< 2 Samweli 15 >

1 Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
И бысть по сих, и сотвори себе Авессалом колесницы и кони и пятьдесят муж текущих пред ним:
2 Akawa anaamka asubuhi na mapema na kusimama kando ya barabara inayoelekea kwenye lango la mji. Wakati wowote alipokuja mtu yeyote mwenye mashtaka yanayohitaji kuletwa mbele ya mfalme kwa maamuzi, Absalomu naye angemwita na kumuuliza, “Wewe unatoka mji upi?” Naye angejibu, “Mtumishi wako anatoka katika mojawapo ya makabila ya Israeli.”
и воставаше рано Авессалом, и стояше при самем пути врат: и бысть всяк муж, емуже бяше пря, прииде пред царя на суд, и возопи к нему Авессалом, и глаголаше ему: от коего града ты еси? И рече ему муж: от единаго колен Израилевых раб твой.
3 Kisha Absalomu angemwambia, “Tazama, malalamiko yako ni ya haki na sawasawa, lakini hakuna mwakilishi wa mfalme wa kukusikiliza.”
И рече к нему Авессалом: се, словеса твоя блага и удобна, но слушающаго несть ти от царя.
4 Absalomu aliongeza, “Laiti tu ningeteuliwa kuwa mwamuzi katika nchi. Ndipo kila mmoja mwenye mashtaka au shauri angekuja kwangu nami ningeona kwamba anapata haki.”
И рече Авессалом: кто мя поставит судию на земли, и ко мне приидет всяк муж имеяй прю и суд, и оправдаю его?
5 Pia, wakati mtu yeyote alipomkaribia ili kusujudu mbele yake, Absalomu alinyoosha mkono wake na kumshika pia kumbusu.
И бысть егда приближашеся муж поклонитися ему, и простираше руку свою, и приимаше его, и целоваше его.
6 Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
И сотвори Авессалом по глаголу сему всему Израилю приходящым на суд к царю и приусвои Авессалом сердца сынов Израилевых.
7 Mnamo mwisho wa mwaka wa nne, Absalomu akamwambia mfalme, “Naomba unipe ruhusa niende Hebroni nikatimize nadhiri niliyomwekea Bwana.
И бысть от конца четыредесяти лет, и рече Авессалом ко отцу своему: пойду ныне и воздам обеты моя, яже обещах Господу в Хевроне:
8 Wakati mtumishi wako alipokuwa huko Geshuri katika nchi ya Aramu, niliweka nadhiri hii, ‘Ikiwa Bwana atanirudisha Yerusalemu, nitamwabudu Bwana huko Hebroni.’”
зане обет обеща раб твой, егда жих в Гедсуре Сирийстем, глаголя: аще возвращая возвратит мя Господь во Иерусалим, и послужу Господу.
9 Mfalme akamwambia, “Enenda kwa amani.” Hivyo akaenda Hebroni.
И рече ему царь: иди с миром. И востав иде в Хеврон.
10 Kisha Absalomu akatuma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Israeli, kusema, “Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta basi semeni, ‘Absalomu ni mfalme huko Hebroni.’”
И посла Авессалом соглядатаи во вся колена Израилева, глаголя: егда услышите вы глас трубы рожаны, и рцыте: воцарися царь Авессалом в Хевроне.
11 Watu mia mbili kutoka Yerusalemu walikuwa wamefuatana na Absalomu. Walikuwa wamealikwa kama wageni nao walikwenda kwa nia njema, pasipo kujua lolote.
И идоша со Авессаломом двести мужей от Иерусалима позвани: и идяху в простоте своей, и не разумеша всякаго глагола.
12 Wakati Absalomu alipokuwa anatoa dhabihu, pia akatuma aitwe Ahithofeli, Mgiloni, mshauri wa Daudi, aje kutoka Gilo, ambao ndio mji wake wa nyumbani. Kwa hiyo mpango wa hila ukapata nguvu, na idadi ya waliofuatana na Absalomu ikaongezeka.
И посла Авессалом, и призва Ахитофела Галамонийскаго, советника Давидова, от града его Голамы, егда жряше жертвы. И бысть смятение крепко: и людий множество идущих со Авессаломом.
13 Mjumbe akaja na kumwambia Daudi, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
И прииде вестник к Давиду, глаголя: бысть сердце мужей Израилевых со Авессаломом.
14 Ndipo Daudi akawaambia maafisa wake wote waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Njooni! Ni lazima tukimbie, la sivyo hakuna hata mmoja wetu atakayeokoka kutoka mkononi mwa Absalomu. Ni lazima tuondoke kwa haraka, la sivyo atakuja mbio na kutupata, atatuangamiza na kuupiga mji kwa upanga.”
И рече Давид всем отроком своим сущым с ним во Иерусалиме: востаните, и бежим, яко несть нам спасения от лица Авессаломля: ускорите ити, да не ускорит и возмет нас, и наведет на нас злобу, и избиет град острием меча.
15 Maafisa wa mfalme wakamjibu, “Watumishi wako tu tayari kufanya lolote mfalme bwana wetu analochagua.”
И реша отроцы царевы к царю: вся елика заповесть господь наш царь, се, мы отроцы твои.
16 Mfalme akatoka, pamoja na watu wa nyumbani mwake wakimfuata; lakini akawaacha masuria kumi ili kuangalia jumba la kifalme.
И изыде царь и весь дом его ногами своими, и остави царь десять жен подложниц своих хранити дом.
17 Hivyo mfalme akaondoka, pamoja na watu wote wakimfuata, wakatua mahali mbali kiasi.
И изыде царь и вси отроцы его пеши и сташа в Дому Сущем Далече:
18 Watu wake wote wakatembea, wakampita wakiwa wamefuatana na Wakerethi na Wapelethi wote; pia Wagiti wote mia sita waliokuwa wamefuatana naye kutoka Gathi wakapita mbele ya mfalme.
и вси отроцы его от обою страну его идяху, и вси Хелефее и вси Фелефее и вси Гефее, шесть сот мужей шедше пеши от Гефа предидяху пред лицем царевым.
19 Mfalme akamwambia Itai, Mgiti, “Kwa nini ufuatane na sisi? Rudi ukakae pamoja na Mfalme Absalomu. Wewe ni mgeni, mkimbizi kutoka nchini mwako.
И рече царь ко Еффею Геффеину: почто и ты идеши с нами? Возвратися и живи с царем, яко чуждь еси ты, и яко преселился еси ты от места твоего:
20 Ulikuja jana tu. Nami leo nikufanye utangetange pamoja nasi, wakati sijui niendako? Rudi, nawe ukawachukue watu wa kwenu. Wema na uaminifu na viwe pamoja nawe.”
аще вчера пришел еси, и днесь ли подвигну тя ити с нами? И аз иду, аможе пойду: иди и возвратися, и возврати братию твою с тобою, и Господь да сотворит с тобою милость и истину.
21 Lakini Itai akamjibu mfalme, “Hakika kama Bwana aishivyo na kama mfalme bwana wangu aishivyo, popote mfalme bwana wangu atakapokuwa, ikiwa ni kuishi au kufa, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa.”
И отвеща Еффей к царю и рече: жив Господь, и жив господин мой царь, яко на месте, идеже будет господин мой царь, или в смерти, или в животе, тамо будет раб твой.
22 Daudi akamwambia Itai, “Songa mbele, endelea.” Kwa hiyo Itai, Mgiti, akaendelea pamoja na watu wake wote, pia jamaa zote waliokuwa pamoja naye.
И рече царь ко Еффею: гряди, и прейди со мною. И прейде Еффей Геффеин и царь и вси отроцы его и весь народ иже с ним.
23 Watu wote wa nje ya mji wakalia kwa sauti wakati watu wote walipokuwa wakipita. Mfalme naye akavuka Bonde la Kidroni, nao watu wote wakaelekea jangwani.
И вся земля плакашеся гласом великим. И вси людие прехождаху по потоку Кедрску, и царь прейде чрез поток Кедрский, и вси людие и царь идяху к лицу пути пустыннаго.
24 Sadoki pia alikuwako, kadhalika Walawi wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wamechukua Sanduku la Agano la Mungu. Wakaweka chini Sanduku la Mungu, naye Abiathari akatoa dhabihu mpaka watu wote walipokuwa wameondoka mjini.
И се, и Садок иерей и вси левити с ним, носяще кивот завета Господня от Вефары: и поставиша кивот Божий: и Авиафар взыде, дондеже престаша вси людие исходити из града.
25 Kisha mfalme akamwambia Sadoki, “Rudisha Sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitapata kibali mbele za Bwana, atanirudisha, nami nitaliona Sanduku hili tena pamoja na Maskani yake.
И рече царь к Садоку: возврати кивот Божий во град, и да станет на месте своем: аще обрящу благодать пред очима Господнима, и возвратит мя, и покажет ми его и лепоту его:
26 Lakini kama yeye atasema, ‘Mimi sipendezwi nawe,’ basi mimi niko tayari; yeye na anifanye chochote aonacho chema kwake.”
и аще тако речет: не благоволих в тебе: се, аз есмь, да сотворит ми по благому пред очима Своима.
27 Pia mfalme alimwambia kuhani Sadoki, “Je, wewe si mwonaji? Rudi mjini kwa amani pamoja na mwanao Ahimaasi na Yonathani mwana wa Abiathari. Wewe na Abiathari wachukueni wana wenu wawili.
И рече царь Садоку иерею: видите, ты возвращаешися во град с миром и Ахимаас сын твой и Ионафан сын Авиафаров, два сыны ваши с вами:
28 Nitasubiri kwenye vivuko katika jangwa mpaka neno litakapotoka kwenu kuniarifu.”
видите, аз вселяюся во аравоф пустынный, дондеже приидет ми слово от вас, еже возвестити ми.
29 Kwa hiyo Sadoki na Abiathari wakarudisha Sanduku la Mungu mpaka Yerusalemu na kukaa huko.
И возврати Садок и Авиафар кивот Божий во Иерусалим, и седе тамо.
30 Bali Daudi akaendelea, akapanda Mlima wa Mizeituni, akaenda huku analia, akiwa amefunika kichwa chake na bila viatu miguuni. Watu wote waliokuwa pamoja naye nao wakafunika vichwa vyao, wakawa wanapanda mlima huku wanalia.
И Давид восхождаше восходом на гору Елеонскую восходя и плачася, и покрыв главу свою, и сам идяше босыма ногама: и вси людие иже с ним покрыша кийждо главу свою, и восхождаху восходяще и плачущеся.
31 Basi Daudi alikuwa ameambiwa, “Ahithofeli alikuwa miongoni mwa washiriki wa shauri baya la Absalomu.” Ndipo Daudi akaomba, akisema, “Ee Bwana, geuza shauri la Ahithofeli kuwa ujinga.”
И возвестиша Давиду глаголюще: и Ахитофел в мятежницех со Авессаломом. И рече Давид: разруши совет Ахитофелев, Господи, Боже мой.
32 Daudi alipofika kwenye kilele cha mlima, mahali ambapo watu walikuwa wamezoea kumwabudu Mungu, Hushai, Mwariki, alikuwako huko kumlaki, joho lake likiwa limeraruka na mavumbi kichwani mwake.
И бе Давид грядый даже до роса, идеже поклонися Богу. И се, на сретение ему (изыде) Хусий первый друг Давидов, растерзав ризы своя, и персть на главе его.
33 Daudi akamwambia, “Kama ukienda pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu.
И рече ему Давид: аще пойдеши со мною, и будеши ми в тягость:
34 Lakini ikiwa utarudi mjini na kumwambia Absalomu, ‘Nitakuwa mtumishi wako, ee mfalme; nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati uliopita, lakini sasa nitakuwa mtumishi wako,’ basi utaweza kunisaidia kwa kupinga shauri la Ahithofeli.
аще же возвратишися во град и речеши Авессалому: минуша братия твоя, и царь за мною мину отец твой, и ныне раб твой есмь, царю, пощади мя жива быти: раб бех отца твоего тогда и доселе, ныне же аз твой раб: и разруши ми совет Ахитофелев:
35 Je, makuhani Sadoki na Abiathari hawatakuwa pamoja nawe? Waambie lolote utakalosikia katika jumba la mfalme.
и се, с тобою тамо Садок и Авиафар иерее: и будет всяк глагол, егоже услышиши из уст царских, и скажеши Садоку и Авиафару иереем:
36 Wana wao wawili, Ahimaasi mwana wa Sadoki na Yonathani mwana wa Abiathari, wako pamoja nao huko. Watume kwangu na lolote utakalosikia.”
се, тамо с ними два сына их, Ахимаас сын Садоков и Ионафан сын Авиафаров: и послите рукою их ко мне всяк глагол, егоже аще услышите.
37 Kwa hiyo Hushai, rafiki wa Daudi, akafika Yerusalemu wakati Absalomu alipokuwa anaingia mjini.
И вниде Хусий друг Давидов во град, и Авессалом тогда вхождаше во Иерусалим.

< 2 Samweli 15 >