< 2 Samweli 1 >

1 Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi.
And it was after [the] death of Saul and David he returned from defeating Amalek and he remained David in Ziklag days two.
2 Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.
And it was - on the day third and there! a man [was] coming from the camp from with Saul and garments his [were] torn and earth [was] on head his and it was when came he to David and he fell [the] ground towards and he bowed down.
3 Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”
And he said to him David where? from this are you coming and he said to him from [the] camp of Israel I have escaped.
4 Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.” Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”
And he said to him David what? was it the word tell please to me and he said that it has fled the people from the battle and also [surely] a multitude has fallen of the people and they have died and also Saul and Jonathan son his they have died.
5 Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”
And he said David to the young man who had told to him how? do you know that he has died Saul and Jonathan son his.
6 Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana.
And he said the young man - who had told to him [surely] by chance I found myself on [the] mountain of Gilboa and there! Saul [was] leaning on spear his and there! the chariotry and [the] owners of the horses they overtook him.
7 Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’
And he turned behind him and he saw me and he called to me and I said here [am] I.
8 “Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’ “Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’
And he said to me who? [are] you (and I said *Q(K)*) to him [am] an Amalekite I.
9 “Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’
And he said to me stand please over me and kill me for it has seized me dizziness for all still life my [is] in me.
10 “Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”
And I stood over him and I killed him for I knew that not he will live after had fallen he and I took the crown - which [was] on head his and an armlet which [was] on arm his and I brought them to lord my here.
11 Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua.
And he took hold David (on garments his *Q(K)*) and he tore them and also all the men who [were] with him.
12 Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.
And they mourned and they wept and they fasted until the evening on Saul and on Jonathan son his and on [the] people of Yahweh and on [the] house of Israel for they had fallen by the sword.
13 Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?” Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”
And he said David to the young man who had told to him where? from this [are] you and he said [am the] son of a man a sojourner an Amalekite I.
14 Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”
And he said to him David how? not were you afraid to stretch out hand your to destroy [the] [one] anointed of Yahweh.
15 Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa.
And he called David to one from the young men and he said draw near fall on him and he struck down him and he died.
16 Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’”
And he said to him David (blood your *Q(K)*) [be] on head your for own mouth your it has testified against you saying I I killed [the] [one] anointed of Yahweh.
17 Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe,
And he lamented David the lamentation this on Saul and on Jonathan son his.
18 naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):
And he said to teach [the] descendants of Judah Bow here! [it is] written on [the] scroll of the Jashar.
19 “Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka. Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!
The beauty O Israel on high places your [is] slain how! they have fallen [the] mighty [ones].
20 “Msilisimulie hili katika Gathi, msilitangaze hili katika barabara za Ashkeloni, binti za Wafilisti wasije wakafurahia, binti za hao wasiotahiriwa wasije wakashangilia.
May not you tell in Gath may not you bear news in [the] streets of Ashkelon lest they should rejoice [the] daughters of [the] Philistines lest they should exult [the] daughters of the uncircumcised.
21 “Enyi milima ya Gilboa, msipate umande wala mvua, wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka. Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa, ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.
O mountains in Gilboa may not dew and may not rain [be] on you and fields of contributions for there it was defiled [the] shield of [the] mighty [ones] [the] shield of Saul not [was] anointed with oil.
22 Kutokana na damu ya waliouawa, kutokana na miili ya wenye nguvu, ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma. Upanga wa Sauli haukurudi bure.
From [the] blood of [those] slain from [the] fat of [the] mighty [ones] [the] bow of Jonathan not it turned back backwards and [the] sword of Saul not it returned empty.
23 “Sauli na Yonathani, maishani walipendwa na kuneemeka, na katika kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
Saul and Jonathan lovable and pleasant in lives their and in death their not they were separated more than eagles they were swift more than lions they were strong.
24 “Enyi binti za Israeli, lieni kwa ajili ya Sauli, ambaye aliwavika nguo nyekundu na maridadi, ambaye aliremba mavazi yenu kwa mapambo ya dhahabu.
O daughters of Israel because of Saul weep who clothed you scarlet with luxuries who brought up ornament[s] of gold on clothing your.
25 “Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa mahali pako palipoinuka.
How! they have fallen [the] mighty [ones] in [the] middle of the battle Jonathan on high places your [is] slain.
26 Nahuzunika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu, kwangu ulikuwa mpendwa sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.
It is distress to me on you O brother my Jonathan you were pleasant to me very it was wonderful love your to me more than [the] love of women.
27 “Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka! Silaha za vita zimeangamia!”
How! they have fallen [the] mighty [ones] and they have perished [the] weapons of war.

< 2 Samweli 1 >