< Danieli 12 >

1 “Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
And at the time that he will arise Michael the prince great who stands over [the] sons of people your and it will be a time of distress which not it has happened from when was a nation until the time that and at the time that it will escape people your every [one who] is found written in the scroll.
2 Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
And many [people] of [the] sleepers of [the] ground of dust they will awake these to life of perpetuity and these to reproaches to abhorrence of perpetuity.
3 Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
And those [who] have insight they will shine like [the] shining of the firmament and [those who] turn to righteousness the many [people] like the stars for ever and ever.
4 Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
And you O Daniel keep secret the words and seal up the scroll until [the] time of [the] end they will rove about many [people] so it may increase knowledge.
5 Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
And I saw I Daniel and there! two others [were] standing one here to [the] bank of the River and one here to [the] bank of the River.
6 Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
And someone said to the man clothed of linen who [was] from above [the] water of the River until when? [will be] [the] end of the wonders.
7 Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
And I heard the man - clothed of linen who [was] from above [the] water of the River and he raised right [hand] his and left [hand] his to the heavens and he swore by [the] living one of perpetuity that to a time times and a half and just as finish to smash [the] hand of [the] people of holiness they will be finished all these [things].
8 Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
And I I heard and not I understood and I said! O lord my what? [will be] [the] latter part of these [things].
9 Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
And he said go O Daniel for [are] kept secret and sealed up the things until [the] time of [the] end.
10 Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
They will purge themselves and they may purify themselves so they may be refined many [people] and they will act wickedly wicked [people] and not they will understand any wicked [people] and those [who] have insight they will understand.
11 “Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
And from [the] time [when] it was abolished the perpetual [offering] and to [the] setting up of [the] abomination desolating [will be] days one thousand two hundred and ninety.
12 Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
How blessed! [is] the [one who] waits and he may arrive to days one thousand three hundreds thirty and five.
13 “Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”
And you go to the end so you may rest and you may arise to allotted portion your to [the] end of the days.

< Danieli 12 >