya makerubi na uyatawanye juu ya mji.” Nilipokuwa nikiangalia, akaingia ndani.
Tedy rzekł do onego męża odzianego szatą lnianą, mówiąc: Wnijdź między koła pod Cherubinów, a napełń ręce swe węglem ognistym z pośród Cherubinów, i rozrzuć po mieście. I wszedł przed oczyma memi.
3 Basi wale makerubi walikuwa wamesimama upande wa kusini wa Hekalu wakati yule mtu alipoingia ndani, wingu likaujaza ule ukumbi wa ndani.
(A Cherubowie stali po prawej stronie domu, gdy wchodził on mąż, a obłok napełnił sień wnętrzną.
4 Kisha utukufu wa Bwana ukainuka kutoka juu ya wale makerubi ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Wingu likajaza Hekalu, nao ukumbi ukajawa na mngʼao wa utukufu wa Bwana.
Bo gdy się była podniosła chwała Pańska z Cherubinów, ku progowi domu, tedy napełniony był dom obłokiem, a sień napełniona była jasnością chwały Pańskiej;
5 Sauti ya mabawa ya wale makerubi ingeweza kusikika mpaka kwenye ukumbi wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi wakati anapoongea.
A szum skrzydeł Cherubinów słyszany był aż do sieni zewnętrznej, jako głos Boga wszechmocnego, gdy mówi.)
6 Bwana alipomwamuru yule mtu aliyevaa nguo za kitani akisema, “Chukua moto toka katikati ya magurudumu, kutoka katikati ya makerubi,” yule mtu aliingia ndani akasimama pembeni mwa gurudumu.
Gdy tedy rozkazał onemu mężowi odzianemu w szatę lnianą, mówiąc: Weźmij ognia z pośrodku kół, z pośrodku Cherubinów: wszedł i stanął podle kół.
7 Ndipo mmoja wa wale makerubi akanyoosha mkono wake kwenye moto uliokuwa katikati yao. Akachukua baadhi ya moto na kuutia mikononi mwa yule mtu aliyevaa mavazi ya kitani, naye akaupokea akatoka nje.
Tedy wyciągnął Cherubin jeden rękę swą w pośród Cherubinów do onego ognia, który był w pośrodku Cherubinów, a wziąwszy podał go w rękę onego odzianego szatą lnianą, który wziąwszy go wyszedł.
8 (Chini ya mabawa ya makerubi paliweza kuonekana kitu kilichofanana na mikono ya mwanadamu.)
Bo się ukazało na onych Cherubinach podobieństwo ręki człowieczej pod skrzydłami ich.
9 Nikatazama, nikaona magurudumu manne kando ya makerubi, moja kando ya kila kerubi. Magurudumu hayo yalimetameta kama kito cha zabarajadi.
Potemem wejrzał, a oto cztery koła podle Cherubinów, koło jedno podle jednego Cherubina, a tak każde koło podle każdego Cherubina, a podobieństwo kół jako barwa kanienia Tarsys;
10 Kule kuonekana kwake, yote manne yalifanana kila gurudumu lilikuwa kama linazunguka ndani ya lingine.
A na wejrzeniu miały jednakie podobieństwa one koła, jakoby było koło w pośrodku koła.
11 Yalipozunguka, yalikwenda kokote katika pande nne walikoelekea wale makerubi. Magurudumu hayakugeuka wakati makerubi yalipokwenda. Makerubi walikwenda upande wowote kichwa kilikoelekea pasipo kugeuka walipokuwa wakienda.
Gdy chodziły, na cztery strony swoje chodziły; nie uchylały się, gdy szły, ale do onego miejsca, do którego się wódź obracał, za nim szły; nie uchylały się, gdy szły.
12 Miili yao yote, pamoja na migongo yao, mikono na mabawa yao yote yalikuwa yamejaa macho kabisa kama yalivyokuwa yale magurudumu yao manne.
A wszytko ciało ich, i grzbiety ich, i ręce ich, i skrzydła ich, także i koła pełne były oczów około onych samych czterech, i kół ich.
13 Nikasikia magurudumu yakiitwa, “Magurudumu ya kisulisuli.”
A koła one nazwał okręgiem, gdziem ja słyszał.
14 Kila mmoja wa wale makerubi alikuwa na nyuso nne: Uso mmoja ulikuwa kama vile wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa nne ulikuwa wa tai.
A każde zwierzę miało cztery twarze; twarz pierwsza była twarz Cherubinowa, druga twarz była twarz człowiecza, trzecia była twarz lwia, a czwarta była twarz orla.
15 Kisha makerubi wakapaa juu. Hawa ndio wale viumbe walio hai niliowaona kando ya Mto Kebari.
I podnieśli się Cherubinowie. Toć są one zwierzęta, którem widział nad rzeką Chebar.
16 Wakati makerubi walipokwenda, magurudumu yaliyoko kando yao yalikwenda na wakati makerubi walipotanda mabawa yao wapate kupaa juu kutoka ardhi, magurudumu yale hayakuondoka pembeni mwao.
A gdy chodzili Cherubinowie, chodziły i koła podle nich; a gdy ponosili Cherubinowie skrzydła swoje, aby się wzbili od ziemi, nie odwracały się też koła od nich.
17 Makerubi yaliposimama kimya, nayo pia yalitulia kimya, nao makerubi yalipoinuka juu, magurudumu nayo yaliinuka juu pamoja nao, kwa sababu roho ya vile viumbe hai ilikuwa ndani yake.
Gdy oni stali, stały, a gdy się ponosili, podnosiły się też z nimi; bo duch zwierząt był w nich.
18 Kisha utukufu wa Bwana ukaondoka pale kwenye kizingiti cha Hekalu na kusimama juu ya wale makerubi.
I odeszła chwała Pańska od progu domu, i stanęła nad Cherubinami.
19 Nilipokuwa nikitazama, makerubi yakatanda mabawa yao na kuinuka kutoka ardhini, nao walipokuwa wakienda, yale magurudumu yakaenda pamoja nao. Wakasimama kwenye ingilio la lango la mashariki la nyumba ya Bwana, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ukawa juu yao.
Gdy podnieśli Cherubinowie skrzydła swoje, a wzbili się od ziemi przed oczyma mojemi odchodząc, a koła przeciwko nim, i stanęli w wejściu bramy domu Pańskiego wschodniej, tedy chwała Boga Izraelskiego z wierzchu nad nimi była.
20 Hawa walikuwa ndio viumbe hai niliokuwa nimewaona chini ya Mungu wa Israeli kando ya Mto Kebari, nami nikatambua ya kuwa hao walikuwa makerubi.
Toć są one zwierzęta, którem widział pod Bogiem Izraelskim nad rzeką Chebar; i poznałem, iż to byli Cherubinowie.
21 Kila mmoja alikuwa na nyuso nne, mabawa manne, chini ya mabawa yao kulikuwa na kile kilichoonekana kama mikono ya mwanadamu.
Po cztery twarze miał każdy z nich, i po cztery skrzydła każdy z nich, a podobieństwo rąk ludzkich pod skrzydłami ich.
22 Nyuso zao zilifanana kama zile nilizokuwa nimeziona kando ya Mto Kebari. Kila mmoja alikwenda mbele moja kwa moja.
A podobieństwo twarzy ich było jako twarzy, którem widział u rzeki Chebar; także i oblicze ich takież było, i oni sami; każdy z nich prosto ku swej stronie chodził.

< Ezekieli 10 >