< Matendo 13 >
1 Katika kanisa huko Antiokia ya Shamu walikuwako manabii na walimu, yaani: Barnaba, Simeoni aitwaye Nigeri, Lukio Mkirene, Manaeni aliyekuwa amelelewa pamoja na Mfalme Herode Agripa, na Sauli.
There were now (some *k*) in Antioch in what is [the] church prophets and teachers, both Barnabas and Simeon who is being called Niger and Lucius the Cyrenian, Manaen also — with Herod the tetrarch brought up — and Saul.
2 Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Sauli na Barnaba kwa kazi ile maalum niliyowaitia.”
As were ministering now they to the Lord and fasting said the Spirit Holy; do set apart then to Me (both *k*) Barnabas and (*k*) Saul for the work to which I have called them.
3 Ndipo baada ya kufunga na kuomba, wakawawekea mikono yao na wakawatuma waende zao.
Then having fasted and having prayed and having laid the hands on them they sent [them] off.
4 Hivyo, wakiwa wametumwa na Roho Mtakatifu, wakashuka kwenda Seleukia na kutoka huko wakasafiri baharini mpaka kisiwa cha Kipro.
(They themselves *N(k)O*) indeed therefore having been sent forth by of the Holy (the *k*) Spirit went down to (*k*) Seleucia, From there (then *NK(o)*) they sailed to (*k*) Cyprus.
5 Walipowasili katika mji wa Salami, wakahubiri neno la Mungu katika sinagogi la Wayahudi. Pia walikuwa na Yohana Marko kuwa msaidizi wao.
And having come into Salamis they were proclaiming the word of God in the synagogues of the Jews; They had now also John [as] a helper.
6 Walipokwisha kupita katika nchi zote hizo wakafika Pafo, ambapo walikutana na Myahudi mmoja mchawi aliyekuwa nabii wa uongo, jina lake Bar-Yesu.
Having passed through now (all *NO*) the island as far as Paphos they found (a man — *NO*) a certain magician a false prophet Jewish — whose name (of Bar-Jesus, *N(k)O*)
7 Mtu huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mtu mwenye hekima aliyekuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala wa kile kisiwa. Sergio Paulo akawaita Sauli na Barnaba akitaka kusikia neno la Mungu.
who was with the proconsul Sergius Paulus, man an intelligent. He having called to [him] Barnabas and Saul desired to hear the word of God.
8 Lakini Elima yule mchawi (hii ndiyo maana ya jina lake), aliwapinga Barnaba na Sauli na kujaribu kumpotosha yule mkuu wa kile kisiwa aiache imani.
Was opposing however to them Elymas the magician — thus for means the name of him — seeking to turn away the proconsul from the faith.
9 Ndipo Sauli, ambaye pia aliitwa Paulo, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akamkazia macho Elima huyo mchawi,
Saul then also [called] Paul having been filled [the] Spirit Holy (and *k*) having looked intently upon him
10 akamwambia, “Ewe mwana wa ibilisi, wewe ni adui wa kila kilicho haki! Umejaa kila aina ya udanganyifu na ulaghai. Je, hutaacha kuzipotosha njia za Bwana zilizonyooka?
said; O full of all deceit and all craft, son of [the] devil, enemy of all righteousness, not will you cease perverting the ways (of the *no*) Lord upright?
11 Nawe sasa sikiliza, mkono wa Bwana u dhidi yako. Utakuwa kipofu, wala hutaona jua kwa muda.” Mara ukungu na giza vikamfunika, naye akaenda huku na huko akitafuta mtu wa kumshika mkono ili amwonyeshe njia.
And now behold [the] hand (*k*) of the Lord [is] upon you, and you will be blind not seeing the sun during a season. Immediately (then descended *N(k)O*) upon him mist and darkness, and going about he was seeking one to lead by hand.
12 Yule mkuu wa kile kisiwa alipoona yaliyotukia, akaamini kwa sababu alistaajabishwa na mafundisho kuhusu Bwana.
Then having seen the proconsul that having happened he believed being astonished at the teaching of the Lord.
13 Kisha Paulo na wenzake wakasafiri toka Pafo wakafika Perga huko Pamfilia. Lakini, Yohana Marko akawaacha huko, akarejea Yerusalemu.
Having sailed then from Paphos [with] those around [him] (*k*) Paul came to Perga of Pamphylia. John however having departed from them he returned to Jerusalem.
14 Kutoka Perga wakaendelea hadi Antiokia ya Pisidia. Siku ya Sabato wakaingia ndani ya sinagogi, wakaketi.
They themselves now having passed through from Perga came to Antioch (Pisidia, *N(k)O*) and (having gone *NK(o)*) into the synagogue on the day of the Sabbaths they sat down.
15 Baada ya Sheria ya Mose na Kitabu cha Manabii kusomwa, viongozi wa sinagogi wakawatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mna neno la kuwafariji watu hawa, tafadhali lisemeni.”
After then the reading of the law and of the Prophets sent the rulers of the synagogue to them saying; Men brothers, if any there is among you a word of exhortation toward the people, do speak.
16 Paulo akasimama, akawapungia mkono na kusema: “Enyi wanaume wa Israeli na ninyi nyote mnaomcha Mungu.
Having risen up then Paul and having made a sign with the hand he said; Men Israelites and you who [are] fearing God, do listen.
17 Mungu wa watu hawa wa Israeli aliwachagua baba zetu, akawafanya kustawi walipokuwa huko Misri, kwa uwezo mwingi akawaongoza na kuwatoa katika nchi ile.
The God of the people this of Israel chose the fathers of us and the people exalted in the sojourn in [the] land (of Egypt *N(k)O*) and with arm uplifted brought them out of it;
18 Kwa muda wa miaka arobaini alivumilia matendo yao walipokuwa jangwani.
and of about forty years for a period He endured the ways of them in the wilderness,
19 Naye baada ya kuyaangamiza mataifa saba waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, akawapa Waisraeli nchi yao iwe urithi wao.
and having destroyed nations seven in [the] land of Canaan He gave as an inheritance (to them *k*) the land of them —
20 Haya yote yalichukua kama muda wa miaka 450. “Baada ya haya, Mungu akawapa waamuzi mpaka wakati wa nabii Samweli.
during years four hundred and fifty; And after these things He gave [them] judges until Samuel the prophet;
21 Ndipo watu wakaomba wapewe mfalme, naye Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi wa kabila la Benyamini, aliyetawala kwa miaka arobaini.
Then Then they asked for a king, and gave to them God Saul son of Kish, a man of [the] tribe of Benjamin, years forty;
22 Baada ya kumwondoa Sauli katika ufalme, akawainulia Daudi kuwa mfalme wao. Mungu pia alimshuhudia, akisema, ‘Nimemwona Daudi mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayetimiza mapenzi yangu yote.’
And having removed him He raised up David to them as king, to whom also He said having carried witness: I have found David the [son of] Jesse a man according to the heart of Mine, who will do all the will of Mine.
23 “Kutoka uzao wa mtu huyu, Mungu amewaletea Israeli Mwokozi Yesu, kama alivyoahidi.
Of this [man] the God of the seed according to promise (has brought *N(K)O*) to Israel ([the] Savior *NK(O)*) Jesus —
24 Kabla ya kuja kwa Yesu, Yohana alihubiri toba na ubatizo kwa watu wote wa Israeli.
When was proclaiming John before [the] face of the coming of Him a baptism of repentance to all the people of Israel.
25 Yohana alipokuwa anakamilisha kazi yake, alisema: ‘Ninyi mnadhani mimi ni nani? Mimi si yeye. La hasha, lakini yeye yuaja baada yangu, ambaye mimi sistahili kufungua kamba za viatu vya miguu yake.’
While then was fulfilling (*k*) John the course he was saying; (whom *N(k)O*) me myself do you suppose to be? Not am [he] I myself; but behold He comes after me myself of whom not I am worthy the sandal of the feet to untie.
26 “Ndugu zangu, wana wa Abrahamu, nanyi watu wa Mataifa mnaomcha Mungu, ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
Men brothers, sons of [the] family of Abraham and you who [are] among you fearing God, (to us *N(K)O*) the message of the salvation this (was sent out. *N(k)O*)
27 Kwa sababu wakaao Yerusalemu na viongozi wao hawakumtambua wala kuelewa maneno ya manabii yasomwayo kila Sabato, bali waliyatimiza maneno hayo kwa kumhukumu yeye.
Those for dwelling in Jerusalem and the rulers of them Him not having known and the voices of the prophets that on every Sabbath are being read, having condemned [Him] they fulfilled [them];
28 Ijapokuwa hawakupata sababu yoyote ya kumhukumu kifo, walimwomba Pilato aamuru auawe.
And no cause of death having found they begged Pilate to execute him.
29 Walipokwisha kufanya yale yote yaliyoandikwa kumhusu, walimshusha kutoka msalabani na kumzika kaburini.
When then they had finished (all *N(k)O*) the [things] about Him written, having taken [Him] down from the tree they put [Him] in a tomb.
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu.
But God raised Him out from [the] dead,
31 Naye kwa siku nyingi akawatokea wale waliokuwa pamoja naye kuanzia Galilaya hadi Yerusalemu. Nao sasa wamekuwa mashahidi wake kwa watu wetu.
who appeared for days many to those having come up with Him from Galilee to Jerusalem, who (now *NO*) are witnesses of Him to the people.
32 “Nasi tunawaletea habari njema, kwamba yale Mungu aliyowaahidi baba zetu
And we ourselves to you evangelise the to the fathers promise having been made,
33 sasa ameyatimiza kwetu sisi watoto wao, kwa kumfufua Yesu, kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili: “‘Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.’
that this God has fulfilled to the children of them (to us *NK(O)*) having raised up Jesus, as also in the psalm it has been written in the (second *NK(O)*) Son of Mine are You yourself, I myself today have begotten you.’
34 Kwa kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu asioze kamwe, alitamka maneno haya: “‘Nitakupa wewe baraka takatifu zilizo za hakika nilizomwahidi Daudi.’
for then He raised Him out from [the] dead no more being about to return to decay, thus He has spoken that I will give to you the holy [blessings] of David the sure [blessings].’
35 Kama ilivyosemwa mahali pengine katika Zaburi, “‘Hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu.’
(therefore *N(k)O*) also in another He says: Not You will allow the Holy One of you to see decay.’
36 “Kwa maana Daudi akiisha kulitumikia kusudi la Mungu katika kizazi chake, alilala; akazikwa pamoja na baba zake na mwili wake ukaoza.
David indeed for in his own generation having served the of God purpose he fell asleep and he was added to the fathers of him and saw decay;
37 Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu hakuona uharibifu.
The [One] however God raised up not did see decay.
38 “Kwa hiyo ndugu zangu, nataka ninyi mjue kwamba kwa kupitia huyu Yesu msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu.
Known therefore it should be to you, men brothers, that through this One to you forgiveness of sins is proclaimed;
39 Kwa kupitia yeye, kila mtu amwaminiye anahesabiwa haki kwa kila kitu ambacho asingeweza kuhesabiwa haki kwa sheria ya Mose.
And from all things from which not you were able in (the *k*) law of Moses to be justified, in Him everyone who is believing is justified.
40 Kwa hiyo jihadharini ili yale waliyosema manabii yasiwapate:
do take heed therefore lest may come about (upon you *K*) that said in the prophets:
41 “‘Angalieni, enyi wenye dhihaka, mkastaajabu, mkaangamie, kwa maana nitatenda jambo wakati wenu ambalo hamtasadiki, hata kama mtu akiwaambia.’”
Behold! you scoffers, and do wonder and do perish for a work am working I myself in the days of you, a work (that *N(k)O*) certainly not you may believe even if one shall declare it to you.’
42 Paulo na Barnaba walipokuwa wakitoka nje ya sinagogi, watu wakawaomba wazungumze tena mambo hayo Sabato iliyofuata.
When are departing then (they *no*) (from the *k*) (synagogue *K*) (of the *k*) (Jews *K*) were begging (the gentiles *K*) on the next Sabbath to be spoken to them declarations these.
43 Baada ya kusanyiko la Sinagogi kutawanyika, wengi wa Wayahudi na waongofu wa dini ya Kiyahudi wakawafuata Paulo na Barnaba, wakazungumza nao na kuwahimiza wadumu katika neema ya Mungu.
When was releasing then the synagogue followed many of the Jews and of the worshipping converts after Paul and after Barnabas, who speaking to them were persuading them (to continue *N(k)O*) in the grace of God.
44 Sabato iliyofuata, karibu watu wote wa mji walikuja kusikiliza neno la Bwana.
On the (now *NK(o)*) coming Sabbath almost all the city was gathered together to hear the word (of the Lord. *N(K)O*)
45 Lakini Wayahudi walipoona ule umati mkubwa wa watu walijawa na wivu, wakayakanusha maneno Paulo aliyokuwa akisema.
Having seen however the Jews the crowds they were filled with jealousy and were contradicting the [things] by (*k*) Paul (spoken *N(k)O*) (denying and *K*) denigrating [him].
46 Ndipo Paulo na Barnaba wakawajibu kwa ujasiri, wakisema, “Ilitupasa kunena nanyi neno la Mungu kwanza. Lakini kwa kuwa mmelikataa, mkajihukumu wenyewe kuwa hamstahili uzima wa milele, sasa tunawageukia watu wa Mataifa. (aiōnios )
Having spoken boldly (also *N(k)O*) Paul and Barnabas said; To you it was necessary first to be spoken the word of God; but since (now *ko*) you thrust away it and not worthy you judge yourselves of eternal life, behold we are turning to the Gentiles. (aiōnios )
47 Kwa maana hili ndilo Bwana alilotuamuru: “‘Nimewafanya ninyi kuwa nuru kwa watu wa Mataifa, ili mpate kuuleta wokovu hadi miisho ya dunia.’”
Thus for has commanded us the Lord: I have set you for a light of [the] Gentiles to be you for salvation until [the] uttermost part of the earth.’
48 Watu wa Mataifa waliposikia haya wakafurahi na kulitukuza neno la Bwana; nao wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. (aiōnios )
Hearing [it] then the Gentiles (were rejoicing *NK(o)*) and they were glorifying the word of the (Lord *NK(O)*) and they believed as many as were appointed to life eternal. (aiōnios )
49 Neno la Bwana likaenea katika eneo lile lote.
Was carried then the word of the Lord through all the region.
50 Lakini Wayahudi wakawachochea wanawake wenye kumcha Mungu, wenye vyeo pamoja na watu maarufu katika mji, wakachochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na kuwafukuza kutoka eneo hilo.
The but Jews incited the worshipping women (and *k*) [those] prominent and the principals of the city and they stirred up a persecution against Paul and (*k*) Barnabas and expelled them from the district of them.
51 Hivyo Paulo na Barnaba wakakungʼuta mavumbi ya miguu yao ili kuwapinga, nao wakaenda Ikonio.
But having shaken off the dust of the feet (of them *k*) against them they went to Iconium.
52 Wanafunzi wakajawa na furaha na Roho Mtakatifu.
(and *N(k)O*) the disciples were filled with joy and [the] Spirit Holy.