< Amosi 4 >

1 Sikilizeni neno hili, ninyi ngʼombe wa Bashani mlioko juu ya Mlima Samaria, ninyi wanawake mnaowaonea maskini, na kuwagandamiza wahitaji, na kuwaambia wanaume wenu, “Tuleteeni vinywaji!”
Hear the word this O cows of Bashan who [are] on [the] mountain of Samaria who oppress poor [people] who crush needy [people] who say to masters their bring! so we may drink.
2 Bwana Mwenyezi ameapa kwa utakatifu wake: “Hakika wakati utakuja mtakapochukuliwa na kulabu, na wanaosalia kwa ndoana za samaki.
He has sworn [the] Lord Yahweh by holiness his for here! days [are] coming on you and someone will take away you with barbs and posterity your with hooks of fishing.
3 Nanyi mtakwenda moja kwa moja kupitia mahali palipobomolewa kwenye ukuta, nanyi mtatupwa nje kuelekea Harmoni,” asema Bwana.
And breaches you will go out each before herself and you will throw Harmon towards [the] utterance of Yahweh.
4 “Nendeni Betheli mkatende dhambi; nendeni Gilgali mkazidi kutenda dhambi. Leteni dhabihu zenu kila asubuhi, zaka zenu kila mwaka wa tatu.
Come Beth-el and transgress Gilgal increase to transgress and bring to the morning sacrifices your to three days tithes your.
5 Mchome mkate uliotiwa chachu kama sadaka ya shukrani, jisifuni kuhusu sadaka zenu za hiari: jigambeni kwa ajili ya sadaka hizo, enyi Waisraeli, kwa kuwa hili ndilo mnalopenda kulitenda,” asema Bwana Mwenyezi.
And make smoke from a thing leavened a thank-offering and proclaim freewill offerings make [them] heard for thus you love O people of Israel [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
6 “Niliwapa njaa kwenye kila mji, na ukosefu wa chakula katika kila mji, hata hivyo bado hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
And also I I gave to you cleanness of teeth in all cities your and lack of bread in all places your and not you returned to me [the] utterance of Yahweh.
7 “Pia niliwazuilia ninyi mvua miezi mitatu kabla ya kufikia mavuno. Nilinyesha mvua kwenye mji mmoja, lakini niliizuia mvua isinyeshe mji mwingine. Shamba moja lilipata mvua, na lingine halikupata, nalo likakauka.
And also I I withheld from you the rain in yet three months [were] to the harvest and I sent rain on a city one and on a city one not I sent rain a portion of ground one it was rained on and a portion of ground which not it sent rain on it it dried up.
8 Watu walitangatanga mji hata mji kutafuta maji, lakini hawakupata ya kuwatosha kunywa, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
And they staggered two three cities to a city one to drink water and not they were satisfied and not you returned to me [the] utterance of Yahweh.
9 “Mara nyingi nilizipiga bustani zenu na mashamba ya mizabibu, niliyapiga kwa kutu na ukungu. Nzige walitafuna tini zenu na miti ya mizeituni, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
I struck you with blight and with mildew to make many gardens your and vineyards your and fig trees your and olive trees your it ate the locust and not you returned to me [the] utterance of Yahweh.
10 “Niliwapelekea tauni miongoni mwenu kama nilivyofanya kule Misri. Niliwaua vijana wenu wa kiume kwa upanga, niliwachukua farasi wenu. Nilijaza pua zenu kwa uvundo kutoka kwenye kambi zenu, hata hivyo hamjanirudia mimi,” asema Bwana.
I sent among you pestilence in [the] manner of Egypt I killed by the sword young men your with [the] capture of horses your and I caused to go up [the] stench of camp your in nose your and not you returned to me [the] utterance of Yahweh.
11 “Niliwaangamiza baadhi yenu kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Mlikuwa kama kijiti kiwakacho kilichonyakuliwa motoni, hata hivyo hamjanirudia,” asema Bwana.
I overthrew among you like [the] overthrow of God Sodom and Gomorrah and you were like a piece of firewood plucked out (from [the] burning *L(abh)*) and not you returned to me [the] utterance of Yahweh.
12 “Kwa hiyo hili ndilo nitakalowafanyia, Israeli, na kwa sababu nitawafanyia hili, jiandaeni kukutana na Mungu wenu, ee Israeli.”
Therefore thus I will do to you O Israel consequence for this I will do to you be prepared to meet God your O Israel.
13 Yeye ambaye hufanya milima, anaumba upepo, na kufunua mawazo yake kwa mwanadamu, yeye ageuzaye asubuhi kuwa giza, na kukanyaga mahali pa juu pa nchi: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
For here! [one who] formed mountains and [one who] created wind and [one who] tells to humankind what? [is] thought his [one who] makes dawn darkness and [one who] treads on [the] high places of [the] earth [is] Yahweh God of hosts name his.

< Amosi 4 >