< 1 Wafalme 17 >

1 Basi Eliya, Mtishbi kutoka Tishbi katika Gileadi, akamwambia Ahabu, “Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninamtumikia, hapatakuwa na umande wala mvua katika miaka hii, isipokuwa kwa neno langu.”
And he said Elijah the Tishbite one of [the] resident aliens of Gilead to Ahab [by] [the] life of Yahweh [the] God of Israel whom I stand before him if it will be the years these dew and rain that except to [the] mouth of word my.
2 Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to him saying.
3 “Ondoka hapa, elekea upande wa mashariki ukajifiche katika Kijito cha Kerithi, mashariki mwa Yordani.
Go from here and you will turn yourself east-ward and you will hide yourself at [the] wadi of Kerith which [is] on [the] face of the Jordan.
4 Utakunywa maji kutoka kile kijito, nami nimeagiza kunguru wakulishe huko.”
And it will be from the wadi you will drink and the ravens I have commanded to supply you there.
5 Hivyo akafanya kile alichoambiwa na Bwana. Akaenda katika Kijito cha Kerithi, mashariki ya Yordani na akakaa huko.
And he went and he did according to [the] word of Yahweh and he went and he dwelt at [the] wadi of Kerith which [is] on [the] face of the Jordan.
6 Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi na mkate na nyama jioni, naye akanywa maji kutoka kile kijito.
And the ravens [were] bringing to him bread and meat in the morning and bread and meat in the evening and from the wadi he drank.
7 Baada ya muda, kile kijito kikakauka kwa sababu mvua haikuwa imenyesha katika nchi.
And it was from [the] end of days and it dried up the wadi for not it had been rain in the land.
8 Kisha neno la Bwana likamjia, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to him saying.
9 “Ondoka, uende Sarepta ya Sidoni na ukae huko. Nimemwagiza mjane katika sehemu ile akupatie chakula.”
Arise go Zarephath towards which [belongs] to Sidon and you will dwell there here! I have commanded there a woman a widow to supply you.
10 Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwambia, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.”
And he arose - and he went Zarephath towards and he came to [the] entrance of the city and there! there a woman a widow [was] gathering wood and he called out to her and he said get please for me a little of water in vessel so I may drink.
11 Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.”
And she went to get [it] and he called out to her and he said get please for me a piece of bread in hand your.
12 Akamjibu, “Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, sina mkate wowote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule, kiishe, tukafe.”
And she said [by] [the] life of Yahweh God your if there to me [is] food that except [the] fullness of a palm of flour in jar and a little of oil in jug and here I [am] gathering two wood and I will go and I will prepare it for myself and for son my and we will eat it and we will die.
13 Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unitengenezee mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyo navyo kisha uniletee na ndipo utayarishe chochote kwa ajili yako na mwanao.
And he said to her Elijah may not you fear go do according to word your only make for me from there a bread cake small at first and you will bring [it] out to me and for yourself and for son your you will prepare at the last.
14 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi.’”
For thus he says Yahweh [the] God of Israel [the] jar of flour not it will be at an end and [the] jug of oil not it will be lacking until [the] day (gives *Q(k)*) Yahweh rain on [the] surface of the ground.
15 Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake.
And she went and she did according to [the] word of Elijah and she ate (she and he *Q(K)*) and household her days.
16 Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la Bwana alilosema Eliya.
[the] jar of Flour not it was at an end and [the] jug of oil not it was lacking according to [the] word of Yahweh which he spoke by [the] hand of Elijah.
17 Baada ya muda, mwana wa yule mwanamke mwenye nyumba akaugua. Hali yake ikaendelea kuwa mbaya sana, na hatimaye akaacha kupumua.
And it was after the things these he became sick [the] son of the woman [the] mistress of the house and it was sickness his severe very until that not it was left in him breath.
18 Akamwambia Eliya, “Una nini dhidi yangu, ewe mtu wa Mungu? Umekuja ili kukumbushia dhambi yangu na kusababisha kifo cha mwanangu?”
And she said to Elijah what? [is] to me and to you O man of God you have come to me to bring to remembrance iniquity my and to put to death son my.
19 Eliya akamjibu, “Nipe mwanao.” Eliya akampokea kutoka kifuani mwake, akambeba mpaka chumba cha juu alipokuwa anaishi, akamlaza kitandani mwake.
And he said to her give to me son your and he took him from bosom her and he took up him to the upper room where he [was] dwelling there and he made lie him on bed his.
20 Kisha akamlilia Bwana, akasema “Ee Bwana Mungu wangu, je, pia umeleta msiba juu ya mjane huyu ninayeishi pamoja naye, kwa kusababisha mwanawe kufa?”
And he called out to Yahweh and he said O Yahweh God my ¿ also on the widow whom I [am] staying as a sojourner with her have you done harm by putting to death son her.
21 Kisha akajinyoosha juu ya kijana mara tatu na kumlilia Bwana, akisema, “Ee Bwana Mungu wangu, nakuomba roho ya huyu kijana imrudie!”
And he stretched himself over the lad three times and he called out to Yahweh and he said O Yahweh God my let it return please [the] life of the lad this to inward part[s] his.
22 Bwana akasikia kilio cha Eliya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.
And he listened Yahweh to [the] voice of Elijah and it returned [the] life of the lad to inward part[s] his and he lived.
23 Eliya akamtwaa kijana na kumbeba kutoka chumbani mwake akamshusha kumpeleka kwenye nyumba. Akampa mama yake na kusema, “Tazama, mwanao yu hai!”
And he took Elijah the lad and he brought down him from the upper room the house towards and he gave him to mother his and he said Elijah see [is] alive son your.
24 Ndipo yule mwanamke akamwambia Eliya, “Sasa ninajua kwamba wewe ni mtu wa Mungu, na kwamba neno la Bwana kutoka kinywani mwako ni kweli.”
And she said the woman to Elijah now this I know that [are] a man of God you and [the] word of Yahweh in mouth your [is] truth.

< 1 Wafalme 17 >