< Kutoka 38 >
1 Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu; nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano
The altar of burned offerings he made of hard wood; a square altar, five cubits long, five cubits wide and three cubits high,
2 Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba.
And he put horns at its four angles made of the same, plating it all with brass;
3 Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto.
And brass was used for all the vessels of the altar, the baskets and the spades, the basins and the meat-hooks and the fire-trays; all the vessels he made of brass
4 Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
And he made a network of brass for the altar, under the frame round it, stretching half-way up;
5 Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba.
And four rings for the four angles of this network, to take the rods.
6 Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba.
The rods he made of hard wood plated with brass.
7 Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.
He put the rods through the rings at the opposite sides of the altar for lifting it; he made the altar hollow, boarded in with wood.
8 Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.
And he made the washing-vessel of brass on a brass base, using the polished brass looking-glasses given by the women who did work at the doors of the Tent of meeting.
9 Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
To make the open space, he put hangings on the south side, of the best linen, a hundred cubits long:
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Their twenty pillars and their twenty bases were brass; and the hooks of the pillars and their bands were of silver.
11 Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
And for the north side. hangings a hundred cubits long, on twenty brass pillars in brass bases, with silver hooks and bands.
12 Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
And on the west side, hangings fifty cubits long, on ten pillars in ten bases, with silver bands.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini.
And on the east side, the open space was fifty cubits long.
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
The hangings on one side of the doorway were fifteen cubits long, on three pillars with their three bases;
15 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
And the same on the other side of the doorway; on this side and on that the hangings were fifteen cubits long, on three pillars with their three bases.
16 Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri.
All the hangings were of the best linen.
17 Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.
And the bases of the pillars were of brass; their hooks and the bands round the tops of them were of silver; all the pillars were ringed with silver.
18 Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano,
And the curtain for the doorway of the open space was of the best linen, with designs of blue and purple and red in needlework; it was twenty cubits long and five cubits high, to go with the hangings round the sides.
19 likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha.
There were four pillars with their bases, all of brass, the hooks being of silver, and their tops and their bands being covered with silver.
20 Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.
All the nails used for the House and the open space round it were of brass.
21 Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni.
This is the price of the making of the House, even the House of witness, as it was valued by the word of Moses, for the work of the Levites under the direction of Ithamar, the son of Aaron the priest.
22 (Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose,
Bezalel, the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah, made everything as the Lord had given orders to Moses.
23 akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.)
And with him was Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan; a designer and a trained workman, expert in needlework of blue and purple and red and the best linen.
24 Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
The gold used for all the different work done for the holy place, the gold which was given, was twenty-nine talents, and seven hundred and thirty shekels in weight, by the scale of the holy place.
25 Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
And the silver given by those who were numbered of the people was a hundred talents, and a thousand, seven hundred and seventy-five shekels in weight, by the scale of the holy place.
26 Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550.
A beka, that is, half a shekel by the holy scale, for everyone who was numbered; there were six hundred and three thousand, five hundred and fifty men of twenty years old and over.
27 Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako.
Of this silver, a hundred talents was used for making the bases of the pillars of the holy place and of the veil; a talent for every base.
28 Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.
And a thousand, seven hundred and seventy-five shekels of silver was used to make the hooks for the pillars, and for plating the tops of the pillars and for making their bands.
29 Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.
The brass which was given was seventy talents, two thousand four hundred shekels;
30 Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote,
From it he made the bases of the doorway of the Tent of meeting and the brass altar and the network for it and all the vessels for the altar,
31 vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.
And the bases for the open space all round and for its doorway, and all the nails for the House and for the open space.