< 1 Samweli 30 >

1 Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
And it was when came David and men his Ziklag on the day third and [the] Amalekite[s] they had made a raid against [the] Negev and against Ziklag and they had struck Ziklag and they had burned it with fire.
2 nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
And they had taken captive the women who [were] in it from small and unto great not they had killed anyone and they had driven them away and they had gone to way their.
3 Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
And he came David and men his to the city and there! [it was] burned with fire and wives their and sons their and daughters their they had been taken captive.
4 Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
And he lifted up David and the people which [was] with him voice their and they wept until that not [was] in them strength to weep.
5 Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
And [the] two [the] wives of David they had been taken captive Ahinoam the Jezreelite [woman] and Abigail [the] wife of Nabal the Carmelite.
6 Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
And it was distress to David exceedingly for they said the people to stone him for it was bitter [the] soul of all the people everyone on (sons his *Q(K)*) and on daughters his and he strengthened himself David in Yahweh God his.
7 Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
And he said David to Abiathar the priest [the] son of Ahimelech bring near! please to me the ephod and he brought near Abiathar the ephod to David.
8 naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
And he enquired David by Yahweh saying will I pursue? after the marauding band this ¿ will I overtake it and he said to him pursue for certainly you will overtake [it] and certainly you will rescue [them].
9 Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
And he went David he and six hundred man who [were] with him and they came to [the] wadi of Besor and those [who] were left behind they remained.
10 kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
And he pursued David he and four hundred man and they remained two hundred man who they were [too] exhausted for passing over [the] wadi of Besor.
11 Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
And they found a man Egyptian in the open country and they took him to David and they gave to him bread and he ate and they gave to drink him water.
12 kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
And they gave to him a slice of fig cake and two bunches of raisins and he ate and it returned spirit his to him for not he had eaten food and not he had drunk water three days and three nights.
13 Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
And he said to him David [belong] to whom? you and where? from this [are] you and he said [am] a young man Egyptian I a slave of a man Amalekite and he abandoned me master my if I was sick the day three.
14 Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
We we had made a raid [the] Negev of the Kerethite[s] and on [that] which [belongs] to Judah and on [the] Negev of Caleb and Ziklag we had burned with fire.
15 Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
And he said to him David ¿ will you take down me to the marauding band this and he said swear! to me by God if you will kill me and if you will deliver up me in [the] hand of master my and I will take down you to the marauding band this.
16 Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
And he took down him and there! [they were] spread out over [the] face of all the land eating and drinking and celebrating in all the plunder great which they had taken from [the] land of [the] Philistines and from [the] land of Judah.
17 Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
And he struck down them David from the twilight and until the evening of next day their and not he escaped of them anyone that except four hundred man young man who they rode on the camels and they fled.
18 Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
And he rescued David all that they had taken Amalek and [the] two wives his he rescued David.
19 Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
And not it was missing to them from the small and unto the great and unto sons and daughters and from [the] booty and unto all that they had taken for themselves everything he brought back David.
20 Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
And he took David all the sheep and the cattle they drove [them] before the livestock that and they said this [is] [the] booty of David.
21 Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
And he came David to two hundred the men who they had been [too] exhausted - for going - after David and they had left behind them at [the] wadi of Besor and they went out to meet David and to meet the people which [was] with him and he approached David the people and he asked of them to welfare.
22 Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
And he answered every man evil and worthlessness from the men who they had gone with David and they said because that not they went with me not we will give to them any of the booty which we have recovered that except everyone wife his and children his so they may lead [them] away and they may go.
23 Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
And he said David not you must do thus O brothers my [that] which he has given Yahweh to us and he has kept us and he has given the marauding band which came on us in hand our.
24 Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
And who? will he listen to you to the matter this for like [the] share of - the [one who] went down in the battle and like [the] share of the [one who] remained with the baggage alike they will share.
25 Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
And it was from the day that and on-wards and he made it into a statute and into a judgment for Israel until the day this.
26 Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
And he came David to Ziklag and he sent some of the booty to [the] elders of Judah to friend his saying here! [is] for you a blessing from [the] booty of [the] enemies of Yahweh.
27 Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
For [those] who [were] in Beth-el and for [those] who [were] in Ramoth Negev and for [those] who [were] in Jattir.
28 kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
And for [those] who [were] in Aroer and for [those] who [were] in Siphmoth and for [those] who [were] in Eshtemoa.
29 na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
And for [those] who [were] in Racal and for [those] who [were] in [the] cities of the Jerahmeelite[s] and for [those] who [were] in [the] cities of the Kenite[s].
30 na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
And for [those] who [were] in Hormah and for [those] who [were] in Bor Ashan and for [those] who ([were] in Athach. *LA(bh)*)
31 na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.
And for [those] who [were] in Hebron and for all the places where he had gone about there David he and men his.

< 1 Samweli 30 >