< Danieli 6 >

1 Ilimpendeza Dario kuteua wakuu 120 kutawala katika ufalme wake wote,
Il plut à Darius d'établir sur le royaume cent vingt gouverneurs locaux, qui devaient être répartis dans tout le royaume;
2 pamoja na wasimamizi watatu juu yao, ambao mmoja wao alikuwa Danieli. Wakuu walitoa hesabu kwa hao wasimamizi ili mfalme asipate hasara.
et sur eux trois présidents, dont Daniel faisait partie, afin que ces gouverneurs locaux leur rendent compte et que le roi ne subisse aucune perte.
3 Basi Danieli alijidhihirisha, miongoni mwa wasimamizi na wakuu kwa sifa zake za kipekee hata mfalme akapanga kumweka juu ya ufalme wote.
Ce Daniel se distingua des présidents et des gouverneurs locaux, parce qu'il avait un esprit excellent, et le roi pensa à l'établir sur tout le royaume.
4 Walipofahamu hilo, wakuu na wasimamizi wakajaribu kutafuta sababu za kumshtaki Danieli kuhusu usimamizi wake wa shughuli za serikali, lakini hawakuweza kufanikiwa. Hawakuweza kupata kosa kwake, kwa sababu alikuwa mwaminifu, wala hakupatikana na upotovu au uzembe.
Alors les présidents et les gouverneurs locaux cherchèrent à trouver une occasion contre Daniel en ce qui concerne le royaume; mais ils ne purent trouver ni occasion ni faute, parce qu'il était fidèle. Ils ne trouvèrent ni erreur ni faute en lui.
5 Mwishoni watu hawa walisema, “Kamwe hatutapata msingi wa mashtaka dhidi ya huyu Danieli isipokuwa iwe inahusiana na sheria ya Mungu wake.”
Alors ces hommes dirent: « Nous ne trouverons aucune occasion contre ce Daniel, à moins que nous ne la trouvions contre lui au sujet de la loi de son Dieu. »
6 Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!
Alors ces présidents et ces gouverneurs locaux s'assemblèrent auprès du roi, et lui dirent ceci: « Roi Darius, vis éternellement!
7 Wasimamizi wa ufalme, wasaidizi, wakuu, washauri na watawala wote wamekubaliana kwamba mfalme atoe sheria na kukazia amri kuwa yeyote atakayetoa dua kwa mungu au mwanadamu yeyote katika muda huu wa siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, ee mfalme, atupwe ndani ya tundu la simba.
Tous les présidents du royaume, les députés et les gouverneurs locaux, les conseillers et les gouverneurs, se sont consultés pour établir une loi royale et un décret fort, selon lequel quiconque demandera une requête à un dieu ou à un homme pendant trente jours, sauf à toi, ô roi, sera jeté dans la fosse aux lions.
8 Sasa, ee mfalme, toa amri na uiandike ili isiweze kubadilishwa: kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Maintenant, ô roi, établis le décret et signe l'écrit, afin qu'il ne soit pas modifié, selon la loi des Mèdes et des Perses, qui ne change pas. »
9 Hivyo Mfalme Dario akaiweka amri hiyo katika maandishi.
Le roi Darius signa donc l'écrit et le décret.
10 Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni.
Lorsque Daniel sut que l'écriture était signée, il entra dans sa maison (les fenêtres de sa chambre étaient maintenant ouvertes vers Jérusalem) et il se mit à genoux trois fois par jour, et pria, et rendit grâce devant son Dieu, comme il le faisait auparavant.
11 Ndipo watu hawa wakaenda kama kikundi na kumkuta Danieli akiomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msaada.
Alors ces hommes s'assemblèrent et trouvèrent Daniel en train de prier et de supplier son Dieu.
12 Basi wakaenda kwa mfalme na kusema naye kuhusu amri ya mfalme: “Je, hukutangaza amri kwamba kwa muda huu wa siku thelathini zijazo mtu yeyote ambaye atamwomba mungu au mwanadamu yeyote isipokuwa wewe, ee mfalme, angetupwa ndani ya tundu la simba?” Mfalme akajibu, “Amri ndivyo ilivyo, kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Alors ils s'approchèrent et parlèrent devant le roi au sujet du décret du roi: « N'as-tu pas signé un décret selon lequel tout homme qui, dans les trente jours, adressera une requête à un dieu ou à un homme, sauf à toi, ô roi, sera jeté dans la fosse aux lions? ». Le roi répondit: « Cette chose est vraie, selon la loi des Mèdes et des Perses, qui ne change pas. »
13 Ndipo wakamwambia mfalme, “Danieli, ambaye ni mmoja wa mahamisho kutoka Yuda, hakuheshimu, ee mfalme, wala hajali amri uliyoiweka kwa maandishi. Bado anaomba mara tatu kwa siku.”
Alors ils prirent la parole et dirent devant le roi: « Ce Daniel, qui est d'entre les enfants de la captivité de Juda, ne te respecte pas, ô roi, ni le décret que tu as signé, mais il fait sa demande trois fois par jour. »
14 Wakati mfalme aliposikia hili, akahuzunika mno. Akakusudia kumwokoa Danieli, hivyo akafanya kila jitihada ya kumwokoa hadi jua likatua.
Alors le roi, en entendant ces paroles, fut très mécontent, et il jeta son dévolu sur Daniel pour le délivrer; et il travailla jusqu'au coucher du soleil pour le secourir.
15 Ndipo wale watu wakamwendea mfalme kama kikundi na kumwambia, “Ee mfalme, kumbuka kwamba kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, hakuna amri wala sheria ambayo mfalme ameitoa inayoweza kubadilishwa.”
Alors ces hommes s'assemblèrent auprès du roi et lui dirent: « Sache, ô roi, que c'est une loi des Mèdes et des Perses, qu'aucun décret ni aucune loi que le roi établit ne peut être modifié. »
16 Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, na wakamtupa ndani ya tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako unayemtumikia daima na akuokoe!”
Alors le roi ordonna qu'on amène Daniel et qu'on le jette dans la fosse aux lions. Le roi prit la parole et dit à Daniel: « Ton Dieu que tu sers sans cesse, il te délivrera. »
17 Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.
On apporta une pierre qu'on posa sur l'ouverture de la fosse, et le roi la scella de son propre sceau et du sceau de ses grands, afin que rien ne fût changé au sujet de Daniel.
18 Kisha mfalme akarudi kwenye jumba lake la kifalme, naye usiku kucha hakula chakula wala kutumia viburudisho alivyoletewa. Lakini hakuweza kulala.
Le roi se rendit ensuite dans son palais, et passa la nuit à jeûner. On ne lui apporta aucun instrument de musique, et le sommeil le quitta.
19 Asubuhi na mapema, mfalme akaondoka na kuharakisha kwenda kwenye tundu la simba.
Le roi se leva de grand matin, et se rendit en hâte à la fosse aux lions.
20 Wakati alipokaribia lile tundu, akamwita Danieli kwa sauti ya uchungu, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima, ameweza kukuokoa kwa simba?”
Lorsqu'il s'approcha de la fosse, Daniel cria d'une voix troublée. Le roi prit la parole et dit à Daniel: « Daniel, serviteur du Dieu vivant, ton Dieu, que tu sers continuellement, est-il capable de te délivrer des lions? »
21 Danieli akajibu, “Ee mfalme, uishi milele!
Alors Daniel dit au roi: « O roi, vis éternellement!
22 Mungu wangu alimtuma malaika wake, naye akafunga vinywa vya hawa simba. Hawajanidhuru, kwa sababu nilionekana sina hatia mbele zake. Wala kamwe sijafanya jambo lolote baya mbele yako, ee mfalme.”
Mon Dieu a envoyé son ange et a fermé la gueule des lions, et ils ne m'ont pas fait de mal, parce que l'innocence a été trouvée en moi devant lui; et aussi devant toi, ô roi, je n'ai fait aucun mal. »
23 Mfalme akafurahi mno, naye akatoa amri Danieli atolewe kutoka kwa lile tundu. Danieli alipotolewa kutoka kwa lile tundu, hakukutwa na jeraha lolote, kwa sababu alikuwa amemtumaini Mungu wake.
Le roi se réjouit et ordonna qu'on fasse sortir Daniel de la fosse. On fit donc sortir Daniel de la fosse, et on ne lui trouva aucun mal, car il avait mis sa confiance en son Dieu.
24 Kwa amri ya mfalme, wale watu waliokuwa wamemshtaki Danieli kwa uongo waliletwa na kutupwa ndani ya lile tundu la simba, pamoja na wake zao na watoto wao. Nao kabla hawajafika chini kwenye sakafu ya lile tundu, simba wakawakamata na kusaga mifupa yao yote.
Le roi donna cet ordre. On amena les hommes qui avaient accusé Daniel et on les jeta dans la fosse aux lions, eux, leurs enfants et leurs femmes; les lions les déchiquetèrent et brisèrent tous leurs os avant qu'ils n'arrivent au fond de la fosse.
25 Kisha Mfalme Dario akawaandikia kabila zote za watu, mataifa, na watu wa kila lugha katika nchi yote: “Ninyi na mstawi sana!
Alors le roi Darius écrivit à tous les peuples, nations et langues qui habitent sur toute la terre: « Que la paix vous soit multipliée.
26 “Natoa amri hii, kwamba katika kila sehemu ya ufalme wangu, lazima watu wamwogope na kumheshimu Mungu wa Danieli. “Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai, naye hudumu milele, ufalme wake hautaangamizwa, nao utawala wake hauna mwisho.
« Je décrète que dans toute la domination de mon royaume, les hommes tremblent et craignent devant le Dieu de Daniel. « Car il est le Dieu vivant, et inébranlable pour toujours. Son royaume est celui qui ne sera pas détruit. Sa domination s'étendra jusqu'à la fin.
27 Huponya na kuokoa; hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani. Amemwokoa Danieli kutoka nguvu za simba.”
Il délivre et sauve. Il accomplit des signes et des prodiges dans le ciel et sur la terre, qui a délivré Daniel de la puissance des lions. »
28 Hivyo Danieli akastawi wakati wa utawala wa Dario, na utawala wa Koreshi Mwajemi.
Ce Daniel prospéra donc sous le règne de Darius et sous le règne de Cyrus le Perse.

< Danieli 6 >