< 1 Wafalme 8 >

1 Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Then he called together Solomon [the] elders of Israel all [the] chiefs of the tribes [the] leaders of the fathers of [the] people of Israel to the king Solomon Jerusalem to bring up [the] ark of [the] covenant of Yahweh from [the] city of David that [is] Zion.
2 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.
And they assembled to the king Solomon every person of Israel in [the] month of Ethanim at the festival that [was] the month seventh.
3 Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano,
And they came all [the] elders of Israel and they lifted the priests the ark.
4 nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba,
And they brought up [the] ark of Yahweh and [the] tent of meeting and all [the] utensils of holiness which [were] in the tent and they brought up them the priests and the Levites.
5 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
And the king Solomon and all [the] congregation of Israel who were gathered to him with him before the ark [were] sacrificing sheep and cattle which not they were counted and not they were numbered from multitude.
6 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
And they brought the priests [the] ark of [the] covenant of Yahweh to place its to [the] innermost room of the house to [the] holy place of the holy places to under [the] wings of the cherubim.
7 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea.
For the cherubim [were] spreading out wings to [the] place of the ark and they covered the cherubim over the ark and over poles its from to above.
8 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
And they were long the poles and they were visible [the] heads of the poles from the holy place on [the] face of the innermost room and not they were visible the outside towards and they have been there until the day this.
9 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
There not [was] in the ark only [the] two [the] tablets of stone which he placed there Moses at Horeb where he made Yahweh with [the] people of Israel when came out they from [the] land of Egypt.
10 Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana.
And it was when came out the priests from the holy place and the cloud it filled [the] house of Yahweh.
11 Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.
And not they were able the priests to stand to serve because of the cloud for it filled [the] glory of Yahweh [the] house of Yahweh.
12 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;
Then he said Solomon Yahweh he has said to dwell in thick darkness.
13 naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”
Certainly I have built a house of loftiness for you a place to dwell in you forever.
14 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
And he turned the king face his and he blessed all [the] assembly of Israel and all [the] assembly of Israel [was] standing.
15 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
And he said [be] blessed Yahweh [the] God of Israel who he spoke with mouth his with David father my and with hand his he has fulfilled saying.
16 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
Since the day when I brought out people my Israel from Egypt not I chose a city from all [the] tribes of Israel to build a house to be name my there and I have chosen David to be over people my Israel.
17 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
And it was with [the] heart of David father my to build a house for [the] name of Yahweh [the] God of Israel.
18 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
And he said Yahweh to David father my because that it was with heart your to build a house for name my you did well that it was with heart your.
19 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Only you not you will build the house that except son your who comes out from loins your he he will build the house for name my.
20 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
And he has established Yahweh word his which he spoke and I have arisen in place of David father my and I have sat on [the] throne of Israel just as he spoke Yahweh and I have built the house for [the] name of Yahweh [the] God of Israel.
21 Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”
And I have set up there a place for the ark where [is] there [the] covenant of Yahweh which he made with ancestors our when brought out he them from [the] land of Egypt.
22 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni
And he stood Solomon before [the] altar of Yahweh before all [the] assembly of Israel and he spread out palms his the heavens.
23 na kusema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
And he said O Yahweh [the] God of Israel there not like you [is] a God in the heavens above and on the earth beneath [who] keeps the covenant and covenant loyalty to servants your who walk before you with all heart their.
24 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
Who you have kept to servant your David father my [that] which you spoke to him and you spoke with mouth your and with hand your you have fulfilled as the day this.
25 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
And therefore O Yahweh - [the] God of Israel keep to servant your David father my [that] which you spoke to him saying not it will be cut off to you a man from to before me [who] sits on [the] throne of Israel only if they will guard descendants your way their to walk before me just as you have walked before me.
26 Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
And therefore O God of Israel let it be established please (word your *Q(K)*) which you spoke to servant your David father my.
27 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
For ¿ really will he dwell God on the earth here! the heavens and [the] heavens of the heavens not they contain you indeed? for the house this which I have built.
28 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
And you will turn to [the] prayer of servant your and to supplication his O Yahweh God my to listen to the cry of entreaty and to the prayer which servant your [is] praying before you this day.
29 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
To be eyes your open to the house this night and day to the place where you have said it will be name my there to listen to the prayer which he will pray servant your to the place this.
30 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
And you will listen to [the] supplication of servant your and people your Israel which they will pray to the place this and you you will listen to [the] place dwelling you to the heavens and you will hear and you will forgive.
31 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
[that] which He will sin anyone to neighbor his and he will impose on him an oath to put under an oath him and he will come he will swear an oath before altar your in the house this.
32 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
And you - you will hear the heavens and you will act and you will judge servants your to condemn as guilty a guilty [person] to requite conduct his on own head his and to declare righteous a righteous [person] to give to him according to righteousness his.
33 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
When are defeated people your Israel before an enemy that they will sin to you and they will turn back to you and they will praise name your and they will pray and they will seek favor to you in the house this.
34 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
And you you will hear the heavens and you will forgive [the] sin of people your Israel and you will bring back them to the land which you gave to ancestors their.
35 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
When are shut up [the] heavens and not it will be rain for they will sin to you and they will pray to the place this and they will praise name your and from sin their they will turn back! for you will afflict them.
36 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
And you - you will hear the heavens and you will forgive [the] sin of servants your and people your Israel that you will teach them the way good which they will walk in it and you will give rain on land your which you gave to people your to an inheritance.
37 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
Famine if it will be in the land pestilence for it will be blight mildew locust[s] locust[s] for it will be that he will lay siege to it enemy its in [the] land of gates its every plague any sickness.
38 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili:
Every prayer every supplication which it will belong to any person to all people your Israel who they will know! each [the] plague of own heart his and he will spread out palms his to the house this.
39 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
And you you will hear the heavens [the] place of dwelling your and you will forgive and you will act and you will give to the person according to all ways his whom you will know heart his for you you know to alone you [the] heart of all [the] children of humankind.
40 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
So that they may fear you all the days which they [will be] alive on [the] surface of the ground which you gave to ancestors our.
41 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako,
And also to the foreigner who not [is] one of people your Israel he and he will come from a land distant for [the] sake of name your.
42 kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili,
For they will hear! name your great and hand your mighty and arm your outstretched and he will come and he will pray to the house this.
43 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
You you will hear the heavens [the] place dwelling you and you will do according to all that he will call to you the foreigner so that they may know! all [the] peoples of the earth name your to fear you like people your Israel and to know that name your it has been called on the house this which I have built.
44 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
If it will go forth people your for battle on enemy its by the way which you will send them and they will pray to Yahweh [the] direction of the city which you have chosen it and the house which I have built for name your.
45 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
And you will hear the heavens prayer their and supplication their and you will do justice their.
46 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu;
If they will sin to you for there not [is] anyone who not he sins and you will be angry with them and will you deliver up them before an enemy and they will take captive them captors their to [the] land of the enemy distant or near.
47 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’;
And they will bring back to heart their in the land where they have been taken captive there and they will repent - and they will seek favor to you in [the] land of captors their saying we have sinned and we have done wrong we have acted wickedly.
48 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako;
And they will return to you with all heart their and with all being their in [the] land of enemies their who they have taken captive them and they will pray to you [the] direction of land their which you gave to ancestors their the city which you have chosen and the house which (I have built *Q(K)*) for name your.
49 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao.
And you will hear the heavens [the] place dwelling you prayer their and supplication their and you will do justice their.
50 Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma;
And you will forgive people your who they have sinned to you and all transgressions their which they transgressed against you and you will make them into [objects of] compassion before captors their and they will have compassion on them.
51 kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.
For [are] people your and inheritance your they whom you brought out from Egypt from [the] midst of [the] furnace of iron.
52 “Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia.
To be eyes your open to [the] supplication of servant your and to [the] supplication of people your Israel to listen to them in all calling they to you.
53 Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”
For you you have separated them for yourself to an inheritance from all [the] peoples of the earth just as you spoke by [the] hand of - Moses servant your when bringing out you ancestors our from Egypt O Lord Yahweh.
54 Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni.
And it was - when had finished Solomon to pray to Yahweh all the prayer and the supplication this he stood up from to before [the] altar of Yahweh from bowing down on knees his and palms his [were] spread out the heavens.
55 Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:
And he stood and he blessed all [the] assembly of Israel a voice great saying.
56 “Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose.
[be] blessed Yahweh who he has given a resting place to people his Israel according to all that he has spoken not it has fallen a word one from every word his good which he spoke by [the] hand of Moses servant his.
57 Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa.
May he be Yahweh God our with us just as he was with ancestors our may not he forsake us and may not he abandon us.
58 Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu.
To incline heart our to him to walk in all ways his and to keep commandments his and statutes his and judgments his which he commanded ancestors our.
59 Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku,
And may they be words my these which I have sought favor before Yahweh near to Yahweh God our by day and night to do - [the] justice of servant his and [the] justice of people his Israel a matter of a day in day its.
60 ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine.
So as to know all [the] peoples of the earth that Yahweh he [is] God there not [is] still more.
61 Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”
And it will be heart your complete with Yahweh God our to walk in statutes his and to keep commandments his as the day this.
62 Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana.
And the king and all Israel with him [were] sacrificing a sacrifice before Yahweh.
63 Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.
And he sacrificed Solomon [the] sacrifice of the peace offerings which he sacrificed to Yahweh cattle twenty and two thousand and sheep one hundred and twenty thousand and they dedicated [the] house of Yahweh the king and all [the] people of Israel.
64 Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.
On the day that he consecrated the king [the] middle of the court which [was] before [the] house of Yahweh for he offered there the burnt offering and the grain offering and [the] fat of the peace offerings for [the] altar of bronze which [was] before Yahweh [was too] small for containing the burnt offering and the grain offering and [the] fat of the peace offerings.
65 Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne.
And he observed Solomon at the time that - the festival and all Israel with him an assembly great from Lebo Hamath - to [the] wadi of Egypt before Yahweh God our seven days and seven days four-teen day[s].
66 Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.
On the day eighth he sent away the people and they blessed the king and they went to tents their joyful and good of heart on all the good which he had done Yahweh to David servant his and to Israel people his.

< 1 Wafalme 8 >