< 2 Nyakati 17 >

1 Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
And he became king Jehoshaphat son his in place of him and he strengthened himself on Israel.
2 Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
And he put an army in all [the] cities of Judah fortified and he put garrisons in [the] land of Judah and in [the] cities of Ephraim which he had captured Asa father his.
3 Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
And he was Yahweh with Jehoshaphat for he walked in [the] ways of David ancestor his former and not he sought the Baals.
4 bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
For [the] God of father his he sought and in commandments his he walked and not according to [the] deed[s] of Israel.
5 Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
And he established Yahweh the kingdom in hand his and they gave all Judah tribute to Jehoshaphat and it belonged to him wealth and honor to abundance.
6 Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
And it was high heart his in [the] ways of Yahweh and again he removed the high places and the Asherah poles from Judah.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
And in year three of reigning his he sent officials his Ben-Hail and Obadiah and Zechariah and Nethanel and Micaiah to teach in [the] cities of Judah.
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
And [were] with them the Levites Shemaiah and Nethaniah and Zebadiah and Asahel (and Shemiramoth *Q(K)*) and Jonathan and Adonijah and Tobijah and Tob-Adonijah the Levites and [were] with them Elishama and Jehoram the priests.
9 Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
And they taught in Judah and [was] with them [the] book of [the] law of Yahweh and they went round in all [the] cities of Judah and they taught among the people.
10 Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
And it was - [the] dread of Yahweh on all [the] kingdoms of the lands which [were] around Judah and not they waged war with Jehoshaphat.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
And some of [the] Philistines [were] bringing to Jehoshaphat tribute and silver a load also the Arabs [were] bringing to him flock[s] rams seven thousand and seven hundred and male goats seven thousand and seven hundred.
12 Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
And it was Jehoshaphat [was] going and [was] becoming great to upwards and he built in Judah fortresses and cities of storage.
13 na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
And property much it belonged to him in [the] cities of Judah and men of war mighty [men] of strength [were] in Jerusalem.
14 Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
And these [were] group[s] their to [the] house of ancestors their of Judah commanders of thousands Adnah [was] the commander and [were] with him mighty [men] of strength three hundred thousand.
15 aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
And on hand his Jehohanan the commander and with him two hundred and eighty thousand.
16 aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
And on hand his Amasiah [the] son of Zikri who volunteered to Yahweh and with him two hundred thousand mighty [man] of strength.
17 Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
And from Benjamin a mighty [man] of strength Eliada and with him [men] equipped of bow and shield two hundred thousand.
18 aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
And on hand his Jehozabad and with him one hundred and eighty thousand [men] equipped of war.
19 Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.
These [were] the [ones who] served the king besides [those] whom he put the king in [the] cities of fortification in all Judah.

< 2 Nyakati 17 >