< 1 Samweli 18 >

1 Baada ya Daudi kumaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ikaambatana na roho ya Daudi, naye akampenda kama nafsi yake mwenyewe.
And it was when finished he to speak to Saul and [the] self of Jonathan it was bound with [the] self of David (and he loved him *Q(k)*) Jonathan like own self his.
2 Kuanzia siku ile Sauli akamchukua Daudi naye hakumruhusu kurudi nyumbani kwa baba yake.
And he took him Saul on the day that and not he permitted him to return [the] house of father his.
3 Yonathani akafanya agano na Daudi kwa sababu alimpenda kama nafsi yake mwenyewe.
And he made Jonathan and David a covenant in love his him like own self his.
4 Yonathani akavua joho alilokuwa amevaa na kumpa Daudi, pamoja na koti lake, silaha zake, hata pamoja na upanga wake, upinde wake na mshipi wake.
And he stripped himself Jonathan the robe which [was] on him and he gave it to David and garments his and to sword his and to bow his and to belt his.
5 Lolote Sauli alilomtuma Daudi kufanya, alitenda kwa hekima, hata Sauli akampa cheo cha juu katika jeshi. Jambo hili likawapendeza watu wote, hata maafisa wa Sauli pia.
And he went out David in every where he sent him Saul he prospered and he appointed him Saul over [the] men of war and it was good in [the] eyes of all the people and also in [the] eyes of [the] servants of Saul.
6 Watu walipokuwa wanarudi nyumbani baada ya Daudi kumuua yule Mfilisti, wanawake wakaja kutoka pande zote za miji ya Israeli kumlaki Mfalme Sauli kwa kuimba na kucheza, kwa nyimbo za furaha na kwa matari na zeze.
And it was when came they when returned David from striking down the Philistine and they came out the women from all [the] cities of Israel (to sing *Q(k)*) and the dancing to meet Saul the king with tambourines with joy and with three-stringed instruments.
7 Walipokuwa wanacheza, wakaimba: “Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake.”
And they sang the women who were playing and they said he has struck down Saul (thousands his *Q(K)*) and David ten thousands his.
8 Sauli akakasirika sana; sehemu hii ya kurudia rudia ya wimbo huu ilimkasirisha sana. Akafikiri kuwa, “Wamempa Daudi makumi elfu, lakini mimi wamenipa elfu tu. Apate nini zaidi isipokuwa ufalme?”
And it burned to Saul exceedingly and it was displeasing in view his the matter this and he said they have ascribed to David ten thousands and to me they have ascribed the thousands and yet for him only the kingship.
9 Kuanzia wakati ule na kuendelea Sauli akawa na jicho la wivu juu ya Daudi.
And he was Saul (looking at *Q(K)*) David from the day that and onwards.
10 Kesho yake roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Mungu ikaja kwa nguvu juu ya Sauli. Alikuwa akitabiri nyumbani mwake, wakati Daudi alikuwa akipiga kinubi, kama alivyozoea. Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake;
And it was from [the] next day and it rushed a spirit of God - evil - to Saul and he prophesied in [the] midst of the house and David [was] playing an instrument with hand his as a day - in a day and the spear [was] in [the] hand of Saul.
11 akautupa kwa nguvu, akijiambia mwenyewe, “Nitamchoma kwa mkuki abaki hapo ukutani.” Lakini Daudi akamkwepa mara mbili.
And he threw Saul the spear and he said I will strike David and the wall and he went around David from before him two times.
12 Sauli akamwogopa Daudi, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Daudi, lakini alikuwa amemwacha yeye.
And he was afraid Saul from to before David for he was Yahweh with him and from with Saul he had turned aside.
13 Kwa hiyo Sauli akamwondoa Daudi mbele yake na kumpa kuwa kiongozi wa watu elfu moja, naye Daudi akatoka na kuingia akiongoza vikosi katika vita.
And he removed him Saul from with him and he appointed him for himself a commander of a thousand and he went out and he came before the people.
14 Katika kila kitu alichofanya, Daudi alipata mafanikio makubwa, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja naye.
And he was David to all (ways his *Q(K)*) successful and Yahweh [was] with him.
15 Sauli alipoona jinsi alivyokuwa akifanikiwa, akamwogopa.
And he saw Saul that he [was] successful exceedingly and he was afraid of him.
16 Lakini Israeli wote na Yuda walimpenda Daudi, kwa sababu ndiye alikuwa akiwaongoza katika vita vyao.
And all Israel and Judah [were] loving David for he [was] going out and [was] coming before them.
17 Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupa umwoe, endapo tu utanitumikia kwa ushujaa na kupigana vita vya Bwana.” Kwa maana Sauli alisema moyoni mwake, “Sitainua mkono wangu dhidi yake. Acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
And he said Saul to David here! daughter my elder Merab her I will give to you to a wife only become of me a son of strength and fight [the] battles of Yahweh and Saul he said may not it be hand my on him and let it be on him [the] hand of [the] Philistines.
18 Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, nayo jamaa yangu ni nini au ukoo wa baba yangu katika Israeli, kwamba mimi niwe mkwewe mfalme?”
And he said David to Saul who? [am] I and who? [are] kinsfolk my [the] clan of father my in Israel that I will be a son-in-law of the king.
19 Basi ulipofika wakati wa Daudi kupewa Merabu, binti Sauli, huyo binti aliozwa kwa Adrieli, Mmeholathi.
And it was at [the] time gave Merab [the] daughter of Saul to David and she she was given to Adriel the Meholathite to a wife.
20 Basi Mikali binti Sauli alimpenda Daudi, nao walipomwambia Sauli juu ya jambo hili, likampendeza.
And she loved Michal [the] daughter of Saul David and people told to Saul and it was pleasing the matter in view his.
21 Sauli akawaza, “Nitampa Daudi binti yangu, ili apate kuwa mtego kwake, ili kwamba mkono wa Wafilisti upate kuwa juu yake.” Hivyo Sauli akamwambia Daudi, “Sasa unayo nafasi ya pili ya kuwa mkwe wangu.”
And he said Saul I will give her to him so she may become for him a snare so it may be on him [the] hand of [the] Philistines and he said Saul to David in two [times] you will be a son-in-law to me this day.
22 Ndipo Sauli akawaagiza watumishi wake, akisema, “Zungumzeni na Daudi kwa siri na kumwambia, ‘Tazama, mfalme amependezwa nawe, nao watumishi wake wote wanakupenda. Basi na uwe mkwewe mfalme.’”
And he commanded Saul (servants his *Q(K)*) speak to David in secrecy saying here! he delights in you the king and all servants his they love you and therefore be son-in-law to the king.
23 Watumishi wa Sauli wakarudia hayo maneno kwa Daudi. Lakini Daudi akasema, “Je, mnafikiri ni jambo dogo kuwa mkwewe mfalme? Mimi ni mtu maskini tu, na nisiyejulikana sana.”
And they spoke [the] servants of Saul in [the] ears of David the words these and he said David ¿ trifling in view your [is] to be son-in-law to the king and I [am] a man poor and lightly esteemed.
24 Watumishi wa Sauli walipomweleza yale Daudi aliyoyasema,
And they told [the] servants of Saul to him saying according to the words these he spoke David.
25 Sauli akajibu, “Mwambieni Daudi, ‘Mfalme hataki zawadi nyingine kuwa mahari isipokuwa magovi 100 ya Wafilisti, ili kulipiza kisasi juu ya adui zake.’” Mawazo ya Sauli yalikuwa Daudi akaanguke mikononi mwa Wafilisti.
And he said Saul thus you will say to David not delight [belongs] to the king in bride-price for for a hundred foreskins of Philistines to avenge himself on [the] enemies of the king and Saul he planned to make fall David by [the] hand of [the] Philistines.
26 Watumishi walipomwambia Daudi mambo haya, ikampendeza kuwa mkwewe mfalme. Basi kabla siku iliyopangwa haijafika,
And they told servants his to David the words these and it was pleasing the matter in [the] eyes of David to be son-in-law to the king and not they were completed the days.
27 Daudi na watu wake walitoka na kuwaua Wafilisti mia mbili. Akayaleta magovi yao na kupeleka hesabu kamilifu kwa mfalme, ili kwamba apate kuwa mkwewe mfalme. Ndipo Sauli akamwoza Daudi Mikali binti yake.
And he arose David and he went - he and men his and he struck down among the Philistines two hundred man and he brought David foreskins their and people gave in full them to the king to be son-in-law to the king and he gave to him Saul Michal daughter his to a wife.
28 Sauli alipotambua kuwa Bwana alikuwa pamoja na Daudi na kwamba Mikali binti yake anampenda Daudi,
And he saw Saul and he knew that Yahweh [was] with David and Michal [the] daughter of Saul she loved him.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi, naye Sauli akabaki kuwa adui yake siku zote za maisha yake.
And he increased Saul to be afraid of David again and he was Saul an enemy David all the days.
30 Majemadari wa jeshi la Wafilisti waliendelea kupigana vita na kadiri walivyoendelea kupigana, Daudi akazidi kutenda kwa hekima kuliko maafisa wengine wa Sauli, nalo jina lake likajulikana sana.
And they went out [the] commanders of [the] Philistines and it was - as often as went out they he was successful David more than all [the] servants of Saul and it was esteemed name his exceedingly.

< 1 Samweli 18 >