< Kutoka 17 >

1 Jumuiya yote ya Israeli ikaondoka kutoka Jangwa la Sini, ikisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kama Bwana alivyoagiza. Wakapiga kambi huko Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
And they set out all [the] congregation of [the] people of Israel from [the] wilderness of Sin to journeyings their on [the] mouth of Yahweh and they encamped at Rephidim and there not [was] water to drink the people.
2 Kwa hiyo wakagombana na Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Bwana?”
And it quarreled the people with Moses and they said give to us water so we may drink and he said to them Moses why? are you quarreling! with me why? are you putting to [the] test! Yahweh.
3 Lakini watu walikuwa na kiu huko, wakanungʼunika dhidi ya Mose, wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri, ukatuleta hapa utuue kwa kiu sisi, watoto wetu na mifugo yetu?”
And it was thirsty there the people for water and it grumbled the people on Moses and it said why? this did you bring up us from Egypt to put to death me and children my and livestock my by thirst.
4 Kisha Mose akamlilia Bwana, akasema, “Niwafanyie nini watu hawa? Sasa wanakaribia kunipiga kwa mawe.”
And he cried out Moses to Yahweh saying what? will I do to the people this yet a little and they will stone me.
5 Bwana akamjibu Mose, “Pita mbele ya watu. Wachukue pamoja nawe baadhi ya wazee wa Israeli, ichukue mkononi mwako ile fimbo uliyopiga nayo Mto Naili, nawe uende.
And he said Yahweh to Moses pass on before the people and take with you some of [the] elders of Israel and staff your which you struck with it the River take in hand your and you will go.
6 Huko nitasimama mbele yako karibu na mwamba wa Horebu. Uupige mwamba na maji yatatoka ndani yake kwa ajili ya watu kunywa.” Kwa hiyo Mose akafanya haya mbele ya wazee wa Israeli.
Here I [will be] standing before you there - on the rock at Horeb and you will strike the rock and they will come out from it waters and it will drink the people and he did so Moses to [the] eyes of [the] elders of Israel.
7 Naye akapaita mahali pale Masa, na Meriba kwa sababu Waisraeli waligombana na kumjaribu Bwana wakisema, “Je, Bwana yu pamoja nasi au la?”
And he called [the] name of the place Massah and Meribah on [the] quarrel of - [the] people of Israel and because put to [the] test they Yahweh saying ¿ [is] there Yahweh in midst our or? not.
8 Waamaleki wakaja na kuwashambulia Waisraeli huko Refidimu.
And it came Amalek and it joined battle with Israel at Rephidim.
9 Mose akamwambia Yoshua, “Chagua baadhi ya watu wetu na uende kupigana na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima nikiwa na fimbo ya Mungu mkononi mwangu.”
And he said Moses to Joshua choose for us men and go out fight against Amalek tomorrow I [will be] standing on [the] top of the hill and [the] staff of God [will be] in hand my.
10 Kwa hiyo Yoshua akapigana na Waamaleki kama Mose alivyomwagiza, nao Mose, Aroni na Huri wakapanda juu ya kilima.
And he did Joshua just as he had said to him Moses by fighting against Amalek and Moses Aaron and Hur they went up [the] top of the hill.
11 Ikawa wakati wote Mose alipokuwa amenyanyua mikono yake, Waisraeli walikuwa wakishinda, lakini kila aliposhusha mikono yake Waamaleki walishinda.
And it was just when he lifted up Moses hand his and it prevailed Israel and just when he gave rest hand his and it prevailed Amalek.
12 Mikono ya Mose ilipochoka, wakachukua jiwe na kumpa alikalie. Aroni na Huri wakaishikilia juu mikono ya Mose, mmoja upande huu na mwingine upande huu. Wakaitegemeza mikono yake ikabaki thabiti mpaka jua lilipozama.
And [the] hands of Moses [were] heavy and they took a stone and they put [it] under him and he sat on it and Aaron and Hur they supported hands his from this one and from this one and it was hands his [were] steadiness until went the sun.
13 Kwa hiyo Yoshua akalishinda jeshi la Waamaleki kwa upanga.
And he defeated Joshua Amalek and people its to [the] mouth of [the] sword.
14 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika mambo haya katika kitabu ili yakumbukwe, na uhakikishe kwamba Yoshua amesikia, kwa sababu nitafuta kabisa kumbukumbu la Amaleki chini ya mbingu.”
And he said Yahweh to Moses write this reminder in the book and put [it] in [the] ears of Joshua for certainly I will wipe out [the] remembrance of Amalek from under the heavens.
15 Mose akajenga madhabahu na kuiita Yehova Nisi.
And he built Moses an altar and he called name its Yahweh - [is] standard my.
16 Mose akasema, “Kwa maana mikono iliinuliwa mpaka kwenye kiti cha enzi cha Bwana. Bwana atakuwa na vita dhidi ya Waamaleki kutoka kizazi hata kizazi.”
And he said that a hand on [the] throne of Yahweh war [will belong] to Yahweh with Amalek from generation generation.

< Kutoka 17 >