< Torati 25 >

1 Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia.
If it will happen a dispute between people and they will draw near to the place of judgment and they will judge them and they will declare righteous the righteous [one] and they will condemn as guilty the guilty [one].
2 Kama mtu mwenye hatia anastahili kuchapwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili achapwe mbele yake idadi ya viboko kulingana na kosa lake,
And it will be if [is] a son of striking the guilty [one] and he will make lie down him the judge and someone will strike him before him according to [the] sufficiency of wickedness his by number.
3 lakini kamwe asichapwe zaidi ya viboko arobaini. Ikiwa atachapwa zaidi ya viboko arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.
Forty [times] he will strike him not he will increase lest he should increase to strike him to these striking much and he will be dishonored countryman your to eyes your.
4 Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.
Not you will muzzle an ox when threshes it.
5 Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake.
If they will dwell brothers together and he will die one from them and a son not [belongs] to him not she will belong [the] wife of the dead [man] the outside towards to a man strange husband's brother her he will go on her and he will take her for himself to a wife and he will act as a husband's brother for her.
6 Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.
And it will be the firstborn whom she will bear he will stand on [the] name of brother his dead and not it will be wiped out name his from Israel.
7 Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.”
And if not he will desire the man to take brother's wife his and she will go up brother's wife his the gate towards to the elders and she will say he has refused husband's brother my to establish for brother his a name in Israel not he was willing to act as a husband's brother for me.
8 Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,”
And they will summon him [the] elders of city his and they will speak to him and he will stand firm and he will say not I desire to take her.
9 mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.”
And she will draw near brother's wife his to him to [the] eyes of the elders and she will draw off sandal his from on foot his and she will spit in face his and she will answer and she will say thus let it be done to the man who not he will build [the] house of (brother his *L(abh)*)
10 Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.
and it will be called name its in Israel [the] house of [the] [one] drawn off of the sandal.
11 Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri,
If they will be struggling together men together anyone and countryman his and she will draw near [the] wife of the one [man] to rescue (husband her *LAB(h)*) from [the] hand of [the] [one who] is striking him and she will stretch out hand her and she will take hold on genitals his.
12 huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.
And you will cut off hand her not it will look with pity eye your.
13 Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi.
Not it will belong to you in bag your a weight and a weight large and small.
14 Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo.
Not it will belong to you in house your a measure and a measure large and small.
15 Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
A weight full and righteousness it will belong to you a measure full and righteousness it will belong to you so that they may be long days your on the land which Yahweh God your [is] about to give to you.
16 Kwa maana Bwana Mungu wako humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.
For [is] [the] abomination of Yahweh God your every [one who] does these [things] every [one who] does injustice.
17 Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri.
Remember [that] which it did to you Amalek on the way when came out you from Egypt.
18 Wakati mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.
That it met you on the way and it attacked in [the] rear you all the stragglers behind you and you [were] exhausted and weary and not it feared God.
19 Bwana Mungu wako atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi akupayo kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!
And it will be when gives rest Yahweh God your - to you from all enemies your from round about in the land which Yahweh God your [is] about to give to you an inheritance to take possession of it you will wipe out [the] remembrance of Amalek from under the heavens not you will forget.

< Torati 25 >