< 2 Nyakati 35 >
1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
Josias célébra à Jérusalem la Pâque en l’honneur de Yahweh, et on immola la Pâque le quatorzième jour du premier mois.
2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
Il établit les prêtres dans leurs fonctions, et il les encouragea à faire le service dans la maison de Yahweh.
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
Il dit aux lévites qui enseignaient tout Israël et qui étaient consacrés à Yahweh: « Placez l’arche sainte dans la maison qu’a bâtie Salomon, fils de David, roi d’Israël; vous n’avez plus à la porter sur l’épaule. Servez maintenant Yahweh, votre Dieu, et son peuple d’Israël.
4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
Tenez-vous prêts, selon vos familles, dans vos classes, selon le règlement de David, roi d’Israël, et selon le dispositif de Salomon, son fils.
5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
Tenez-vous dans le sanctuaire, selon les divisions des familles de vos frères, les fils du peuple, — pour chaque division une classe de la famille des lévites.
6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
Immolez la Pâque, sanctifiez-vous et préparez- la pour vos frères, pour qu’on se conforme à la parole de Yahweh, qu’il a dite par l’organe de Moïse. »
7 Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
Josias donna aux gens du peuple du petit bétail, agneaux et chevreaux, au nombre de trente mille, le tout en vue de la Pâque, pour tous ceux qui se trouvaient là, et trois mille bœufs, le tout pris sur les biens du roi.
8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
Ses chefs firent spontanément un présent au peuple, aux prêtres et aux lévites: Helcias, Zacharias et Jahiel, princes de la maison de Dieu, donnèrent aux prêtres pour la Pâque deux mille six cents agneaux et trois cents bœufs;
9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
Chonénias, Séméïas et Nathanaël, ses frères, Hasabias, Jéhiel et Jozabad, princes des lévites, donnèrent aux lévites pour la Pâque cinq mille agneaux et cinq cents bœufs.
10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
Ainsi le service fut organisé: les prêtres se tinrent à leurs postes, ainsi que les lévites, selon leurs divisions, conformément à l’ordre du roi.
11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
Les lévites immolèrent la Pâque, et les prêtres répandaient le sang qu’ils recevaient de leur main, tandis que les lévites dépouillaient les victimes.
12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
Ils mirent à part les morceaux destinés à l’holocauste, pour les donner aux divisions des familles des gens du peuple, afin qu’ils les offrissent à Yahweh, comme il est écrit dans le livre de Moïse; et de même pour les bœufs.
13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
Ils firent rôtir au feu la Pâque, selon le règlement, et ils firent cuire les saintes offrandes dans des pots, des chaudrons et des poêles, et ils s’empressèrent de les distribuer à tous les gens du peuple.
14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
Ensuite ils préparèrent la Pâque pour eux et pour les prêtres; car les prêtres, fils d’Aaron, furent occupés, jusqu’à la nuit, à offrir l’holocauste et les graisses: c’est pourquoi les lévites la préparèrent pour eux et pour les prêtres, fils d’Aaron.
15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
Les chantres, fils d’Asaph, étaient à leur place, selon l’ordre de David, d’Asaph, d’Héman et d’Idithun, le voyant du roi, et les portiers étaient à chaque porte; ils n’avaient pas à se détourner de leur office, car leurs frères, les lévites, préparaient pour eux la Pâque.
16 Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
Ainsi fut organisé tout le service de Yahweh, en ce jour-là, pour célébrer la Pâque et offrir des holocaustes sur l’autel de Yahweh, conformément à l’ordre du roi Josias.
17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
Les enfants d’Israël qui se trouvaient là célébrèrent la Pâque en ce temps, et la fête des Azymes pendant sept jours.
18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
Aucune Pâque pareille à celle-ci n’avait été célébrée en Israël depuis les jours de Samuel le prophète, et aucun des rois d’Israël n’avait fait une Pâque pareille à celle que célébrèrent Josias, les prêtres et les lévites, tout Juda et tout Israël qui se trouvaient là, et les habitants de Jérusalem.
19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
Ce fut la dix-huitième année du règne de Josias que cette Pâque fut célébrée.
20 Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
Après tout cela, lorsque Josias eut réparé la maison de Yahweh, Néchao, roi d’Égypte, monta pour combattre à Charcamis, sur l’Euphrate; et Josias sortit à sa rencontre.
21 Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
Et Néchao lui envoya des messagers pour dire: « Que me veux-tu, roi de Juda? Ce n’est pas contre toi que je viens aujourd’hui; mais c’est contre une maison avec laquelle je suis en guerre, et Dieu m’ a dit de me hâter. Cesse de t’opposer à Dieu, qui est avec moi, et qu’il ne te fasse pas mourir! »
22 Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
Mais Josias ne se détourna pas de lui et se déguisa pour l’attaquer; il n’écouta pas les paroles de Néchao, qui venaient de la bouche de Dieu; il s’avança pour combattre dans la plaine de Mageddo.
23 Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
Les archers tirèrent sur le roi Josias, et le roi dit à ses serviteurs: « Transportez-moi, car je suis gravement blessé. »
24 Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
Ses serviteurs le transportèrent du char, et le placèrent dans l’autre char qui était à lui, et l’emmenèrent à Jérusalem. Il mourut, et fut enterré dans les sépulcres de ses pères. Tout Juda et Jérusalem pleurèrent Josias.
25 Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
Jérémie composa une lamentation sur Josias; tous les chanteurs et toutes les chanteuses ont parlé de Josias dans leurs lamentations, jusqu’à ce jour; on en a fait une coutume en Israël. Et voici que ces chants sont écrits dans les Lamentations.
26 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
Le reste des actes de Josias, et ses œuvres pieuses conformes à ce qui est écrit dans la loi de Yahweh,
27 matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
ses actes, les premiers et les derniers, voici que cela est écrit dans le livre des rois d’Israël et de Juda.