< Mhubiri 9 >

1 Kwa hiyo niliyatafakari yote haya nikafikia uamuzi kwamba waadilifu na wenye hekima na yale wanayoyafanya yako mikononi mwa Mungu, lakini hakuna mtu ajuaye kama anangojewa na upendo au chuki.
Car tout cela, je l'ai mis dans mon cœur, jusqu'à l'explorer: que le juste et le sage, et leurs œuvres, sont dans la main de Dieu; que ce soit l'amour ou la haine, l'homme ne le sait pas; tout est devant eux.
2 Wote wanayo hatima inayofanana, mwadilifu na mwovu, mwema na mbaya, aliye safi na aliye najisi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa. Kama ilivyo kwa mtu mwema, ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye dhambi; kama ilivyo kwa wale wanaoapa, ndivyo ilivyo kwa wale wasioapa.
Tout se passe de la même manière pour tous. Il y a un même événement pour le juste et pour le méchant, pour le bon, pour le pur, pour l'impur, pour celui qui sacrifie et pour celui qui ne sacrifie pas. Tel est le bon, tel est le pécheur; celui qui fait un serment, comme celui qui craint un serment.
3 Huu ni ubaya ulio katika kila kitu kinachotendeka chini ya jua: Mwisho unaofanana huwapata wote. Zaidi ya hayo, mioyo ya watu, imejaa ubaya na kuna wazimu mioyoni mwao wangali hai, hatimaye huungana na waliokufa.
C'est un mal dans tout ce qui se fait sous le soleil, qu'il y ait un seul événement pour tous. Oui aussi, le cœur des fils de l'homme est rempli de mal, et la folie est dans leur cœur tant qu'ils vivent, et après cela ils vont chez les morts.
4 Yeyote aliye miongoni mwa walio hai analo tumaini, hata mbwa hai ni bora kuliko simba aliyekufa!
Pour celui qui est uni à tous les vivants, il y a de l'espoir; car un chien vivant vaut mieux qu'un lion mort.
5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui chochote, hawana tuzo zaidi, hata kumbukumbu yao imesahaulika.
Car les vivants savent qu'ils vont mourir, mais les morts ne savent rien, et ils n'ont plus de récompense, car leur mémoire est oubliée.
6 Upendo wao, chuki yao na wivu wao vimetoweka tangu kitambo, kamwe hawatakuwa tena na sehemu katika lolote linalotendeka chini ya jua.
De même, leur amour, leur haine et leur envie ont disparu depuis longtemps; et ils n'ont plus de part pour toujours à tout ce qui se fait sous le soleil.
7 Nenda, kula chakula chako kwa furaha, unywe divai yako kwa moyo wa shangwe, kwa maana sasa Mungu anakubali unachofanya.
Va, mange ton pain avec joie, et bois ton vin avec un cœur joyeux, car Dieu a déjà accepté tes œuvres.
8 Daima uvae nguo nyeupe na daima upake kichwa chako mafuta.
Que tes vêtements soient toujours blancs, et que ta tête ne manque pas d'huile.
9 Furahia maisha na mke wako, umpendaye, siku zote za maisha ya ubatili uliyopewa na Mungu chini ya jua, siku zote za ubatili. Kwa maana hili ndilo fungu lako katika maisha na katika kazi yako ya taabu chini ya jua.
Vis dans la joie avec la femme que tu aimes, tous les jours de ta vie de vanité, qu'il t'a donnée sous le soleil, tous tes jours de vanité, car c'est là ta part dans la vie, et dans le travail que tu fais sous le soleil.
10 Lolote mkono wako upatalo kufanya, fanya kwa nguvu zako zote, kwa kuwa huko kuzimu, unakokwenda, hakuna kufanya kazi wala mipango wala maarifa wala hekima. (Sheol h7585)
Tout ce que ta main trouve à faire, fais-le avec ta force; car il n'y a ni œuvre, ni plan, ni connaissance, ni sagesse, dans le séjour des morts où tu vas. (Sheol h7585)
11 Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.
Je suis revenu et j'ai vu sous le soleil que la course n'est pas pour les rapides, ni la bataille pour les forts, ni le pain pour les sages, ni la richesse pour les intelligents, ni la faveur pour les habiles; mais le temps et le hasard leur arrivent à tous.
12 Zaidi ya hayo, hakuna mwanadamu ajuaye wakati saa yake itakapokuja: Kama vile samaki wavuliwavyo katika wavu mkatili, au ndege wanaswavyo kwenye mtego, vivyo hivyo wanadamu hunaswa na nyakati mbaya zinazowaangukia bila kutazamia.
Car l'homme aussi ne connaît pas son temps. Comme les poissons qui sont pris dans un mauvais filet, et comme les oiseaux qui sont pris au piège, ainsi les fils de l'homme sont pris au piège dans un mauvais moment, quand il leur tombe dessus tout à coup.
13 Pia niliona chini ya jua mfano huu wa hekima ambao ulinivutia sana:
J'ai aussi vu la sagesse sous le soleil de cette manière, et elle m'a paru grande.
14 Palikuwa na mji mdogo uliokuwa na watu wachache ndani yake. Mfalme mwenye nguvu akainuka dhidi yake, akauzunguka akaweka jeshi kubwa dhidi yake.
Il y avait une petite ville, et peu d'hommes à l'intérieur; un grand roi vint contre elle, l'assiégea, et construisit contre elle de grands remparts.
15 Katika mji huo kulikuwepo mtu mmoja maskini lakini mwenye hekima, naye akauokoa ule mji kwa hekima yake. Lakini hakuna aliyemkumbuka yule maskini.
Il s'y trouva un pauvre sage qui, par sa sagesse, délivra la ville; mais personne ne se souvenait de ce pauvre homme.
16 Kwa hiyo, nikasema, “Hekima ni bora kuliko nguvu.” Lakini hekima ya maskini imedharauliwa, wala hakuna anayesikiliza maneno yake.
Alors j'ai dit: « La sagesse vaut mieux que la force. » Cependant la sagesse du pauvre homme est méprisée, et ses paroles ne sont pas écoutées.
17 Maneno ya utulivu ya mwenye hekima husikiwa kuliko makelele ya mtawala wa wapumbavu.
Les paroles des sages, entendues dans le calme, valent mieux que le cri de celui qui domine parmi les insensés.
18 Hekima ni bora kuliko silaha za vita, lakini mwenye dhambi mmoja huharibu mema mengi.
La sagesse vaut mieux que les armes de guerre, mais un seul pécheur détruit beaucoup de bien.

< Mhubiri 9 >