< 1 Wafalme 13 >

1 Kwa neno la Bwana, mtu wa Mungu alifika Betheli kutoka Yuda wakati Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu ili kutoa sadaka.
И се, человек Божий прииде от Иуды по словеси Господню в Вефиль, и Иеровоам стояше на олтари своем жрети хотя:
2 Akapiga kelele dhidi ya madhabahu kwa neno la Bwana: “Ee madhabahu, madhabahu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi. Juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu wale ambao wanatoa sadaka hapa sasa, nayo mifupa ya wanadamu itachomwa juu yako.’”
и воззва ко олтарю словом Господним и рече: олтарю, олтарю, сице глаголет Господь: се, сын раждается дому Давидову, Иосиа имя ему, и пожрет на тебе жерцы, иже на высоких жрущыя на тебе, и кости человеческия сожжет на тебе.
3 Siku iyo hiyo, mtu wa Mungu akatoa ishara: “Hii ndiyo ishara Bwana aliyotangaza: Madhabahu haya yatapasuka na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.”
И даст в день той чудо, глаголя: сей глаголгол, егоже рече Господь, глаголя: се, олтарь разсядется, и излиется тук иже на нем.
4 Mfalme Yeroboamu aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, alipopiga kelele dhidi ya madhabahu huko Betheli, akanyoosha mkono wake kutoka madhabahuni na kusema, “Mkamate!” Lakini mkono aliokuwa ameunyoosha kumwelekea yule mtu ukasinyaa na kubaki hapo hapo, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha.
И бысть егда услыша царь Иеровоам словеса человека Божия воззвавшаго ко олтарю иже в Вефили, и простре царь руку свою от олтаря, глаголя: имите его. И се, усше рука его, юже простре нань, и не можаше возвратити ю к себе:
5 Pia, madhabahu yalipasuka na majivu yakamwagika sawasawa na ishara iliyotolewa na mtu wa Mungu kwa neno la Bwana.
и олтарь разседеся, и излияся тук от олтаря, по чудеси, еже даде человек Божий словом Господним.
6 Kisha mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “Niombee kwa Bwana Mungu wako ili mkono wangu upate kupona.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwombea kwa Bwana, nao mkono wa mfalme ukapona na kuwa kama ulivyokuwa hapo kwanza.
И рече царь Иеровоам человеку Божию: помолися ныне пред лицем Господа Бога твоего, дабы возвратилася рука моя ко мне. И помолися человек Божий пред лицем Господним, и возвратися рука царя к нему, и бысть якоже прежде.
7 Mfalme akamwambia yule mtu wa Mungu, “Twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
И глагола царь к человеку Божию: вниди со мною в дом, и обедай, и дам ти дар.
8 Lakini yule mtu wa Mungu akamjibu mfalme, “Hata kama ungenipa nusu ya mali zako, nisingekwenda pamoja na wewe, wala nisingekula mkate au kunywa maji hapa.
И рече человек Божий к цареви: аще даси ми пол дому твоего, не вниду с тобою, ниже ям хлеба, ниже пию воды на месте сем,
9 Kwa kuwa niliagizwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate wala usinywe maji au kurudi kwa njia uliyojia.’”
яко тако заповеда ми Господь словом, глаголя: ни яждь хлеба, ни пий воды, ниже возвратися путем, имже шел еси.
10 Kwa hiyo akafuata njia nyingine na hakurudi kupitia njia ile ambayo alikuwa ameijia Betheli.
И отиде путем иным, и не возвратися путем, имже прииде во Вефиль.
11 Basi kulikuwepo na nabii fulani mzee aliyekuwa anaishi Betheli, ambaye wanawe walikuja kumwambia yote ambayo mtu wa Mungu alikuwa ameyafanya pale siku ile. Pia wakamwambia baba yao yale aliyomwambia mfalme.
И пророк един стар живяше в Вефили, и приидоша сынове его и поведаша ему вся дела, яже сотвори человек Божий в день той в Вефили, и словеса, яже глагола цареви, поведаша отцу своему.
12 Baba yao akawauliza, “Ameelekea njia gani?” Nao wanawe wakamwonyesha ile njia yule mtu wa Mungu kutoka Yuda aliyopita.
И рече к ним отец их, глаголя: киим путем иде? И показаша ему сынове его путь, имже иде человек Божий изшедый от Иуды.
13 Hivyo akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda.” Walipokwisha kumtandikia punda, akampanda
И рече сыном своим: оседлайте ми осля. И оседлаша ему осля, и вседе на не,
14 na kumfuatilia yule mtu wa Mungu. Akamkuta ameketi chini ya mwaloni na akamuuliza, “Je, wewe ndiwe mtu wa Mungu kutoka Yuda?” Akamjibu, “Mimi ndiye.”
и иде вслед человека Божия, и обрете его под дубом седяща, и рече ему: ты ли еси человек Божий пришедый от Иуды? И рече ему: аз.
15 Basi nabii akamwambia, “Karibu nyumbani pamoja na mimi ule.”
И рече ему: гряди со мною, и яждь хлеб.
16 Yule mtu wa Mungu akasema, “Siwezi kurudi na kwenda nawe, wala siwezi kula mkate au kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.
И рече ему: не могу возвратитися с тобою, ниже ям хлеба, ни пию воды на месте сем,
17 Nimeambiwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate au kunywa maji huko au kurudia njia uliyojia.’”
яко тако заповеда ми Господь словом, глаголя: не яждь хлеба тамо, ниже пий воды тамо, и да не возвратишися путем тем, имже шел еси.
18 Yule nabii mzee akajibu, “Mimi pia ni nabii, kama wewe. Naye malaika alisema nami kwa neno la Bwana: ‘Mrudishe aje katika nyumba yako ili apate kula mkate na kunywa maji.’” (Lakini alikuwa akimwambia uongo.)
И рече к нему: и аз пророк есмь якоже ты, и Ангел глагола ко мне словом Господним, глаголя: возврати его к себе в дом твой, да снест хлеба и пиет воду. И солга ему,
19 Hivyo mtu wa Mungu akarudi pamoja naye na akala na kunywa katika nyumba yake.
и возврати его: и яде хлеб, и пи воду в дому его.
20 Wakati walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia yule nabii mzee aliyemrudisha huyo mtu wa Mungu.
И бысть им седящым на трапезе, и бысть слово Господне ко пророку возвращшему его.
21 Akampazia sauti yule mtu wa Mungu aliyekuwa ametoka Yuda, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Umeasi neno la Bwana na hukushika amri uliyopewa na Bwana Mungu wako,
И рече к человеку Божию пришедшему от Иуды, глаголя: сице глаголет Господь: понеже преогорчил еси глаголгол Господень и не сохранил еси заповеди, юже заповеда тебе Господь Бог твой,
22 bali ulirudi na ukala mkate na kunywa maji mahali ambapo alikuambia usile wala usinywe. Kwa hiyo maiti yako haitazikwa katika kaburi la baba zako.’”
и возвратився ял еси хлеб и пил еси воду на месте сем, о немже рече к тебе, глаголя: да не яси хлеба и не пиеши воды: сего ради не внидет во гроб тело твое со отцы твоими.
23 Wakati huyo mtu wa Mungu alipomaliza kula na kunywa, nabii aliyekuwa amemrudisha akamtandikia punda wake.
И бысть по ядении хлеба и по питии воды, и оседла осля тому пророку, и возвратися, и отиде:
24 Alipokuwa akienda akakutana na simba njiani, akamuua na maiti yake ikabwagwa barabarani, yule punda wake na simba wakiwa wamesimama karibu yake.
и обрете его лев на пути, и умертви его: и бе тело его повержено на пути, и осел стояше над ним, и лев стояше близ телесе (его):
25 Baadhi ya watu waliopita pale waliona maiti imebwagwa pale chini, simba akiwa amesimama kando ya maiti, wakaenda na kutoa habari katika mji ambao nabii mzee aliishi.
и се, мужие мимоидуще, и видеша мертва повержена на пути и льва стояща близ мертваго: и приидоша, и поведаша во граде, в немже живяше пророк старый.
26 Yule nabii aliyekuwa amemrudisha kutoka safari yake aliposikia habari hii akasema, “Ni yule mtu wa Mungu ambaye aliasi neno la Bwana. Bwana amemtoa kwa simba, ambaye amemrarua na kumuua, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limemwonya.”
И услыша (сие пророк) возвративый его с пути и рече: человек Божии сей есть, иже преступи глаголгол Божий, и предаде его Господь льву, и сокруши его, и умертви его по глаголголу Господню, егоже рече ему.
27 Nabii akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda,” nao wakafanya hivyo.
И повеле сыном своим, глаголя: оседлайте ми осля. И оседлаша.
28 Kisha akatoka akaenda akakuta maiti imebwagwa chini barabarani, punda na simba wakiwa wamesimama kando yake. Simba hakuwa amekula ile maiti wala kumrarua punda.
И пойде, и обрете тело его повержено на пути, и осел и лев стояста над телом, и не снеде лев телесе человека Божия и не сокруши осла.
29 Basi yule nabii mzee akachukua maiti ya mtu wa Mungu, akailaza juu ya punda na akairudisha katika mji wake, ili amwombolezee na kumzika.
И взя пророк тело человека Божия, и возложи е на осля, и возврати е пророк, и вниде во град погребсти его,
30 Kisha akailaza ile maiti katika kaburi lake huyo nabii mzee, nao wakaomboleza juu yake na kusema, “Ee ndugu yangu!”
и положи тело его во гробе своем, и рыдаше по нем: увы, брате.
31 Baada ya kumzika, akawaambia wanawe, “Wakati nitakapokufa, mnizike kwenye kaburi alimozikwa huyu mtu wa Mungu; lazeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
И бысть по рыдании о нем, и рече к сыном своим, глаголя: аще умру, погребите мя во гробе сем, идеже человек Божий погребен есть, при костех его положите мя, да спасутся кости моя с костьми его,
32 Kwa maana ujumbe alioutangaza kwa neno la Bwana dhidi ya madhabahu huko Betheli na dhidi ya madhabahu yote katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Samaria, hakika yatatokea kweli.”
яко сбудется глагол, егоже глагола словом Господним о олтари, иже во Вефили, и о домех высоких, иже в Самарии.
33 Hata baada ya haya, Yeroboamu hakubadili njia zake mbaya, lakini mara nyingine tena akaweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu kutoka watu wa aina zote. Yeyote aliyetaka kuwa kuhani alimweka wakfu kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu.
И по глаголе сем не обратися Иеровоам от злобы своея, и возвратися, и сотвори от части единыя людий жерцы высоких: иже хотяше, исполняше руку свою, и бываше жрец на высоких.
34 Hii ilikuwa ndiyo dhambi ya nyumba ya Yeroboamu ambayo iliisababishia kuanguka na kuangamia kwake hadi kutoweka kwenye uso wa dunia.
И бысть глагол сей в прегрешение дому Иеровоамлю, и на испровержение, и на изчезновение от лица земли.

< 1 Wafalme 13 >