< 2 Samweli 21 >

1 Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
And it was a famine in [the] days of David three years year after year and he sought David [the] face of Yahweh. And he said Yahweh because of Saul and because of [the] house of blood on that he put to death the Gibeonites.
2 Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
And he summoned the king the Gibeonites and he said to them and the Gibeonites not [were] from [the] people of Israel they that except from [the] remnant of the Amorite[s] and [the] people of Israel they had sworn an oath to them and he had sought Saul to strike down them because was zealous he for [the] people of Israel and Judah.
3 Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
And he said David to the Gibeonites what? will I do for you and how? will I make amends and bless [the] inheritance of Yahweh.
4 Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
And they said to him the Gibeonites not (to us *Q(K)*) silver and gold with Saul and with house his and not to us a man to put to death in Israel and he said what? [are] you saying I will do for you.
5 Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
And they said to the king the man who he made an end of us and who he planned to us we were destroyed from standing in all [the] territory of Israel.
6 tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
(Let it be given *Q(K)*) to us seven men from descendants his and we will impale them to Yahweh at Gibeah of Saul [the] chosen one of Yahweh. And he said the king I I will give [them].
7 Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
And he had compassion the king on Mephi-bosheth [the] son of Jonathan [the] son of Saul on [the] oath of Yahweh which [was] between them between David and between Jonathan [the] son of Saul.
8 Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
And he took the king [the] two [the] sons of Rizpah [the] daughter of Aiah whom she had borne to Saul Armoni and Mephibosheth and [the] five [the] sons of Michal [the] daughter of Saul whom she had borne to Adriel [the] son of Barzillai the Meholathite.
9 Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
And he gave them in [the] hand of the Gibeonites and they impaled them on the mountain before Yahweh and they fell ([the] seven of them *Q(K)*) together (and they *Q(k)*) they were put to death in [the] days of harvest in the first (at [the] beginning of *Q(K)*) [the] harvest of barley.
10 Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
And she took Rizpah [the] daughter of Aiah sackcloth and she spread out it for herself to the rock from [the] beginning of harvest until it was poured out water on them from the heavens and not she permitted [the] bird[s] of the heavens to rest on them by day and [the] animal[s] of the field night.
11 Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
And it was told to David [that] which she had done Rizpah [the] daughter of Aiah [the] concubine of Saul.
12 alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
And he went David and he took [the] bones of Saul and [the] bones of Jonathan son his from with [the] citizens of Jabesh Gilead who they had stolen them from [the] open square of Beth Shan where (they had hung up them there [the] Philistines *Q(K)*) on [the] day struck down [the] Philistines Saul on Gilboa.
13 Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
And he brought up from there [the] bones of Saul and [the] bones of Jonathan son his and they gathered [the] bones of the impaled [men].
14 Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
And they buried [the] bones of Saul and Jonathan son his in [the] land of Benjamin at Zela in [the] tomb of Kish father his and they did all that he commanded the king and he was entreated God for the land after thus.
15 Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
And it belonged again war to the Philistines with Israel and he went down David and servants his with him and they fought with [the] Philistines and he was weary David.
16 Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
(And Ishbi-*Q(K)*) Benob who - [was] among those born of the Raphah and [the] weight of spear his [was] three hundred [the] weight of bronze and he [was] girded a new [weapon] and he said to strike down David.
17 Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
And he helped him Abishai [the] son of Zeruiah and he struck the Philistine and he killed him then they swore [the] men of David to him saying not you will go out again with us for battle and not you will extinguish [the] lamp of Israel.
18 Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
And it was after thus and it was again war at Gob with [the] Philistines then he struck down Sibbecai the Hushathite Saph who [was] among those born of the Raphah.
19 Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
And it was again war at Gob with [the] Philistines and he struck down Elhanan [the] son of Jaare-Oregim [the] Beth-lehemite Goliath the Gittite and [the] wood of spear his [was] like a beam of weavers.
20 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
And it was again war at Gath and he was - a man of (stature *Q(K)*) and [the] fingers of hands his and [the] toes of feet his [were] six and six [was] twenty and four [the] number and also he he was born to the Raphah.
21 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
And he taunted Israel and he struck down him Jonathan [the] son of (Shimeah *Q(K)*) [the] brother of David.
22 Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Four these they were born to the Raphah in Gath and they fell by [the] hand of David and by [the] hand of servants his.

< 2 Samweli 21 >