< 2 Wafalme 7 >

1 Elisha akasema, “Sikiliza neno la Bwana. Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
And he said Elisha hear [the] word of Yahweh thus - he says Yahweh about this time - tomorrow a seah of fine flour for a shekel and two seahs barley for a shekel at [the] gate of Samaria.
2 Yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake akamwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Elisha akajibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
And he answered the officer who [belonged] to the king [who] was leaning on hand his [the] man of God and he said here! Yahweh [is] making windows in the heavens ¿ will it happen the thing this and he said here you [are] about to see with own eyes your and from there not you will eat.
3 Basi kulikuwepo na watu wanne wenye ukoma katika ingilio la lango la mji. Wakaambiana, “Kwa nini tukae hapa mpaka tufe?
And four men they were [people] having a skin disease [the] entrance of the gate and they said each to neighbor his why? [are] we sitting here until we have died.
4 Kama tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Kama tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kwenye kambi ya Waaramu na tujisalimishe. Kama wakituacha hai, tutaishi; kama wakituua, basi na tufe.”
If we said we will enter the city and the famine [is] in the city and we will die there and if we sat here and we will die and therefore come so let us fall to [the] camp of Aram if they will let live us we will live and if they will put to death us and we will die.
5 Wakati wa giza la jioni, wakaondoka na kwenda kwenye kambi ya Waaramu. Walipofika mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu,
And they arose at twilight to go to [the] camp of Aram and they came to [the] edge of [the] camp of Aram and there! there not there [was] anyone.
6 kwa kuwa Bwana alilifanya jeshi la Waaramu lisikie sauti kama ya magari ya vita, farasi na jeshi kubwa, kiasi kwamba waliambiana, “Tazama, mfalme wa Israeli ameajiri mfalme wa Wahiti na mfalme wa Wamisri kuja kutushambulia sisi!”
And [the] Lord he had caused to hear - [the] camp of Aram a sound of chariotry a sound of horse[s] a sound of an army large and they said each to brother his here! he has hired on us [the] king of Israel [the] kings of the Hittites and [the] kings of Egypt to come on us.
7 Kwa hiyo wakaondoka na kukimbia wakati wa giza la jioni na kuacha mahema yao, farasi wao na punda wao. Wakakimbia kuokoa maisha yao na kuacha kila kitu ndani ya kambi kama kilivyokuwa.
And they arose and they fled at twilight and they abandoned tents their and horses their and donkeys their the camp [was] just as it [was] and they fled to life their.
8 Wale watu wenye ukoma walipofika mwanzoni mwa kambi, wakaingia kwenye mojawapo ya mahema. Wakala na kunywa, na kuchukua fedha, dhahabu na nguo, wakaenda kuvificha. Wakarudi na kuingia katika hema jingine, na kuchukua baadhi ya vitu kutoka ndani yake na kuvificha pia.
And they came the [people] having a skin disease these to [the] edge of the camp and they went into a tent one and they ate and they drank and they carried off from there silver and gold and clothes and they went and they hid [them] and they returned and they went into a tent another and they carried off [things] from there and they went and they hid [them].
9 Kisha wakaambiana, “Hili tunalolifanya sio jema. Hii ni siku ya habari njema, nasi tunakaa kimya. Kama tukisubiri mpaka mapambazuko, maafa yatatupata. Twendeni mara moja tukatoe habari hizi katika jumba la mfalme.”
And they said each to neighbor his not right - we [are] doing the day this [is] a day of good news it and we [are] silent and we will delay until [the] light of the morning and it will find us punishment and therefore come so let us go and let us tell [the] household of the king.
10 Hivyo wakaenda mjini na kuwaita walinzi wa langoni, wakawaambia, “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu lakini hapakuwepo na mtu huko, hata sauti ya mtu yeyote, ila farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.”
And they went and they called out to [the] gatekeeper of the city and they told to them saying we went into [the] camp of Aram and there! there not there [was] anyone and [the] sound of anyone that except the horse[s] tied up and the donkey[s] tied up and tents [are] just as they [were].
11 Walinzi wa langoni wakatangaza habari ile kwa sauti kuu, na taarifa hii ikatolewa ndani ya jumba la mfalme.
And he called out the gatekeepers and they told [the] household of the king within.
12 Mfalme akaamka usiku na kuwaambia maafisa wake, “Nitawaambia kile Waaramu walichotufanyia. Wanajua kwamba tuna njaa, hivyo wameacha kambi yao ili kujificha mashambani, wakifikiri, ‘Kwa hakika watatoka nje ya mji, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia ndani ya mji.’”
And he arose the king night and he said to servants his let me tell please to you [that] which they have done to us Aram they know that [are] hungry we and they have gone out from the camp to hide themselves (in open country *Q(K)*) saying that they will come out from the city and we will seize them alive and into the city we will go.
13 Mmoja wa maafisa wake akajibu, “Waamuru watu wachache wakawachukue farasi watano kati ya wale waliobaki katika mji. Hatima yao itakuwa kama ya Waisraeli wote walio hapa. Watakuwa tu kama Waisraeli hawa ambao wanangoja kifo. Hivyo tuwatumeni wajue kumetendeka nini.”
And he answered one from servants his and he said and they may take please five of the horses remaining which they are left in it here they [will be] like all ([the] multitude of *Q(K)*) Israel which they are left in it here they [will be] like all [the] multitude of Israel which they have come to an end and let us send and we may see.
14 Ndipo wakachagua magari mawili ya vita pamoja na farasi wake, naye mfalme akawatuma wafuatilie jeshi la Waaramu. Akawaamuru waendeshaji akisema, “Nendeni mkaone ni nini kilichotokea.”
And people took two chariot[s] horses and he sent [them] the king after [the] camp of Aram saying go and see.
15 Wakawafuatia hadi Yordani, nao wakakuta barabara yote ikiwa imetapakaa nguo na vyombo vya Waaramu walivyokuwa wamevitupa walipokuwa wanatoroka. Basi wale wajumbe wakarudi na kutoa taarifa kwa mfalme.
And they went after them to the Jordan and there! all the road [was] full clothes and equipment which they had thrown away Aram (in hurrying of them *Q(K)*) and they returned the messengers and they told to the king.
16 Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
And it went out the people and they plundered [the] camp of Aram and it was a seah of fine flour for a shekel and two seahs barley for a shekel according to [the] word of Yahweh.
17 Basi mfalme alikuwa amemweka yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake awe msimamizi wa lango. Nao watu wakamkanyaga walipoingia langoni, naye akafa, kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa ametangulia kusema wakati mfalme alipofika nyumbani kwake.
And the king he appointed the officer who [was] leaning on hand his over the gate and they trampled him the people in the gate and he died just as he had spoken [the] man of God who he spoke when came down the king to him.
18 Ikatokea kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia mfalme: “Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
And it was as had spoken [the] man of God to the king saying two seahs barley for a shekel and a seah of fine flour for a shekel it will be about this time tomorrow in [the] gate of Samaria.
19 Yule afisa alikuwa amemwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Naye yule mtu wa Mungu alikuwa amemjibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
And he had answered the officer [the] man of God and he said and here! Yahweh [is] making windows in the heavens ¿ will it happen according to the manner this and he said here you [are] about to see with own eyes your and from there not you will eat.
20 Ndivyo hasa ilivyotokea kwake, kwa kuwa watu walimkanyaga langoni, naye akafa.
And it happened to him thus and they trampled him the people in the gate and he died.

< 2 Wafalme 7 >