< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
And he went up Nahash the Ammonite and he encamped on Jabesh Gilead and they said all [the] men of Jabesh to Nahash make to us a covenant and we will serve you.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
And he said to them Nahash the Ammonite by this I will make to you by gouging out of you every eye of [the] right [side] and I will make it a reproach on all Israel.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
And they said to him [the] elders of Jabesh refrain to us seven days so let us send messengers in all [the] territory of Israel and if there not [is one who] delivers us and we will come out to you.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
And they came the messengers Gibeah of Saul and they spoke the words in [the] ears of the people and they lifted up all the people voice their and they wept.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
And there! Saul [was] coming after the cattle from the field and he said Saul what? [is] to the people that they are weeping and they recounted to him [the] words of [the] men of Jabesh.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
And it rushed [the] spirit of God on Saul (just as heard he *Q(K)*) the words these and it burned anger his exceedingly.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
And he took a pair of ox[en] and he cut in pieces it and he sent [them] in all [the] territory of Israel by [the] hand of the messengers - saying [the one] who not he [is] coming out after Saul and after Samuel thus it will be done to ox[en] his and it fell [the] dread of Yahweh on the people and they came out like a man one.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
And he mustered them at Bezek and they were [the] people of Israel three hundred thousand and [the] man of Judah [was] thirty thousand.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
And they said to the messengers who had come thus you will say! to [the] man of Jabesh Gilead tomorrow it will belong to you deliverance (like [the] heat of *Q(K)*) the sun and they went the messengers and they told to [the] men of Jabesh and they were glad.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
And they said [the] men of Jabesh tomorrow will we go out to you and you will do to us according to all the good in view your.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
And it was from [the] next day and he made Saul the people three companies and they went in [the] midst of the camp in [the] watch of the morning and they struck down Ammon until [the] heat of the day and it was those [who] remained and they were scattered and not they remained among them two together.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
And it said the people to Samuel who? [is] the [one who] said Saul will he reign? over us deliver up the men so we may put to death them.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
And he said Saul not he will be put to death anyone on the day this for this day he has done Yahweh deliverance in Israel.
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
And he said Samuel to the people come so let us go Gilgal so we may renew there the kingship.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
And they went all the people Gilgal and they made king there Saul before Yahweh in Gilgal and they sacrificed there sacrifices peace offerings before Yahweh and he rejoiced there Saul and all [the] men of Israel up to muchness.

< 1 Samweli 11 >