< 1 Yohana 1 >
1 Tunawajulisha lile lililokuwepo tangu mwanzo, lile tulilosikia, ambalo tumeliona kwa macho yetu, ambalo tumelitazama na kuligusa kwa mikono yetu, kuhusu Neno la uzima.
That which was from the beginning, which we have heard, which we have seen with our eyes, which we have looked upon, and our hands have handled, of the word of life;
2 Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. (aiōnios )
(For the life was manifested, and we have seen [it], and testify, and show to you that eternal life which was with the Father, and was manifested to us; ) (aiōnios )
3 Twawatangazia lile tuliloliona na kulisikia, ili nanyi mwe na ushirika nasi. Na ushirika wetu hasa ni pamoja na Baba na Mwanawe, Yesu Kristo.
That which we have seen and heard we declare to you, that ye also may have fellowship with us: and truly our fellowship [is] with the Father, and with his Son Jesus Christ.
4 Tunaandika mambo haya ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
And these things we write to you, that your joy may be full.
5 Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake na kuwatangazia ninyi: kwamba Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza lolote.
This then is the message which we have heard from him, and declare to you, that God is light, and in him is no darkness at all.
6 Kama tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli.
If we say that we have fellowship with him, and walk in darkness, we lie, and do not the truth:
7 Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.
But if we walk in the light, as he is in the light, we have fellowship one with another, and the blood of Jesus Christ his Son cleanseth us from all sin.
8 Kama tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu.
If we say that we have no sin, we deceive ourselves, and the truth is not in us.
9 Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha kutoka kwenye udhalimu wote.
If we confess our sins, he is faithful and just to forgive us [our] sins, and to cleanse us from all unrighteousness.
10 Kama tukisema hatukutenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo na neno lake halimo ndani yetu.
If we say that we have not sinned, we make him a liar, and his word is not in us.