< 2 Wafalme 14 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
Roku wtórego Joaza, syna Joachaza, króla Izraelskiego, począł królować Amazyjasz, syn Joaza, króla Judzkiego.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
Dwadzieścia i pięć lat miał, gdy królować począł, a dwadzieścia i dziewięć lat królował w Jeruzalemie. Imię matki jego było Joadana z Jeruzalemu.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
Ten czynił, co dobrego jest przed oczyma Pańskiemi, aczkolwiek nie tak jako Dawid, ojciec jego; według wszystkiego, co czynił Joaz, ojciec jego, postępował.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Wszakże wyżyny nie były zniesione; jeszcze lud ofiarował i kadził po wyżynach.
5 Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
A gdy zmocnione było królestwo w ręku jego, pobił sługi swe, którzy byli zabili króla, ojca jego.
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose ambako Bwana aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
Lecz synów onych morderców nie pobił, jako napisano w księgach zakonu Mojżeszowego, gdzie rozkazał Pan, mówiąc: Nie pomrą ojcowie za synów, ani synowie pomrą za ojców, ale każdy za grzech swój umrze.
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
Ten też poraził Edomczyków dziesięć tysięcy w dolinie solnej, i wziął mocą Selę, a nazwał imię jej Jokteel, aż do tego czasu.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane uso kwa uso.”
Tedy posłał Amazyjasz posły do Joaza, syna Joachaza, syna Jehu, króla Izraelskiego, mówiąc: Pójdź, wejrzymy sobie w oczy.
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
Posłał zasię Joaz, król Izraelski, do Amazyjasza, króla Judzkiego, mówiąc: Oset, który jest na Libanie, posłał do cedru Libańskiego, mówiąc: Daj córkę twoję synowi memu za żonę. Wtem przyszedł zwierz polny, który jest na Libanie, i podeptał on oset.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
Żeś ty bardzo poraził Edomczyki, dlatego się podniosło serce twoje. Chlubże się, a siedź w domu twoim; i przeczże się masz wdawać w to złe, abyś upadł ty, i Juda z tobą?
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
Ale nie usłuchał Amazyjasz. Przetoż wyciągnął Joaz, król Izraelski, a wejrzeli sobie w oczy, on i Amazyjasz, król Judzki, w Betsemes, które jest w Judztwie.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
I porażony jest Juda od ludu Izraelskiego, a uciekł każdy do przybytku swego.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
Lecz Amazyjasza, króla Judzkiego, syna Joaza, syna Ochozyjaszowego, pojmał Joaz, król Izraelski, w Betsemes, a przyciągnąwszy do Jeruzalemu, zburzył mur Jeruzalemski od bramy Efraim aż do bramy narożnej, na cztery sta łokci.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
I zabrał wszystko złoto i srebro i wszystkie naczynia, które się znalazły w domu Pańskim, i w skarbach domu królewskiego, i ludzie zastawne, i wrócił się do Samaryi.
15 Matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
A inne sprawy Joazowe, które czynił, i moc jego, i jako walczył z Amazyjaszem, królem Judzkim, azaż tego nie zapisano w kronikach o królach Izraelskich?
16 Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
I zasnął Joaz z ojcami swymi, a pogrzebiony jest w Samaryi z królmi Izraelskimi, a królował Jeroboam, syn jego, miasto niego.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
I żył Amazyjasz, syn Joazowy, król Judzki, po śmierci Joaza, syn Joachaza, króla Izraelskiego, piętnaście lat.
18 Matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A inne sprawy Amazyjaszowe, azaż nie są opisane w kronikach o królach Judzkich?
19 Wakafanya shauri baya dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuulia huko.
Potem sprzysięgli się przeciwko niemu niektórzy w Jeruzalemie; ale uciekł do Lachys. Przetoż posławszy za nim do Lachys, zabili go tam.
20 Akarudishwa kwa farasi na akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
Skąd przynieśli go na koniach, i pogrzebiony jest w Jeruzalemie z ojcami swymi, w mieście Dawidowem.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa baba yake Amazia.
A tak wziąwszy wszystek lud Judzki Azaryjasza, któremu było szesnaście lat, postanowili go królem na miejscu ojca jego Amazyjasza.
22 Ndiye aliijenga tena Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
Ten pobudował Elat, i przywrócił je do Judy, gdy zasnął król z ojcami swymi.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na mmoja.
Roku piętnastego Amazyjasza, syna Joaza, króla Judzkiego, królował Jeroboam, syn Joaza, króla Izraelskiego, w Samaryi czterdzieści lat i rok.
24 Akafanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
A czynił złe przed oczyma Pańskiemi, nie uchylając się od wszystkich grzechów Jeroboama, syn Nabatowego, który przywiódł do grzechu Izraela.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
Ten zasię przywrócił granice Izraelskie od wejścia do Emat aż do morza pustego, według słowa Pana, Boga Izraelskiego, które był wyrzekł przez sługę swego Jonasza, syna Amaty, proroka; który był z Gatefer.
26 Bwana alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwepo na yeyote wa kuwasaidia.
Albowiem widział Pan utrapienie Izraelskie, im dalej tem większe, tak, że i więzień, i opuszczony zniszczeni byli, a nie był, ktoby ratował Izraela.
27 Kwa kuwa Bwana alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
A nie rzekł był Pan, aby miał wygładzić imię Izraela, żeby nie zostało pod niebem: przetoż je wybawił przez rękę Jeroboama, syna Joazaowego.
28 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
A inne sprawy Jeroboamowe, i wszystko co czynił, i moc jego, którą walczył, i którą przywrócił Damaszek i Emat Judzkie Izraelowi, azaż tego nie zapisano w kronikach o królach Izraelskich?
29 Yeroboamu akalala pamoja na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
I zasnął Jeroboam z ojcami swymi, z królmi Izraelskimi, a królował Zacharyjasz, syn jego, miasto niego.