< 2 Samweli 15 >

1 Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
And it was from after thus and he acquired for himself Absalom a chariot and horses and fifty man [who] ran before him.
2 Akawa anaamka asubuhi na mapema na kusimama kando ya barabara inayoelekea kwenye lango la mji. Wakati wowote alipokuja mtu yeyote mwenye mashtaka yanayohitaji kuletwa mbele ya mfalme kwa maamuzi, Absalomu naye angemwita na kumuuliza, “Wewe unatoka mji upi?” Naye angejibu, “Mtumishi wako anatoka katika mojawapo ya makabila ya Israeli.”
And he rose early Absalom and he stood at [the] side of [the] road of the gate and it was every person whom it belonged to him a case at law to come to the king for judgment and he called out Absalom to him and he said where? from this city [are] you and he said [is] from one of [the] tribes of Israel servant your.
3 Kisha Absalomu angemwambia, “Tazama, malalamiko yako ni ya haki na sawasawa, lakini hakuna mwakilishi wa mfalme wa kukusikiliza.”
And he said to him Absalom see matter your [are] good and right and [one who] hears not [belongs] to you from with the king.
4 Absalomu aliongeza, “Laiti tu ningeteuliwa kuwa mwamuzi katika nchi. Ndipo kila mmoja mwenye mashtaka au shauri angekuja kwangu nami ningeona kwamba anapata haki.”
And he said Absalom who? will he make me a judge in the land and to me he will come every person whom it belongs to him a case at law and a judgment and I will do justice him.
5 Pia, wakati mtu yeyote alipomkaribia ili kusujudu mbele yake, Absalomu alinyoosha mkono wake na kumshika pia kumbusu.
And it was when drew near anyone to bow down to him and he stretched out hand his and he took hold of him and he kissed him.
6 Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
And he did Absalom according to the manner this to all Israel who they came for judgment to the king and he stole Absalom [the] heart of [the] men of Israel.
7 Mnamo mwisho wa mwaka wa nne, Absalomu akamwambia mfalme, “Naomba unipe ruhusa niende Hebroni nikatimize nadhiri niliyomwekea Bwana.
And it was from [the] end of forty year[s] and he said Absalom to the king let me go please so I may pay vow my which I vowed to Yahweh in Hebron.
8 Wakati mtumishi wako alipokuwa huko Geshuri katika nchi ya Aramu, niliweka nadhiri hii, ‘Ikiwa Bwana atanirudisha Yerusalemu, nitamwabudu Bwana huko Hebroni.’”
For a vow he vowed servant your when dwelt I at Geshur in Aram saying if (certainly *Q(K)*) he will bring back me Yahweh Jerusalem and I will serve Yahweh (in Hebron. *X*)
9 Mfalme akamwambia, “Enenda kwa amani.” Hivyo akaenda Hebroni.
And he said to him the king go in peace and he arose and he went Hebron towards.
10 Kisha Absalomu akatuma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Israeli, kusema, “Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta basi semeni, ‘Absalomu ni mfalme huko Hebroni.’”
And he sent Absalom spies in all [the] tribes of Israel saying when hear you [the] sound of the ram's horn and you will say he has become king Absalom in Hebron.
11 Watu mia mbili kutoka Yerusalemu walikuwa wamefuatana na Absalomu. Walikuwa wamealikwa kama wageni nao walikwenda kwa nia njema, pasipo kujua lolote.
And with Absalom they went two hundred man from Jerusalem [those who] were invited and [those who] were going to innocence their and not they knew any thing.
12 Wakati Absalomu alipokuwa anatoa dhabihu, pia akatuma aitwe Ahithofeli, Mgiloni, mshauri wa Daudi, aje kutoka Gilo, ambao ndio mji wake wa nyumbani. Kwa hiyo mpango wa hila ukapata nguvu, na idadi ya waliofuatana na Absalomu ikaongezeka.
And he sent Absalom Ahithophel the Gilonite [the] counselor of David from city his from Giloh when sacrificed he the sacrifices and it was the conspiracy strong and the people [was] going and numerous with Absalom.
13 Mjumbe akaja na kumwambia Daudi, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
And he came the messenger to David saying it is [the] heart of [the] man of Israel after Absalom.
14 Ndipo Daudi akawaambia maafisa wake wote waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Njooni! Ni lazima tukimbie, la sivyo hakuna hata mmoja wetu atakayeokoka kutoka mkononi mwa Absalomu. Ni lazima tuondoke kwa haraka, la sivyo atakuja mbio na kutupata, atatuangamiza na kuupiga mji kwa upanga.”
And he said David to all servants his who [were] with him in Jerusalem arise so let us flee for not it will belong to us an escape from before Absalom hurry to go lest he should hurry and he will overtake us and he will thrust on us calamity and he will strike the city to [the] mouth of [the] sword.
15 Maafisa wa mfalme wakamjibu, “Watumishi wako tu tayari kufanya lolote mfalme bwana wetu analochagua.”
And they said [the] servants of the king to the king according to all that he will choose lord my the king here! [are] servants your.
16 Mfalme akatoka, pamoja na watu wa nyumbani mwake wakimfuata; lakini akawaacha masuria kumi ili kuangalia jumba la kifalme.
And he went out the king and all household his at feet his and he left the king ten women concubines to keep the house.
17 Hivyo mfalme akaondoka, pamoja na watu wote wakimfuata, wakatua mahali mbali kiasi.
And he went out the king and all the people at feet his and they stood [the] house of the distance.
18 Watu wake wote wakatembea, wakampita wakiwa wamefuatana na Wakerethi na Wapelethi wote; pia Wagiti wote mia sita waliokuwa wamefuatana naye kutoka Gathi wakapita mbele ya mfalme.
And all servants his [were] passing by at side his and all the Kerethite[s] and all the Pelethite[s] and all the Gittites six hundred man who they had come at foot his from Gath [were] passing by at [the] face of the king.
19 Mfalme akamwambia Itai, Mgiti, “Kwa nini ufuatane na sisi? Rudi ukakae pamoja na Mfalme Absalomu. Wewe ni mgeni, mkimbizi kutoka nchini mwako.
And he said the king to Ittai the Gittite why? will you go also you with us return and dwell with the king for [are] a foreigner you and also [are] an exile you to place your.
20 Ulikuja jana tu. Nami leo nikufanye utangetange pamoja nasi, wakati sijui niendako? Rudi, nawe ukawachukue watu wa kwenu. Wema na uaminifu na viwe pamoja nawe.”
[was] yesterday - Coming you and this day (will I make wander? you *Q(K)*) with us to go and I [am] going to where I [am] going return and take back brothers your [be] with you covenant loyalty and truth.
21 Lakini Itai akamjibu mfalme, “Hakika kama Bwana aishivyo na kama mfalme bwana wangu aishivyo, popote mfalme bwana wangu atakapokuwa, ikiwa ni kuishi au kufa, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa.”
And he answered Ittai the king and he said [by] [the] life of Yahweh and [by] [the] life of lord my the king that except in [the] place where he will be there - lord my the king whether for death or for life for there he will be servant your.
22 Daudi akamwambia Itai, “Songa mbele, endelea.” Kwa hiyo Itai, Mgiti, akaendelea pamoja na watu wake wote, pia jamaa zote waliokuwa pamoja naye.
And he said David to Ittai come and pass on and he passed on Ittai the Gittite and all men his and all the little one[s] who [were] with him.
23 Watu wote wa nje ya mji wakalia kwa sauti wakati watu wote walipokuwa wakipita. Mfalme naye akavuka Bonde la Kidroni, nao watu wote wakaelekea jangwani.
And all the land [were] weeping a voice great and all the people [were] passing by and the king [was] passing in [the] wadi of Kidron and all the people [were] passing on on [the] face of [the] road the wilderness.
24 Sadoki pia alikuwako, kadhalika Walawi wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wamechukua Sanduku la Agano la Mungu. Wakaweka chini Sanduku la Mungu, naye Abiathari akatoa dhabihu mpaka watu wote walipokuwa wameondoka mjini.
And there! also Zadok and all the Levites with him [were] carrying [the] ark of [the] covenant of God and they set down [the] ark of God and he went up Abiathar until was finished all the people to pass out from the city.
25 Kisha mfalme akamwambia Sadoki, “Rudisha Sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitapata kibali mbele za Bwana, atanirudisha, nami nitaliona Sanduku hili tena pamoja na Maskani yake.
And he said the king to Zadok take back [the] ark of God the city if I will find favor in [the] eyes of Yahweh and he will bring back me and he will show me it and habitation his.
26 Lakini kama yeye atasema, ‘Mimi sipendezwi nawe,’ basi mimi niko tayari; yeye na anifanye chochote aonacho chema kwake.”
And if thus he will say not I delight in you here [am] I let him do to me just as it is good in view his.
27 Pia mfalme alimwambia kuhani Sadoki, “Je, wewe si mwonaji? Rudi mjini kwa amani pamoja na mwanao Ahimaasi na Yonathani mwana wa Abiathari. Wewe na Abiathari wachukueni wana wenu wawili.
And he said the king to Zadok the priest ¿ a seer [are] you return! the city in peace and Ahimaaz son your and Jonathan [the] son of Abiathar [the] two sons your with you.
28 Nitasubiri kwenye vivuko katika jangwa mpaka neno litakapotoka kwenu kuniarifu.”
See I [will] delay (in [the] desert plains of *Q(K)*) the wilderness until comes word from with you to tell to me.
29 Kwa hiyo Sadoki na Abiathari wakarudisha Sanduku la Mungu mpaka Yerusalemu na kukaa huko.
And he took back Zadok and Abiathar [the] ark of God Jerusalem and they remained there.
30 Bali Daudi akaendelea, akapanda Mlima wa Mizeituni, akaenda huku analia, akiwa amefunika kichwa chake na bila viatu miguuni. Watu wote waliokuwa pamoja naye nao wakafunika vichwa vyao, wakawa wanapanda mlima huku wanalia.
And David [was] going up on [the] ascent of the olive trees going up - and weeping and head of him [was] covered and he [was] walking barefoot and all the people which [was] with him they covered each head his and they went up continuously and wept.
31 Basi Daudi alikuwa ameambiwa, “Ahithofeli alikuwa miongoni mwa washiriki wa shauri baya la Absalomu.” Ndipo Daudi akaomba, akisema, “Ee Bwana, geuza shauri la Ahithofeli kuwa ujinga.”
And David someone told saying Ahithophel [is] among the conspirators with Absalom and he said David make foolish please [the] counsel of Ahithophel O Yahweh.
32 Daudi alipofika kwenye kilele cha mlima, mahali ambapo watu walikuwa wamezoea kumwabudu Mungu, Hushai, Mwariki, alikuwako huko kumlaki, joho lake likiwa limeraruka na mavumbi kichwani mwake.
And he was David coming to the top where he bowed down there to God and there! to meet him Hushai the Arkite [was] torn tunic his and earth [was] on head his.
33 Daudi akamwambia, “Kama ukienda pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu.
And he said to him David if you pass over with me and you will become on me a burden.
34 Lakini ikiwa utarudi mjini na kumwambia Absalomu, ‘Nitakuwa mtumishi wako, ee mfalme; nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati uliopita, lakini sasa nitakuwa mtumishi wako,’ basi utaweza kunisaidia kwa kupinga shauri la Ahithofeli.
And if the city you will return and you will say to Absalom servant your I O king I will be [was] [the] servant of father your I from then and now I [will be] servant your and you will frustrate for me [the] counsel of Ahithophel.
35 Je, makuhani Sadoki na Abiathari hawatakuwa pamoja nawe? Waambie lolote utakalosikia katika jumba la mfalme.
And ¿ not with you there [are] Zadok and Abiathar the priests and it will be every word which you will hear from [the] house of the king you will tell to Zadok and to Abiathar the priests.
36 Wana wao wawili, Ahimaasi mwana wa Sadoki na Yonathani mwana wa Abiathari, wako pamoja nao huko. Watume kwangu na lolote utakalosikia.”
There! there [are] with them [the] two sons their Ahimaaz of Zadok and Jonathan of Abiathar and you will send by hand their to me every word which you will hear.
37 Kwa hiyo Hushai, rafiki wa Daudi, akafika Yerusalemu wakati Absalomu alipokuwa anaingia mjini.
And he came Hushai [the] friend of David the city and Absalom he came Jerusalem.

< 2 Samweli 15 >