< Matendo 20 >

1 Baada ya zile ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi pamoja akawatia moyo, akawaaga, akaanza safari kwenda Makedonia.
骚乱平息以后,保罗把信徒们召集在一起,鼓励他们一番后便辞行前往马其顿。
2 Alipita katika sehemu zile, akinena na watu maneno mengi ya kuwatia moyo. Ndipo hatimaye akawasili Uyunani,
他走遍该地区的各个角落,激励鼓舞那里的信徒,然后来到了希腊。
3 ambako alikaa kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa anakaribia kuanza safari kwa njia ya bahari kwenda Shamu, kwa sababu Wayahudi walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yake, aliamua kurudi kupitia njia ya Makedonia.
他在那里住了三个月后,准备乘船去叙利亚。就在这时,他发现有些犹太人想要密谋对付他,于是他决定通过马其顿返回。
4 Paulo alikuwa amefuatana na Sopatro mwana wa Piro, Mberoya, Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonike na Gayo, mtu wa Derbe, Timotheo pamoja na Tikiko na Trofimo kutoka sehemu ya Asia.
与他同行的人有:比里亚人所巴特(毕罗斯之子)、帖撒罗尼迦人亚里达古和西公都,特庇人该犹和提摩太,亚西亚人推基古和特罗非摩。
5 Hawa watu walitutangulia wakaenda kutungojea Troa.
这些人先行,在特罗亚等候我们。
6 Lakini sisi tukasafiri kwa njia ya bahari kwa siku tano kutoka Filipi baada ya siku za Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, nasi tukaungana na wengine huko Troa, ambako tulikaa kwa siku saba.
我们则在除酵节后乘船从腓立比出发,五天后在特罗亚与他们会合,在那里停留了一个星期。
7 Siku ya kwanza ya juma tulikutana pamoja kwa ajili ya kumega mkate. Paulo akaongea na watu, naye kwa kuwa alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliendelea kuongea mpaka usiku wa manane.
星期日那天,我们聚在一起用餐。保罗计划第二天清晨离开,在当天一直讲道到午夜时分。
8 Kwenye chumba cha ghorofani walimokuwa wamekutania kulikuwa na taa nyingi.
(我们聚餐地点的楼上,点亮了许多灯火。)
9 Kijana mmoja jina lake Eutiko, alikuwa amekaa dirishani, wakati Paulo alipokuwa akihubiri kwa muda mrefu, alipatwa na usingizi mzito, akaanguka kutoka ghorofa ya tatu, wakamwinua akiwa amekufa.
有一个名叫犹推古的少年坐在窗台上,因为保罗讲道的时间很长,他越发困倦,于是便睡了过去,从三楼坠下去,待众人把他扶起来时,发现他已经死去。
10 Paulo akashuka chini, akajitupa juu yake na kumkumbatia, akasema, “Msishtuke, uzima wake bado umo ndani yake.”
保罗走下楼,趴在他身上把其抱住,说:“别担心,他还活着。”
11 Kisha Paulo akapanda tena ghorofani, akamega mkate na kula. Baada ya kuongea mpaka mapambazuko, akaondoka.
随即他回到楼上,掰开饼与众人继续讲道,直到天明才离开。
12 Watu wakamrudisha yule kijana nyumbani akiwa hai nao wakafarijika sana.
他们把已经活过来的少年带回家,对此事深表感激。
13 Tukatangulia melini tukasafiri mpaka Aso ambako tungempakia Paulo. Alikuwa amepanga hivyo kwa maana alitaka kufika kwa miguu.
我们上船后向亚朔出发,按计划我们需要在那里与保罗会和,因为他走的是陆路。
14 Alipotukuta huko Aso, tulimpakia melini, tukasafiri wote mpaka Mitilene.
我们在亚朔与他会合后,接他上船一同去往米推利尼。
15 Kutoka huko tuliendelea kwa njia ya bahari, na kesho yake tukafika mahali panapokabili Kio. Siku iliyofuata tukavuka kwenda Samo, na kesho yake tukawasili Mileto.
随后又乘船去了基阿,第二天在撒摩短暂停留,接下来到了米利都。
16 Paulo alikuwa ameamua tusipitie Efeso ili asitumie muda mwingi huko sehemu za Asia, kwa sababu alikuwa anatamani kama ikiwezekana kufika Yerusalemu kabla ya siku ya Pentekoste.
保罗希望能在五旬节赶到耶路撒冷,所以决定不在以弗所停留,以免在亚西亚耽搁时间。
17 Paulo akiwa Mileto, alituma mjumbe kwenda Efeso kuwaita wazee wa kanisa waje wakutane naye.
在米利都,他派人给以弗所教会的长老捎去口信。
18 Walipofika akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua jinsi nilivyoishi katikati yenu muda wote tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia.
他们抵达目的地后,保罗说:“你们知道从我们一起抵达亚西亚的第一天起,我的表现一直都很好。
19 Nilimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi nikivumilia taabu na mapingamizi yaliyonipata kutokana na hila za Wayahudi.
我以谦卑之心服侍主,经常泪流满面,还要忍受犹太人密谋带来的麻烦和压力。
20 Mnajua kwamba sikusita kuhubiri jambo lolote ambalo lingekuwa la kuwafaa ninyi, lakini nilifundisha hadharani na nyumba kwa nyumba.
但我一直向你们讲述会对你们有益的事,毫无保留。在走街串巷的过程中,我公开向你们讲道。
21 Nimewashuhudia Wayahudi na Wayunani kwamba inawapasa kumgeukia Mungu kwa kutubu dhambi na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.
我向犹太人和希腊人都作过见证,想要他们悔改并归于上帝,相信我们的主耶稣,这一点很重要。
22 “Nami sasa nimesukumwa na Roho, ninakwenda Yerusalemu wala sijui ni nini kitakachonipata huko.
现在,灵坚持让我去耶路撒冷,我不知道自己在那里会遭遇什么事,
23 Ila ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu amenionya kuwa vifungo na mateso vinaningoja.
只知道在我所造访的所有城中,圣灵都在警告我,将有监牢和苦难在等着我。
24 Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani kwangu, kama kuyamaliza mashindano na kukamilisha ile kazi Bwana Yesu aliyonipa, yaani, kazi ya kuishuhudia Injili ya neema ya Mungu.
但我并不吝惜自己的性命,只想完成自己的使命,达成主耶稣分派给我的职责,为上帝恩典的福音作见证。
25 “Nami sasa najua ya kuwa hakuna hata mmoja miongoni mwenu ambaye nimemhubiria Ufalme wa Mungu katika kwenda kwangu huku na huko, atakayeniona uso tena.
我与你们讲述了上帝之国。现在我确信,你们无法再见到我了。
26 Kwa hiyo nawatangazia leo, sina hatia ya damu ya mtu awaye yote.
所以我今天要向你们宣布,如果有人迷失,那不是我的责任。
27 Kwa kuwa sikusita kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
上帝想要你们知道的,我已经毫无保留地告诉了你们。
28 Jilindeni nafsi zenu na mlilinde lile kundi lote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi wake. Lichungeni kanisa lake Mungu alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
请照顾好自己,也照顾好圣灵派你们看管的羊群。主用自己的鲜血建立的教会,你们要为之做出贡献。
29 Najua kwamba baada yangu kuondoka, mbwa mwitu wakali watakuja katikati yenu ambao hawatalihurumia kundi.
我知道在我离开之后,必有凶狠豺狼闯到你们中间,不肯放过你们所看守的羊群。
30 Hata kutoka miongoni mwenu watainuka watu na kuupotosha ukweli ili wawavute wanafunzi wawafuate.
你们中也会有人开始颠倒黑白,引诱信徒跟从他们。
31 Hivyo jilindeni! Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuacha kamwe kuwaonya kila mmoja kwa machozi usiku na mchana.
所以要小心,别忘记三年来,我日夜不停地教导你们,经常为你们泪流满面。
32 “Sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, linaloweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi miongoni mwa wote ambao wametakaswa.
现在我就要把你们交给上帝的关爱,交给他恩典之道,这道可以让你们成长,并为你提供属于所有遵守正道的人的遗产。
33 Sikutamani fedha wala dhahabu wala vazi la mtu yeyote.
我从未贪念任何人的金银或衣服。
34 Ninyi wenyewe mnajua kwamba mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami.
你们知道我凭借自己的双手行事,满足我自己和同伴们的需要。
35 Katika kila jambo nimewaonyesha kwamba kwa njia hii ya kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wadhaifu, mkikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe jinsi alivyosema, ‘Ni heri kutoa kuliko kupokea.’”
我凡事都以身作则,努力帮助那些软弱之人,牢记主耶稣的教会:‘给予远比获得更有福。’”
36 Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba.
说罢这番话,他跪下来同大家一起祷告。
37 Wote wakalia, wakamkumbatia Paulo na kumbusu,
众人痛哭着抱住保罗,亲吻他。
38 Kilichowahuzunisha zaidi ni kwa sababu ya yale maneno aliyosema kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Wakaenda naye mpaka kwenye meli.
保罗说他们不会再见他,这句话让他们伤心不已。随后,他们和他一起走到船上。

< Matendo 20 >