< 2 Wafalme 23 >

1 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
And he sent the king and they gathered to him all [the] elders of Judah and Jerusalem.
2 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
And he went up the king [the] house of Yahweh and every person of Judah and all [the] inhabitants of Jerusalem with him and the priests and the prophets and all the people from [the] small and unto [the] great and he read aloud in ears their all [the] words of [the] scroll of the covenant which had been found in [the] house of Yahweh.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
And he stood the king at the pillar and he made the covenant - before Yahweh to walk after Yahweh and to keep commandments his and testimonies his and statutes his with all heart and with all being to establish [the] words of the covenant this which were written on the scroll this and it took its stand all the people in the covenant.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
And he commanded the king Hilkiah the priest great and [the] priests of the second rank and [the] keepers of the threshold to bring out from [the] temple of Yahweh all the articles which were made for Baal and for Asherah and for all [the] host of the heavens and he burned them from [the] outside of Jerusalem in [the] fields of Kidron and he carried dust their Beth-el.
5 Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
And he removed the pagan priests whom they had appointed [the] kings of Judah and he made smoke at the high places in [the] cities of Judah and [the] surroundings of Jerusalem and the [ones who] made smoke to Baal to the sun and to the moon and to the constellations and to all [the] host of the heavens.
6 Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
And he brought out the Asherah pole from [the] house of Yahweh from [the] outside of Jerusalem to [the] wadi of Kidron and he burned it in [the] wadi of Kidron and he crushed [it] to dust and he threw dust its on [the] burial site of [the] sons of the people.
7 Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
And he broke down [the] houses of the male cult prostitutes which [were] in [the] house of Yahweh where the women [were] weaving there containers for Asherah.
8 Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
And he brought all the priests from [the] cities of Judah and he made unclean the high places where they had made smoke there the priests from Geba to Beer Sheba and he broke down [the] high places of the gates which [were at] [the] entrance of [the] gate of Joshua [the] governor of the city which [was] at [the] left [side] of anyone at [the] gate of the city.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Nevertheless not they went up [the] priests of the high places to [the] altar of Yahweh in Jerusalem that except they ate unleavened bread in among brothers their.
10 Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
And he made unclean Topheth which [was] in [the] valley of (Ben *Q(K)*) Hinnom to not to make pass anyone son his and daughter his in the fire to Molech.
11 Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
And he removed the horses which they had dedicated [the] kings of Judah to the sun from [the] going of [the] house of Yahweh to [the] room of Nathan Melech the court-official which [was] in the Parbar and [the] chariots of the sun he burned with fire.
12 Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
And the altars which [were] on the roof of [the] upper room of Ahaz which they had made - [the] kings of Judah and the altars which he had made Manasseh in [the] two [the] courtyards of [the] house of Yahweh he pulled down the king and he ran from there and he threw dust their into [the] wadi of Kidron.
13 Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
And the high places which - [were] on [the] face of Jerusalem which [were] from [the] south of [the] mountain of destruction which he had built Solomon [the] king of Israel to Astarte - [the] detestable thing of [the] Sidonians and to Chemosh [the] detestable thing of Moab and to Milcom [the] abomination of [the] people of Ammon he made unclean the king.
14 Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
And he broke the sacred pillars and he cut down the Asherah poles and he filled place their bones of humankind.
15 Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
And also the altar which [was] at Beth-el the high place which he had made Jeroboam [the] son of Nebat who he caused to sin Israel also the altar that and the high place he tore down and he burned the high place he crushed [it] to dust and he burned [the] Asherah pole.
16 Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
And he turned Josiah and he saw the graves which [were] there on the mountain and he sent and he took the bones from the graves and he burned [them] on the altar and he made unclean it according to [the] word of Yahweh which he had proclaimed [the] man of God who he proclaimed the words these.
17 Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
And he said what? [is] the monument this which I [am] seeing and they said to him [the] people of the city the grave of [the] man of God who he came from Judah and he proclaimed the things these which you have done on the altar of Beth-el.
18 Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
And he said leave alone him anyone may not he disturb bones his and they left undisturbed bones his [the] bones of the prophet who he had come from Samaria.
19 Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
And also all [the] houses of the high places which - [were] in [the] cities of Samaria which they had made [the] kings of Israel to provoke anger he removed Josiah and he did to them according to all the deeds which he had done at Beth-el.
20 Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
And he slaughtered all [the] priests of the high places who [were] there on the altars and he burned bones of humankind on them and he returned Jerusalem.
21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
And he commanded the king all the people saying observe a passover to Yahweh God your according to [what] is written on [the] scroll of the covenant this.
22 Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
For not it had been observed like the passover this since [the] days of the judges who they judged Israel and all [the] days of [the] kings of Israel and [the] kings of Judah.
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
That except in eight-teen year of the king Josiah it was observed the passover this to Yahweh in Jerusalem.
24 Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
And also the necromancers and the soothsayers and the teraphim and the idols and all the detestable things which they were seen in [the] land of Judah and in Jerusalem he removed Josiah so as to carry out [the] words of the law which were written on the scroll which he had found Hilkiah the priest [the] house of Yahweh.
25 Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
And like him not he had been before him a king who he turned back to Yahweh with all heart his and with all being his and with all strength his according to all [the] law of Moses and after him not he arose like him.
26 Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
Nevertheless - not he turned back Yahweh from [the] burning of anger his great which it burned anger his on Judah on all the provocations which he had provoked to anger him Manasseh.
27 Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
And he said Yahweh also Judah I will remove from on face my just as I removed Israel and I will reject the city this which I chose Jerusalem and the house which I said it will be name my there.
28 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Josiah and all that he did ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
29 Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
In days his he went up Pharaoh Necho [the] king of Egypt on [the] king of Assyria to [the] river of Euphrates and he went the king Josiah to meet him and he killed him at Megiddo when saw he him.
30 Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
And they made ride him servants his dead from Megiddo and they brought him Jerusalem and they buried him in own grave his and it took [the] people of the land Jehoahaz [the] son of Josiah and they anointed him and they made king him in place of father his.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
[was] a son of Twenty and three year[s] Jehoahaz when became king he and three months he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Hamutal [the] daughter of Jeremiah from Libnah.
32 Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh according to all that they had done ancestors his.
33 Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
And he confined him Pharaoh Necho at Riblah in [the] land of Hamath (from reigning *Q(K)*) in Jerusalem and he put a fine on the land one hundred talent[s] of silver and a talent of gold.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
And he made king Pharaoh Necho Eliakim [the] son of Josiah in place of Josiah father his and he changed name his Jehoiakim and Jehoahaz he took and he came Egypt and he died there.
35 Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
And the silver and the gold he gave Jehoiakim to Pharaoh only he taxed the land to give the silver on [the] mouth of Pharaoh each according to valuation his he exacted the silver and the gold [the] people of the land to give [it] to Pharaoh Necho.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
[was] a son of Twenty and five year[s] Jehoiakim when became king he and one [plus] ten year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his ([was] Zebudah *Q(K)*) [the] daughter of Pedaiah from Rumah.
37 Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh according to all that they had done ancestors his.

< 2 Wafalme 23 >