< Kutoka 28 >
1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
« Fais venir auprès de toi Aaron, ton frère, et ses fils avec lui, du milieu des enfants d'Israël, afin qu'il soit à mon service dans le sacerdoce: Aaron, avec Nadab, Abihu, Éléazar et Ithamar, fils d'Aaron.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
Tu feras à Aaron, ton frère, des vêtements sacrés, pour sa gloire et sa beauté.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Tu parleras à tous ceux qui ont le cœur sage, que j'ai remplis de l'esprit de sagesse, pour qu'ils fassent les vêtements d'Aaron afin de le sanctifier, pour qu'il soit à mon service dans le sacerdoce.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Voici les vêtements qu'ils feront: un pectoral, un éphod, une robe, une tunique ajustée, un turban et une ceinture. Ils feront des vêtements sacrés pour Aaron, ton frère, et pour ses fils, afin qu'ils soient à mon service dans le sacerdoce.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
Ils utiliseront l'or, le bleu, le pourpre, l'écarlate et le lin fin.
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
« On fera l'éphod d'or, de bleu, de pourpre, d'écarlate et de fin lin retors, ouvrage d'un habile ouvrier.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
Il aura deux bretelles attachées à ses deux extrémités, afin qu'on puisse le joindre.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
La ceinture qui l'entourera sera semblable à son ouvrage et de la même pièce, en or, en bleu, en pourpre, en cramoisi et en fin lin retors.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
Tu prendras deux pierres d'onyx, et tu graveras sur elles les noms des enfants d'Israël.
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
Six de leurs noms sur l'une des pierres, et les noms des six autres sur l'autre pierre, dans l'ordre de leur naissance.
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
Avec le travail d'un graveur sur pierre, comme les gravures d'un sceau, tu graveras les deux pierres, selon les noms des enfants d'Israël. Tu les feras enfermer dans des montures d'or.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
Tu mettras les deux pierres sur les bretelles de l'éphod, comme pierres de souvenir pour les enfants d'Israël. Aaron portera leurs noms devant Yahvé sur ses deux épaules, en souvenir.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
Tu feras des montures d'or,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
et deux chaînettes d'or pur; tu les feras comme des cordons tressés. Tu mettras les chaînettes tressées sur les montures.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
« Tu feras un pectoral de jugement, ouvrage d'un habile ouvrier; tu le feras comme l'ouvrage de l'éphod; tu le feras d'or, de bleu, de pourpre, d'écarlate, et de fin lin retors.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
Il sera carré et plié en deux; sa longueur sera d'un empan, et sa largeur d'un empan.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
Tu y sertiras des pierres, quatre rangées de pierres: une rangée de rubis, de topaze et de béryl pour la première rangée;
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
une deuxième rangée de turquoise, de saphir et d'émeraude;
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
une troisième rangée de jacinthe, d'agate et d'améthyste;
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
une quatrième rangée de chrysolithe, d'onyx et de jaspe. Ils seront entourés d'or dans leurs montures.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Les pierres seront selon les noms des enfants d'Israël, douze, selon leurs noms; comme les gravures d'un cachet, chacun selon son nom, elles seront pour les douze tribus.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Tu feras sur le pectoral des chaînettes semblables à des cordons, tressées d'or pur.
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
Tu feras sur le pectoral deux anneaux d'or, et tu mettras les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
Tu mettras les deux chaînes d'or tressées dans les deux anneaux, aux extrémités du pectoral.
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Tu mettras les deux autres extrémités des deux chaînettes tressées sur les deux montures, et tu les mettras sur les bretelles de l'éphod dans sa partie antérieure.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
Tu feras deux anneaux d'or, et tu les mettras aux deux extrémités du pectoral, sur son bord, qui est du côté de l'éphod, vers l'intérieur.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Tu feras deux anneaux d'or, et tu les mettras sur les deux bretelles de l'éphod, en dessous, dans sa partie antérieure, près de son attache, au-dessus de la bande habilement tissée de l'éphod.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
On attachera le pectoral par ses anneaux aux anneaux de l'éphod, avec un lacet bleu, pour qu'il soit sur la ceinture de l'éphod et que le pectoral ne se détache pas de l'éphod.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
Aaron portera sur son cœur les noms des enfants d'Israël dans le pectoral du jugement, lorsqu'il entrera dans le sanctuaire, en souvenir permanent devant l'Éternel.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
Tu mettras dans le pectoral du jugement l'urim et le thummim, et ils seront sur le cœur d'Aaron, lorsqu'il entrera devant l'Éternel. Aaron portera sur son cœur le jugement des enfants d'Israël, devant Yahvé, en permanence.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
« Tu feras la robe de l'éphod toute bleue.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
Elle sera percée en son milieu d'un trou pour la tête. Il sera entouré d'une bordure tissée, comme le trou d'une cotte de mailles, afin qu'il ne se déchire pas.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
Sur son ourlet, tu feras des grenades bleues, pourpres et écarlates, tout autour de l'ourlet, avec des clochettes d'or entre elles et autour d'elles:
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
une clochette d'or et une grenade, une clochette d'or et une grenade, autour du bord de la robe.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
Elle sera sur Aaron pour le service; on en entendra le son quand il entrera dans le sanctuaire devant l'Éternel et quand il en sortira, afin qu'il ne meure pas.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
Tu feras une plaque d'or pur, et tu graveras dessus, comme on grave un cachet: « Sainteté à Yahvé ».
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
Tu la mettras sur un lacet bleu, et elle sera sur la ceinture. Elle sera sur le devant de la ceinture.
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
Elle sera sur le front d'Aaron; Aaron portera l'iniquité des choses saintes que les enfants d'Israël sanctifieront dans tous leurs dons sacrés; elle sera toujours sur son front, afin qu'ils soient agréés devant l'Éternel.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
Tu tisseras la tunique avec du lin fin. Tu feras un turban de fin lin. Tu feras une ceinture, ouvrage du brodeur.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
« Tu feras des tuniques pour les fils d'Aaron. Tu leur feras des ceintures. Tu leur feras des bandeaux, pour leur gloire et leur beauté.
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Tu les mettras sur Aaron, ton frère, et sur ses fils avec lui; tu les oindras, tu les consacreras et tu les sanctifieras, afin qu'ils puissent exercer mon ministère dans le cadre du sacerdoce.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
Tu leur feras un pantalon de lin pour couvrir leur chair nue. Il ira de la taille jusqu'aux cuisses.
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
Ils seront sur Aaron et sur ses fils, lorsqu'ils entreront dans la tente de la Rencontre ou lorsqu'ils s'approcheront de l'autel pour faire le service dans le lieu saint, afin qu'ils ne portent pas l'iniquité et ne meurent pas. Ce sera une loi pour lui et pour sa descendance après lui, pour toujours.