< 2 Samweli 11 >
1 Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
Au retour de l'année, au moment où les rois sortent, David envoya avec lui Joab et ses serviteurs, et tout Israël; ils détruisirent les fils d'Ammon et assiégèrent Rabba. Mais David resta à Jérusalem.
2 Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
Le soir, David se leva de son lit et se promena sur le toit de la maison du roi. Du toit, il vit une femme qui se baignait, et cette femme était très belle à voir.
3 naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
David envoya demander des nouvelles de cette femme. On lui dit: « N'est-ce pas Bethsabée, fille d'Eliam, la femme d'Urie le Héthien? »
4 Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
David envoya des messagers, qui la prirent; elle entra chez lui, et il coucha avec elle (car elle était purifiée de son impureté); puis elle retourna dans sa maison.
5 Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
La femme devint enceinte; elle envoya avertir David, et dit: « Je suis enceinte. »
6 Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
David envoya dire à Joab: « Envoie-moi Urie, le Hittite. » Joab envoya Urie à David.
7 Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
Lorsque Urie fut arrivé auprès de lui, David lui demanda comment allait Joab, comment se portait le peuple et comment la guerre avait prospéré.
8 Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
David dit à Urie: « Descends dans ta maison et lave-toi les pieds. » Urie sortit de la maison du roi, et un présent du roi fut envoyé après lui.
9 Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
Mais Urie se coucha à l'entrée de la maison du roi avec tous les serviteurs de son maître, et il ne descendit pas dans sa maison.
10 Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
Lorsqu'on eut dit à David: « Urie n'est pas descendu dans sa maison », David dit à Urie: « Ne reviens-tu pas d'un voyage? Pourquoi n'es-tu pas descendu dans ta maison? »
11 Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
Urie dit à David: « L'arche, Israël et Juda sont sous des tentes, et mon seigneur Joab et les serviteurs de mon seigneur campent en plein champ. Irai-je donc dans ma maison pour manger et boire, et pour coucher avec ma femme? Aussi longtemps que tu vivras et que ton âme vivra, je ne ferai pas cela! ».
12 Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
David dit à Urie: « Reste ici aujourd'hui encore, et demain je te laisserai partir. » Urie resta donc à Jérusalem ce jour-là et le lendemain.
13 Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
Lorsque David l'eut appelé, il mangea et but en sa présence, et il le fit boire. Le soir, il sortit pour se coucher sur son lit avec les serviteurs de son seigneur, mais il ne descendit pas dans sa maison.
14 Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
Le matin, David écrivit une lettre à Joab et l'envoya par la main d'Urie.
15 Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
Il écrivit dans la lettre: « Envoie Urie au premier rang du combat le plus acharné, et retire-toi de lui, afin qu'il soit frappé et qu'il meure. »
16 Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
Joab, qui surveillait la ville, plaça Urie à l'endroit où il savait qu'il y avait des hommes vaillants.
17 Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
Les hommes de la ville sortirent et se battirent avec Joab. Une partie du peuple tomba, même des serviteurs de David, et Urie, le Hittite, mourut aussi.
18 Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
Joab envoya raconter à David tout ce qui s'était passé pendant la guerre.
19 Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
Il donna cet ordre au messager: « Quand tu auras fini de raconter au roi tout ce qui s'est passé pendant la guerre,
20 hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
si la colère du roi se manifeste et qu'il te demande: « Pourquoi t'es-tu approché de la ville pour combattre? Ne savais-tu pas qu'on tirerait du haut de la muraille?
21 Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
Qui a frappé Abimélec, fils de Jerubbesheth? Une femme n'a-t-elle pas jeté sur lui, du haut de la muraille, une meule de moulin, de sorte qu'il est mort à Thèbes? Pourquoi t'es-tu approché de la muraille? Tu diras alors: « Ton serviteur Urie, le Héthien, est mort lui aussi ».
22 Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
Le messager partit, et vint montrer à David tout ce que Joab lui avait envoyé chercher.
23 Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
Le messager dit à David: « Les hommes ont eu raison de nous, ils sont sortis dans les champs, et nous les avons poursuivis jusqu'à l'entrée de la porte.
24 Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
Les tireurs ont tiré sur tes serviteurs du côté de la muraille; certains des serviteurs du roi sont morts, et ton serviteur Urie le Hittite est également mort. »
25 Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
David dit au messager: « Dis à Joab: « Que cela ne te déplaise, car l'épée dévore aussi bien les uns que les autres. Fortifie ton combat contre la ville, et renverse-la ». Encourage-le. »
26 Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
Lorsque la femme d'Urie apprit qu'Urie, son mari, était mort, elle porta le deuil de son mari.
27 Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.
Lorsque le deuil fut terminé, David l'envoya chercher et la prit dans sa maison; elle devint sa femme et lui donna un fils. Mais ce que David avait fait déplut à Yahvé.