< 1 Wafalme 12 >

1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
And Rehoboam goeth to Shechem, for to Shechem hath all Israel come to make him king.
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
And it cometh to pass, at Jeroboam son of Nebat's hearing (and he [is] yet in Egypt where he hath fled from the presence of Solomon the king, and Jeroboam dwelleth in Egypt),
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
that they send and call for him; and they come — Jeroboam and all the assembly of Israel — and speak unto Rehoboam, saying,
4 “Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
'Thy father made hard our yoke, and thou, now, make light [some] of the hard service of thy father, and his heavy yoke that he put upon us, and we serve thee.'
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
And he saith unto them, 'Go — yet three days, and come back unto me;' and the people go.
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
And king Rehoboam consulteth with the elders who have been standing in the presence of Solomon his father, in his being alive, saying, 'How are ye counselling to answer this people?'
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
And they speak unto him, saying, 'If, to-day, thou art servant to this people, and hast served them, and answered them, and spoken unto them good words, then they have been to thee servants all the days.'
8 Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
And he forsaketh the counsel of the elders which they counselled him, and consulteth with the lads who have grown up with him, who are standing before him;
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
and he saith unto them, 'What are ye counselling, and we answer this people, who have spoken unto me, saying, Lighten [somewhat] of the yoke that thy father put upon us?'
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
And they speak unto him — the lads who had grown up with him — saying, 'Thus dost thou say to this people who have spoken unto thee, saying, Thy father made our yoke heavy, and thou, make [it] light upon us; thus dost thou speak unto them, My little [finger] is thicker than the loins of my father;
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
and now, my father laid on you a heavy yoke, and I add to your yoke; my father chastised you with whips, and I — I chastise you with scorpions.'
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
And they come — Jeroboam and all the people — unto Rehoboam, on the third day, as the king had spoken, saying, 'Come back unto me on the third day.'
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
And the king answereth the people sharply, and forsaketh the counsel of the elders which they counselled him,
14 akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
and speaketh unto them, according to the counsel of the lads, saying, 'My father made your yoke heavy, and I add to your yoke; my father chastised you with whips, and I — I chastise you with scorpions;'
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
and the king hearkened not unto the people, for the revolution was from Jehovah, in order to establish His word that Jehovah spake by the hand of Ahijah the Shilonite unto Jeroboam son of Nebat.
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
And all Israel see that the king hath not hearkened unto them, and the people send the king back word, saying, 'What portion have we in David? yea, there is no inheritance in the son of Jesse; to thy tents, O Israel; now see thy house, O David!' and Israel goeth to its tents.
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
As to the sons of Israel, those dwelling in the cities of Judah — over them reign doth Rehoboam.
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
And king Rehoboam sendeth Adoram who [is] over the tribute, and all Israel cast at him stones, and he dieth; and king Rehoboam hath strengthened himself to go up into a chariot to flee to Jerusalem;
19 Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
and Israel transgresseth against the house of David unto this day.
20 Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
And it cometh to pass, at all Israel's hearing that Jeroboam hath returned, that they send and call him unto the company, and cause him to reign over all Israel; none hath been after the house of David save the tribe of Judah alone.
21 Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
And Rehoboam cometh to Jerusalem, and assembleth all the house of Judah and the tribe of Benjamin, a hundred and eighty thousand chosen warriors, to fight with the house of Israel, to bring back the kingdom to Rehoboam son of Solomon.
22 Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
And the word of God is unto Shemaiah a man of God, saying,
23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
'Speak unto Rehoboam son of Solomon, king of Judah, and unto all the house of Judah and Benjamin, and the rest of the people, saying,
24 ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
Thus said Jehovah, Ye do not go up nor fight with your brethren the sons of Israel; turn back each to his house, for from Me hath this thing been;' and they hear the word of Jehovah, and turn back to go according to the word of Jehovah.
25 Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
And Jeroboam buildeth Shechem in the hill-country of Ephraim, and dwelleth in it, and goeth out thence, and buildeth Penuel;
26 Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
and Jeroboam saith in his heart, 'Now doth the kingdom turn back to the house of David —
27 Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
if this people go up to make sacrifices in the house of Jehovah in Jerusalem, then hath the heart of this people turned back unto their lord, unto Rehoboam king of Judah, and they have slain me, and turned back unto Rehoboam king of Judah.'
28 Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
And the king taketh counsel, and maketh two calves of gold, and saith unto them, 'Enough to you of going up to Jerusalem; lo, thy gods, O Israel, which brought thee up out of the land of Egypt.'
29 Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
And he setteth the one in Beth-El, and the other he hath put in Dan,
30 Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
and this thing becometh a sin, and the people go before the one — unto Dan.
31 Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
And he maketh the house of high places, and maketh priests of the extremities of the people, who were not of the sons of Levi;
32 Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
and Jeroboam maketh a festival in the eighth month, in the fifteenth day of the month, like the festival that [is] in Judah, and he offereth on the altar — so did he in Beth-El — to sacrifice to the calves which he made, and he hath appointed in Beth-El the priests of the high places that he made.
33 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.
And he offereth up on the altar that he made in Beth-El, on the fifteenth day of the eighth month, in the month that he devised of his own heart, and he maketh a festival to the sons of Israel, and offereth on the altar — to make perfume.

< 1 Wafalme 12 >