< 2 Nyakati 15 >
1 Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
L'Esprit de Dieu descendit sur Azaria, fils d'Oded.
2 Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
Il alla à la rencontre d'Asa, et lui dit: « Écoute-moi, Asa, et tout Juda et Benjamin! Yahvé est avec vous tant que vous êtes avec lui; si vous le cherchez, vous le trouverez; mais si vous l'abandonnez, il vous abandonnera.
3 Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
Or, pendant longtemps, Israël a été sans le vrai Dieu, sans prêtre enseignant, et sans loi.
4 Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
Mais quand, dans leur détresse, ils se sont tournés vers Yahvé, le Dieu d'Israël, et l'ont cherché, ils l'ont trouvé.
5 Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
En ces temps-là, il n'y avait pas de paix pour celui qui sortait et pour celui qui entrait, mais de grandes détresses pour tous les habitants des pays.
6 Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
Ils furent mis en pièces, nation contre nation, et ville contre ville, car Dieu les troubla par toutes sortes d'épreuves.
7 Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
Mais vous, soyez forts! Ne laissez pas vos mains se relâcher, car votre travail sera récompensé. »
8 Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
Lorsque Asa entendit ces paroles et la prophétie d'Oded le prophète, il prit courage et fit disparaître les abominations de tout le pays de Juda et de Benjamin et des villes qu'il avait prises dans la montagne d'Éphraïm, et il renouvela l'autel de l'Éternel qui était devant le portique de l'Éternel.
9 Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
Il rassembla tout Juda et Benjamin, et ceux qui habitaient avec eux, d'Éphraïm, de Manassé et de Siméon, car ils étaient venus à lui en abondance d'Israël, quand ils virent que Yahvé son Dieu était avec lui.
10 Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
Ils s'assemblèrent donc à Jérusalem au troisième mois, la quinzième année du règne d'Asa.
11 Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
En ce jour-là, ils sacrifièrent à l'Éternel, sur le butin qu'ils avaient apporté, sept cents têtes de bétail et sept mille moutons.
12 Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
Ils conclurent l'alliance de chercher l'Éternel, le Dieu de leurs pères, de tout leur cœur et de toute leur âme;
13 Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
et que quiconque ne chercherait pas l'Éternel, le Dieu d'Israël, serait mis à mort, petit ou grand, homme ou femme.
14 Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
Ils jurèrent à l'Éternel d'une voix forte, en poussant des cris, avec des trompettes et des cornets.
15 Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
Tout Juda se réjouit de ce serment, car ils avaient juré de tout leur cœur, ils l'avaient cherché de tout leur désir, et ils l'avaient trouvé. Alors Yahvé leur donna du repos tout autour.
16 Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
Il enleva aussi à Maaca, mère du roi Asa, le titre de reine-mère, parce qu'elle avait fait une image abominable d'Astarté; Asa abattit son image, la réduisit en poussière, et la brûla au torrent de Cédron.
17 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
Mais les hauts lieux ne furent pas enlevés d'Israël; cependant le cœur d'Asa fut parfait pendant toute sa vie.
18 Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Il apporta à la maison de Dieu les choses que son père avait consacrées et qu'il avait lui-même consacrées, de l'argent, de l'or et des ustensiles.
19 Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.
Il n'y eut plus de guerre jusqu'à la trente-cinquième année du règne d'Asa.