< Esta 4 >

1 Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu.
And Mordecai he knew all that it had been done and he tore Mordecai clothes his and he put on sackcloth and ash[es] and he went out in [the] midst of the city and he cried a cry loud and bitter.
2 Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia.
And he went to before [the] gate of the king for not to go into [the] gate of the king in clothing of sackcloth.
3 Katika kila jimbo ambapo amri na agizo la mfalme lilifika, kulikuwa na maombolezo makuu miongoni mwa Wayahudi pamoja na kufunga, kulia na kuomboleza. Watu wengi wakalala juu ya nguo za magunia na majivu.
And in every province and province [the] place where [the] word of the king and law his [were] reaching mourning great [belonged] to the Jews and fasting and weeping and wailing sackcloth and ash[es] it was spread as a bed by many [people].
4 Wajakazi wa Esta na matowashi walipokuja na kumwambia kuhusu Mordekai, alipatwa na huzuni kuu. Alimtumia nguo avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai hakuzikubali.
(And they came *Q(k)*) [the] maids of Esther and eunuchs her and they told to her and she agonized the queen exceedingly and she sent garments to clothe Mordecai and to remove sackcloth his from on him and not he accepted [them].
5 Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmojawapo wa matowashi wa mfalme ambaye alikuwa amewekwa kumhudumia Esta, akamwagiza kutafuta ni nini kilikuwa kikimtaabisha Mordekai na ni kwa nini.
And she summoned Esther Hathach one of [the] eunuchs of the king whom he had made stand before her and she commanded him on Mordecai to know what? [was] this and concerning what? [was] this.
6 Basi Hathaki alitoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanja ulio wazi wa mji mbele ya lango la mfalme.
And he went out Hathach to Mordecai to [the] open place of the city which [was] before [the] gate of the king.
7 Mordekai akamwambia kila kitu ambacho kimempata, pamoja na hesabu kamili ya fedha ambazo Hamani aliahidi kulipa katika hazina ya mfalme kwa ajili ya maangamizi ya Wayahudi.
And he told to him Mordecai all that it had happened to him and - [the] exact amount of the silver which he had said Haman to weigh out to [the] treasuries of the king (for the Jews *Q(k)*) to destroy them.
8 Akampa nakala ya andiko la amri kwa ajili ya maangamizi yao, lililokuwa limechapishwa huko Shushani, kumwonyesha Esta na kumwelezea. Mordekai akamwambia towashi amshawishi Esta kwenda mbele ya mfalme kuomba rehema na kumsihi kwa ajili ya watu wake.
And copy of [the] writing of the law which it had been given in Susa to annihilate them he gave to him to show Esther and to tell to her and to command to her to go to the king to seek favor to him and to request from to before him on people her.
9 Hathaki akarudi kwa Esta na kumwarifu alilolisema Mordekai.
And he came Hathach and he told to Esther [the] words of Mordecai.
10 Kisha Esta akamwamuru Hathaki amweleze Mordekai,
And she said Esther to Hathach and she commanded him to Mordecai.
11 “Maafisa wote wa mfalme na watu wa majimbo ya ufalme wanajua kuwa mwanaume au mwanamke yeyote ambaye ataingia kumwona mfalme katika ua wa ndani bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu: Atauawa. Njia pekee kinyume na hili ni mfalme kumnyooshea fimbo ya dhahabu ili aishi. Lakini siku thelathini zimepita tangu nilipoitwa kwenda kwa mfalme.”
All [the] servants of the king and [the] people of [the] provinces of the king [are] knowing that every man and woman who he goes to the king into the court inner who not he is summoned [is] one law his to put to death apart from that he extends to him the king [the] scepter of gold and he will live and I not (I have been summoned *L(abh)*) to go to the king this thirty day[s].
12 Wakati Mordekai aliarifiwa maneno ya Esta,
And they told to Mordecai [the] words of Esther.
13 Mordekai alirudisha jibu hili: “Usifikiri kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mfalme wewe pekee katika Wayahudi wote utapona.
And he said Mordecai to bring back to Esther may not you imagine in self your to escape [the] house of the king from all the Jews.
14 Kwa kuwa kama utakaa kimya wakati huu, msaada na ukombozi kwa Wayahudi utatoka mahali pengine, lakini wewe na jamaa ya baba yako mtaangamia. Nani ajuaye kwamba hukuja kwenye nafasi ya mamlaka kwa ajili ya wakati kama huu?”
That except certainly you will keep quiet at the time this relief and deliverance it will arise for the Jews from a place another and you and [the] house of father your you will perish and who? [is] knowing if for a time like this you have reached the queenhood.
15 Kisha Esta alituma jibu hili kwa Mordekai:
And she said Esther to bring back to Mordecai.
16 “Nenda, kusanya pamoja Wayahudi wote walioko Shushani, nanyi mfunge kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu, usiku na mchana. Mimi na wajakazi wangu tutafunga kama mnavyofanya. Baada ya kufanyika hili, nitakwenda kwa mfalme, hata ingawa ni kinyume cha sheria. Ikiwa ni kuangamia na niangamie.”
Go gather all the Jews who are found in Susa and fast on me and may not you eat and may not you drink three days night and day also I and maids my I will fast thus and in such I will go to the king which not [is] according to the law and just as I have perished I have perished.
17 Kwa hiyo Mordekai alikwenda zake na kutekeleza maagizo yote ya Esta.
And he passed on Mordecai and he did according to all that she had commanded to him Esther.

< Esta 4 >