< Esta 1 >
1 Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
Du temps d'Assuérus, qui régna depuis l'Inde jusqu'en Éthiopie, sur cent vingt-sept provinces,
2 Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
en ce temps-là, le roi Assuérus, assis sur le trône de son royaume, qui était à Suse, le palais,
3 Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
la troisième année de son règne, donna un festin à tous ses chefs et à ses serviteurs; l'armée de la Perse et de la Médie, les nobles et les chefs des provinces étaient devant lui.
4 Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
Il exposa les richesses de son glorieux royaume et l'honneur de son excellente majesté pendant de nombreux jours, et même pendant cent quatre-vingts jours.
5 Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
Lorsque ces jours furent accomplis, le roi fit un festin de sept jours pour tout le peuple qui se trouvait à Suse le palais, grands et petits, dans la cour du jardin du palais du roi.
6 Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
Il y avait des tentures d'étoffe blanche et bleue, attachées par des cordons de lin fin et de pourpre à des anneaux d'argent et à des colonnes de marbre. Les divans étaient d'or et d'argent, sur un pavement de marbre rouge, blanc, jaune et noir.
7 Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
On leur donnait à boire dans des vases d'or de différentes sortes, dont du vin royal en abondance, selon la générosité du roi.
8 Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
Conformément à la loi, la consommation n'était pas obligatoire, car le roi avait donné des instructions à tous les fonctionnaires de sa maison pour qu'ils agissent selon le bon plaisir de chacun.
9 Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
La reine Vasthi fit aussi un festin pour les femmes de la maison royale qui appartenait au roi Assuérus.
10 Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
Le septième jour, lorsque le cœur du roi fut réjoui par le vin, il ordonna à Mehuman, Biztha, Harbona, Bigtha, et Abagtha, Zethar et Carcass, les sept eunuques qui servaient en présence du roi Assuérus,
11 kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
d'amener la reine Vasthi devant le roi, portant la couronne royale, pour montrer au peuple et aux princes sa beauté, car elle était belle.
12 Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
Mais la reine Vasthi refusa de venir sur l'ordre du roi par les eunuques. C'est pourquoi le roi fut très irrité, et sa colère brûla en lui.
13 Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
Alors le roi dit aux sages, qui connaissaient les temps (car c'était la coutume du roi de consulter ceux qui connaissaient la loi et le jugement;
14 nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
et, à côté de lui, Carshena, Shethar, Admatha, Tarsis, Mérès, Marsena et Memucan, les sept princes de Perse et de Médie, qui voyaient le visage du roi et étaient assis les premiers dans le royaume),
15 Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
« Que ferons-nous à la reine Vasthi selon la loi, parce qu'elle n'a pas exécuté les ordres du roi Assuérus par les eunuques? »
16 Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
Memucan prit la parole devant le roi et les princes: « La reine Vasthi n'a pas fait du tort seulement au roi, mais aussi à tous les princes et à tout le peuple qui se trouve dans toutes les provinces du roi Assuérus.
17 Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
En effet, cette action de la reine sera connue de toutes les femmes, ce qui les amènera à mépriser leurs maris, lorsqu'on racontera: « Le roi Assuérus avait ordonné que la reine Vasthi soit amenée devant lui, mais elle n'est pas venue ".
18 Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
Aujourd'hui, les princesses de Perse et de Médie qui ont entendu parler de l'acte de la reine le diront à tous les princes du roi. Cela provoquera beaucoup de mépris et de colère.
19 “Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
« S'il plaît au roi, qu'un ordre royal parte de lui et qu'il soit écrit parmi les lois des Perses et des Mèdes, afin qu'il ne puisse être modifié, afin que Vasthi ne se présente plus jamais devant le roi Assuérus; et que le roi donne son domaine royal à un autre qui soit meilleur qu'elle.
20 Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
Lorsque l'édit du roi qu'il fera sera publié dans tout son royaume (car il est grand), toutes les femmes rendront honneur à leurs maris, grands et petits. »
21 Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
Cet avis plut au roi et aux princes, et le roi fit selon la parole de Memucan:
22 Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.
car il envoya des lettres dans toutes les provinces du roi, dans chaque province selon son écriture, et à chaque peuple dans sa langue, afin que chacun dirige sa propre maison, en parlant la langue de son peuple.