< 2 Timotheo 3 >
1 Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari.
But of this be assured: in the last days grievous times will set in.
2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu,
For men will be lovers of self, lovers of money, boastful, haughty, profane. They will be disobedient to parents, thankless, irreligious,
3 wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,
destitute of natural affection, unforgiving, slanderers. They will have no self-control, but will be brutal, opposed to goodness,
4 wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:
treacherous, headstrong, self-important. They will love pleasure instead of loving God,
5 wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.
and will keep up a make-believe of piety and yet live in defiance of its power. Turn away from people of this sort.
6 Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.
Among them are included the men who make their way into private houses and carry off weak women as their prisoners--women who, weighed down by the burden of their sins, are led by ever-changing caprice,
7 Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.
and are always learning something new, and yet are never able to arrive at real knowledge of the truth.
8 Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
And just as Jannes and Jambres withstood Moses, so also these false teachers withstand the truth--being, as they are, men of debased intellects, and of no real worth so far as faith is concerned.
9 Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.
But they will have no further success; for their folly will be as clearly manifest to all men, as that of the opponents of Moses came to be.
10 Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,
But you have intimately known my teaching, life, aims, faith, patience, love, resignation,
11 mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.
and the persecutions and sufferings which I have endured; the things which happened to me in Antioch, Iconium and Lystra. You know the persecutions I endured, and how the Lord delivered me out of them all.
12 Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.
And indeed every one who is determined to live a godly life as a follower of Christ Jesus will be persecuted.
13 Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
But bad men and impostors will go on from bad to worse, misleading and being misled.
14 Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,
But you must cling to the things which you have learnt and have been taught to believe, knowing who your teachers were,
15 na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
and that from infancy you have known the sacred writings which are able to make you wise to obtain salvation through faith in Christ Jesus.
16 Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,
Every Scripture is inspired by God and is useful for teaching, for convincing, for correction of error, and for instruction in right doing;
17 ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.
so that the man of God may himself be complete and may be perfectly equipped for every good work.