< Waefeso 5 >
1 Kwa hiyo, mfuateni Mungu kama watoto wapendwao,
Be ye therefore followers of God, as dear children;
2 mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.
And walk in love, as Christ also hath loved us, and hath given himself for us an offering and a sacrifice to God for a sweet-smelling savor.
3 Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.
But lewdness and all uncleanness or covetousness, let it not be once named among you, as becometh saints;
4 Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.
Neither filthiness, nor foolish talking, nor jesting, which are not convenient: but rather giving of thanks.
5 Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.
For this ye know, that no lewd, nor unclean person, nor covetous man, who is an idolater, hath any inheritance in the kingdom of Christ and of God.
6 Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.
Let no man deceive you with vain words: for because of these things cometh the wrath of God upon the children of disobedience.
7 Kwa hiyo, msishirikiane nao.
Be ye not therefore partakers with them.
8 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
For ye were sometime darkness, but now [are ye] light in the Lord: walk as children of light;
9 (kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
(For the fruit of the Spirit [is] in all goodness, and righteousness, and truth; )
10 nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
Proving what is acceptable to the Lord.
11 Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
And have no fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather reprove [them].
12 Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
For it is a shame even to speak of those things which are done by them in secret.
13 Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
But all things that are reproved, are made manifest by the light: for whatever doth make manifest is light.
14 kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
Wherefore he saith, Awake, thou that sleepest, and arise from the dead, and Christ will give thee light.
15 Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,
See then that ye walk circumspectly, not as fools, but as wise,
16 mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.
Redeeming the time, because the days are evil.
17 Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.
Wherefore be ye not unwise, but understanding what the will of the Lord [is].
18 Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.
And be not drunk with wine, in which is excess; but be filled with the Spirit;
19 Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,
Speaking to yourselves in psalms, and hymns, and spiritual songs, singing and making melody in your heart to the Lord,
20 siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Giving thanks always for all things to God and the Father, in the name of our Lord Jesus Christ;
21 Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.
Submitting yourselves one to another in the fear of God.
22 Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.
Wives, submit yourselves to your own husbands, as to the Lord.
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.
For the husband is the head of the wife, even as Christ is the head of the church: and he is the Savior of the body.
24 Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.
Therefore as the church is subject to Christ, so [let] wives [be] to their own husbands in every thing.
25 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake
Husbands, love your wives, even as Christ also loved the church, and gave himself for it;
26 kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,
That he might sanctify and cleanse it with the washing of water by the word,
27 apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia.
That he might present it to himself a glorious church, not having spot or wrinkle, or any such thing; but that it should be holy and without blemish.
28 Vivyo hivyo imewapasa waume kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
So ought men to love their wives, as their own bodies. He that loveth his wife, loveth himself.
29 Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake mwenyewe, bali huulisha na kuutunza vizuri, kama Kristo anavyolitunza Kanisa lake.
For no man ever yet hated his own flesh; but nourisheth and cherisheth it, even as the Lord the church:
30 Sisi tu viungo vya mwili wake.
For we are members of his body, of his flesh, and of his bones.
31 “Kwa sababu hii, mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
For this cause shall a man leave his father and mother, and shall be joined to his wife, and they two shall be one flesh.
32 Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.
This is a great mystery: but I speak concerning Christ and the church.
33 Hata hivyo, kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake mwenyewe, naye mke lazima amheshimu mumewe.
Nevertheless, let every one of you in particular so love his wife even as himself: and the wife [see] that she reverence [her] husband.