< 2 Nyakati 20 >

1 Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
And it was after this they came [the] people of Moab and [the] people of Ammon and with them - some of the Ammonites on Jehoshaphat for battle.
2 Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
And people came and they told to Jehoshaphat saying [is] coming on you a multitude great from [the] other side of the sea from Aram and there they [are] in Hazezon Tamar it [is] En Gedi.
3 Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
And he was afraid and he gave Jehoshaphat face his to seek Yahweh and he proclaimed a fast over all Judah.
4 Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
And they gathered Judah to seek from Yahweh also from all [the] cities of Judah they came to seek Yahweh.
5 Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
And he stood Jehoshaphat in [the] assembly of Judah and Jerusalem in [the] house of Yahweh before the courtyard new.
6 akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
And he said O Yahweh [the] God of ancestors our ¿ not [are] you he God in the heavens and you [are] ruler over all [the] kingdoms of the nations and [are] in hand your power and strength and there not [is] with you to hold ground.
7 Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
¿ Not - you O God our did you dispossess [the] inhabitants of the land this from to before people your Israel and you gave it to [the] offspring of Abraham friend your for ever.
8 Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
And they have dwelt in it and they have built for you - in it a sanctuary for name your saying.
9 ‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
If it will come on us calamity sword judgment and pestilence and famine we will stand before the house this and before you for name your [is] in the house this so we may cry out to you from distress our so you may hear and you may save.
10 “Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
And therefore here! [the] people of Ammon and Moab and [the] mountain of Seir which not you permitted to Israel to go in them when came they from [the] land of Egypt for they turned aside from on them and not they destroyed them.
11 tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
And here! they [are] repaying to us by coming to drive out us from possession your which you caused to possess us.
12 Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
O God our ¿ not will you enter into judgment on them for there not in us [is] strength before the multitude great this which is coming on us and we not we know what? will we do for [are] on you eyes our.
13 Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
(And all *LAB(h)*) Judah [were] standing before Yahweh also little one[s] their wives their and children their.
14 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
And Jahaziel [the] son of Zechariah [the] son of Benaiah [the] son of Jeiel [the] son of Mattaniah the Levite one of [the] descendants of Asaph it was on him [the] spirit of Yahweh in [the] midst of the assembly.
15 Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
And he said pay attention O all Judah and [the] inhabitants of Jerusalem and the king Jehoshaphat thus he says Yahweh to you O you may not you be afraid and may not you be dismayed because of the multitude great this for not [belongs] to you the battle for to God.
16 Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
Tomorrow go down on them there they [will be] coming up on [the] ascent of Ziz and you will find them at [the] end of the wadi [the] face of [the] wilderness of Jeruel.
17 Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
Not [belongs] to you to fight in this [battle] take your stand stand and see [the] victory of Yahweh with you O Judah and Jerusalem may not you be afraid and may not you be dismayed tomorrow go out before them and Yahweh [will be] with you.
18 Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
And he bowed low Jehoshaphat face [the] ground towards and all Judah and [the] inhabitants of Jerusalem they fell down before Yahweh to bow down to Yahweh.
19 Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
And they stood the Levites of [the] descendants of the Kohathites and of [the] descendants of the Korahites to praise Yahweh [the] God of Israel with a voice great upwards.
20 Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
And they rose early in the morning and they went out to [the] wilderness of Tekoa and when went out they he stood Jehoshaphat and he said listen to me O Judah and [the] inhabitants of Jerusalem trust in Yahweh God your so you may be established trust in prophets his and succeed.
21 Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
And he consulted the people and he appointed [those who] sang to Yahweh and [those who] praised to adornment of holiness when went out before the [man] equipped and saying give thanks to Yahweh for [is] for ever covenant loyalty his.
22 Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
And at [the] time [when] they began with a shout of joy and praise he set Yahweh - ambushers on [the] people of Ammon Moab and [the] mountain of Seir who were coming to Judah and they were defeated.
23 Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
And they rose up [the] people of Ammon and Moab on [the] inhabitants of [the] mountain of Seir to totally destroy [them] and to destroy [them] and just as had finished they with [the] inhabitants of Seir they helped each on neighbor his to destruction.
24 Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
And Judah it came to the watchtower of the wilderness and they turned to the multitude and there they [were] corpses lying [the] ground towards and there not [was] an escaped remnant.
25 Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
And he went Jehoshaphat and people his to plunder booty their and they found among them to abundance and property and corpses and articles of precious things and they plundered for themselves to there not [was] carrying and they were days three plundering the booty for [was] much it.
26 Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
And on the day fourth they assembled to [the] valley of Berachah for there they blessed Yahweh there-fore people have called [the] name of the place that [the] valley of Berachah until this day.
27 Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
And they turned back every man of Judah and Jerusalem and Jehoshaphat at head their to return to Jerusalem with joy for he had made rejoice them Yahweh from enemies their.
28 Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
And they came Jerusalem with lyres and with harps and with trumpets to [the] house of Yahweh.
29 Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
And it was [the] dread of God on all [the] kingdoms of the lands when heard they that he had fought Yahweh with [the] enemies of Israel.
30 Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
And it was at peace [the] kingdom of Jehoshaphat and he had given rest to him God his from round about.
31 Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
And he reigned Jehoshaphat over Judah a son of thirty and five year[s] when became king he and twenty and five year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Azubah [the] daughter of Shilhi.
32 Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
And he walked in [the] way of father his Asa and not he turned aside from it to do the right in [the] eyes of Yahweh.
33 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
Only the high places not they were removed and still the people not they directed heart their to [the] God of ancestors their.
34 Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
And [the] rest of [the] matters of Jehoshaphat former and latter there they [are] written in [the] words of Jehu [the] son of Hanani which it was recorded on [the] scroll of [the] kings of Israel.
35 Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
And after this he made an alliance Jehoshaphat [the] king of Judah with Ahaziah [the] king of Israel he he acted wickedly to do.
36 Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
And he allied himself with him to make ships to go Tarshish and they made ships in Ezion Geber.
37 Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.
And he prophesied Eliezer [the] son of Dodavahu from Mareshah on Jehoshaphat saying as making alliance you with Ahaziah he will break Yahweh works your and they were broken ships and not they retained to go to Tarshish.

< 2 Nyakati 20 >