< 1 Wafalme 19 >

1 Ahabu akamwambia Yezebeli kila kitu Eliya alichokuwa amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
Ahab ispriča Izebeli sve što je Ilija učinio i kako je mačem poubijao sve proroke.
2 Hivyo Yezebeli akamtuma mjumbe kwa Eliya, kusema, “Hao miungu initendee hivyo na kuzidi, kama kufikia kesho wakati kama huu sitaifanya roho yako kama mmojawapo wa hao manabii.”
Tada Izebela posla Iliji glasnika s porukom: “Neka mi bogovi učine sva zla i neka nadodadu, ako sutra u ovo doba ne učinim s tvojim životom kao što si ti učinio sa životom svakoga od njih!”
3 Eliya aliogopa, na akakimbia kuokoa maisha yake. Alipofika Beer-Sheba katika Yuda, akamwacha mtumishi wake huko,
On se uplaši, ustade i ode da bi spasio život. Došao je u Beer Šebu, koja je u Judeji, i otpustio ondje svoga momka.
4 lakini yeye mwenyewe akatembea mwendo wa kutwa nzima katika jangwa. Akafika kwenye mti wa mretemu, akakaa chini yake na kuomba ili afe. Akasema, “Yatosha sasa, Bwana, ondoa roho yangu, kwani mimi si bora kuliko baba zangu.”
A sam ode dan hoda u pustinju; sjede ondje pod smreku, zaželje umrijeti i reče: “Već mi je svega dosta, Jahve! Uzmi dušu moju, jer nisam bolji od otaca svojih.”
5 Kisha akajinyoosha chini ya mti, akalala usingizi. Mara malaika akamgusa na akamwambia, “Inuka na ule.”
Zatim leže i zaspa. Ali gle, anđeo ga taknu i reče mu: “Ustani i jedi.”
6 Akatazama pande zote, napo hapo karibu na kichwa chake palikuwepo mkate uliookwa kwenye makaa ya moto na gudulia la maji. Akala na kunywa, kisha akajinyoosha tena.
On pogleda, kad gle - kraj njegova uzglavlja na kamenu pečen kruh i vrč vode. Jeo je i pio, pa opet legao.
7 Yule malaika wa Bwana akaja tena mara ya pili, akamgusa akamwambia, “Inuka na ule, kwa kuwa safari ni ndefu kwako.”
Ali se anđeo Jahvin javi i drugi put, dotače ga i reče: “Ustani i jedi, jer je pred tobom dalek put!”
8 Kwa hiyo akainuka, akala na kunywa. Akiwa ametiwa nguvu na kile chakula, akasafiri siku arobaini usiku na mchana mpaka akafika Horebu, mlima wa Mungu.
Ustao je, jeo i pio. Okrijepljen tom hranom, išao je četrdeset dana i četrdeset noći sve do Božje gore Horeba.
9 Huko akaingia katika pango, akalala humo usiku ule. Nalo neno la Bwana likamjia, kusema, “Unafanya nini hapa, Eliya?”
Ondje je ušao u neku spilju i prenoćio u njoj. I gle, eto k njemu riječi Jahvine: “Što ćeš ti ovdje, Ilija?”
10 Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
On odgovori: “Revnovao sam gorljivo za Jahvu, Boga nad vojskama, jer su sinovi Izraelovi napustili tvoj Savez, srušili tvoje žrtvenike i pobili mačem tvoje proroke. Ostao sam sam, a oni traže da i meni uzmu život.”
11 Bwana akasema, “Toka nje ukasimame juu ya mlima mbele za Bwana, kwa kuwa Bwana yu karibu kupita hapo.” Kisha upepo mwingi na wenye nguvu ukapasua milima ile na kuvunjavunja miamba mbele za Bwana, lakini Bwana hakuwamo katika ule upepo. Baada ya upepo palikuwa na tetemeko la nchi, lakini Bwana hakuwamo kwenye lile tetemeko.
Glas mu reče: “Iziđi i stani u gori pred Jahvom. Evo Jahve upravo prolazi.” Pred Jahvom je bio silan vihor, tako snažan da je drobio brda i lomio hridi, ali Jahve nije bio u olujnom vihoru; poslije olujnog vihora bio je potres, ali Jahve nije bio u potresu;
12 Baada ya tetemeko la nchi ukaja moto, lakini Bwana hakuwamo katika ule moto. Baada ya moto ikaja sauti ya utulivu ya kunongʼona.
a poslije potresa bio je oganj, ali Jahve nije bio u ognju; poslije ognja šapat laganog i blagog lahora.
13 Eliya alipoisikia, akafunika uso kwa vazi lake, akatoka na kusimama kwenye mdomo wa pango. Kisha ile sauti ikamwambia, “Eliya, unafanya nini hapa?”
Kad je to čuo Ilija, zakri lice plaštem, iziđe i stade na ulazu u pećinu. Tada mu progovori glas i reče: “Što ćeš ovdje, Ilija?”
14 Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
On odgovori: “Revnovao sam veoma gorljivo za Jahvu nad vojskama, jer su sinovi Izraelovi napustili tvoj Savez, srušili tvoje žrtvenike i mačem poubijali tvoje proroke. Ostadoh sam, a oni traže da i meni oduzmu život.”
15 Bwana akamwambia, “Rudi kwa njia uliyoijia, uende kwenye Jangwa la Dameski. Wakati utakapofika huko, mtie Hazaeli mafuta awe mfalme wa Aramu
Jahve mu reče: “Idi, vrati se istim putem u damaščansku pustinju. Kad dođeš, pomaži ondje Hazaela za kralja aramskog.
16 Pia mtie mafuta Yehu mwana wa Nimshi awe mfalme wa Israeli, na umtie Elisha mwana wa Shafati kutoka Abel-Mehola mafuta awe nabii badala yako.
Pomaži Jehuu, sina Nimsijeva, za kralja izraelskoga i pomaži Elizeja, sina Šafatova, iz Abel Mehole, za proroka namjesto sebe.
17 Yehu atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Hazaeli, naye Elisha atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Yehu.
Koji utekne od mača Hazaelova, njega će pogubiti Jehu; a tko utekne od Jehuova mača, njega će pogubiti Elizej.
18 Hata sasa nimeweka akiba watu elfu saba katika Israeli, wote ambao hawajampigia Baali magoti, na wote ambao midomo yao haijambusu.”
Ali ću ostaviti u Izraelu sedam tisuća, sve koljena koja se nisu savila pred Baalom i sva usta koja ga nisu cjelivala.”
19 Hivyo Eliya akaondoka kutoka huko na kumkuta Elisha mwana wa Shafati. Alikuwa akilima kwa jozi kumi na mbili za maksai, na yeye mwenyewe aliongoza ile jozi ya kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akamrushia vazi lake.
Ode on i na povratku naiđe na Elizeja, sina Šafatova, gdje ore: pred njim dvanaest jarmova, sam bijaše kod dvanaestoga. Ilija prođe kraj njega i baci na nj svoj plašt.
20 Kisha Elisha akawaacha maksai wake, akamkimbilia Eliya, akamwambia, “Niruhusu nikawabusu baba yangu na mama yangu, halafu nitafuatana nawe.” Eliya akajibu, “Rudi zako, kwani nimekutendea nini?”
On ostavi volove, potrča za Ilijom i reče: “Dopusti mi da zagrlim svoga oca i majku, pa ću poći za tobom.” Ilija mu odgovori: “Idi, vrati se, jer što sam ti učinio?”
21 Basi Elisha akamwacha Eliya, naye akarudi. Akachukua ile jozi yake ya maksai na kuwachinja. Akaipika ile nyama kwa kutumia miti ya nira kama kuni na kuwapa watu, nao wakala. Kisha akaondoka, akamfuata Eliya, akamtumikia.
On ga ostavi, uze jaram volova i žrtvova ih. Volujskim jarmom skuha meso i dade ga ljudima da jedu. Zatim ustade i pođe za Ilijom da ga poslužuje.

< 1 Wafalme 19 >