< 1 Wakorintho 15 >
1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
Dozivljem vam, braćo, u pamet evanđelje koje vam navijestih, koje primiste, u kome stojite,
2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
po kojem se spasavate, ako držite što sam vam navijestio; osim ako uzalud povjerovaste.
3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
Doista, predadoh vam ponajprije što i primih: Krist umrije za grijehe naše po Pismima;
4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
bi pokopan i uskrišen treći dan po Pismima;
5 na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
ukaza se Kefi, zatim dvanaestorici.
6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
Potom se ukaza braći, kojih bijaše više od pet stotina zajedno; većina ih još i sada živi, a neki usnuše.
7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
Zatim se ukaza Jakovu, onda svim apostolima.
8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
Najposlije, kao nedonoščetu, ukaza se i meni.
9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
Da, ja sam najmanji među apostolima i nisam dostojan zvati se apostolom jer sam progonio Crkvu Božju.
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
Ali milošću Božjom jesam što jesam i njegova milost prema meni ne bijaše zaludna; štoviše, trudio sam se više nego svi oni - ali ne ja, nego milost Božja sa mnom.
11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
Ili dakle ja ili oni: tako propovijedamo, tako vjerujete.
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
No ako se propovijeda da je Krist od mrtvih uskrsnuo, kako neki među vama govore da nema uskrsnuća mrtvih?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
Ako nema uskrsnuća mrtvih, ni Krist nije uskrsnuo.
14 Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
Ako pak Krist nije uskrsnuo, uzalud je doista propovijedanje naše, uzalud i vjera vaša.
15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
Zatekli bismo se i kao lažni svjedoci Božji što posvjedočismo protiv Boga: da je uskrisio Krista, kojega nije uskrisio, ako doista mrtvi ne uskršavaju.
16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
Jer ako mrtvi ne uskršavaju, ni Krist nije uskrsnuo.
17 Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
A ako Krist nije uskrsnuo, uzaludna je vjera vaša, još ste u grijesima.
18 Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
Onda i oni koji usnuše u Kristu, propadoše.
19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
Ako se samo u ovom životu u Krista ufamo, najbjedniji smo od svih ljudi.
20 Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
Ali sada: Krist uskrsnu od mrtvih, prvina usnulih!
21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
Doista po čovjeku smrt, po Čovjeku i uskrsnuće od mrtvih!
22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
Jer kao što u Adamu svi umiru, tako će i u Kristu svi biti oživljeni.
23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
Ali svatko u svom redu: prvina Krist, a zatim koji su Kristovi, o njegovu Dolasku;
24 Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
potom - svršetak, kad preda kraljevstvo Bogu i Ocu, pošto obeskrijepi svako Vrhovništvo, svaku Vlast i Silu.
25 Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
Doista, on treba da kraljuje dok ne podloži sve neprijatelje pod noge svoje.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
Kao posljednji neprijatelj bit će obeskrijepljena Smrt
27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
jer sve podloži nogama njegovim. A kad veli: Sve je podloženo, jasno - sve osim Onoga koji mu je sve podložio.
28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
I kad mu sve bude podloženo, tada će se i on sam, Sin, podložiti Onomu koji je njemu sve podložio da Bog bude sve u svemu.
29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
Što onda čine oni koji se krste za mrtve? Ako mrtvi uopće ne uskršavaju, što se krste za njih?
30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
Što se onda i mi svaki čas izlažemo pogiblima?
31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
Dan za danom umirem, tako mi slave vaše, braćo, koju imam u Kristu Isusu, Gospodinu našem!
32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
Ako sam se po ljudsku borio sa zvijerima u Efezu, kakva mi korist? Ako mrtvi ne uskršavaju, jedimo i pijmo jer sutra nam je umrijeti.
33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
Ne varajte se: “Zli razgovori kvare dobre običaje.”
34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
Otrijeznite se kako valja i ne griješite jer neki, na sramotu vam kažem, ne znaju za Boga.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
Ali reći će netko: Kako uskršavaju mrtvi? I s kakvim li će tijelom doći?
36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
Bezumniče! Što siješ, ne oživljuje ako ne umre.
37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
I što siješ, ne siješ tijelo buduće, već golo zrno, pšenice - recimo - ili čega drugoga.
38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
A Bog mu daje tijelo kakvo hoće, i to svakom sjemenu svoje tijelo.
39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
Nije svako tijelo isto tijelo; drugo je tijelo čovječje, drugo tijelo stoke, drugo tijelo ptičje, a drugo riblje.
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
Ima tjelesa nebeskih i tjelesa zemaljskih, ali drugi je sjaj nebeskih, a drugi zemaljskih.
41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
Drugi je sjaj sunca, drugi sjaj mjeseca i drugi sjaj zvijezda; jer zvijezda se od zvijezde razlikuje u sjaju.
42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
Tako i uskrsnuće mrtvih: sije se u raspadljivosti, uskršava u neraspadljivosti;
43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
sije se u sramoti, uskršava u slavi; sije se u slabosti, uskršava u snazi;
44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
sije se tijelo naravno, uskršava tijelo duhovno. Ako ima tijelo naravno, ima i duhovno.
45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
Tako je i pisano: Prvi čovjek, Adam, postade živa duša, posljednji Adam - duh životvorni.
46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
Ali ne bi najprije duhovno, nego naravno pa onda duhovno.
47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
Prvi je čovjek od zemlje, zemljan; drugi čovjek - s neba.
48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
Kakav je zemljani takvi su i zemljani, a kakav je nebeski takvi su i nebeski.
49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
I kao što smo nosili sliku zemljanoga, nosit ćemo i sliku nebeskoga.
50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
A ovo, braćo, tvrdim: tijelo i krv ne mogu baštiniti kraljevstva Božjega i raspadljivost ne baštini neraspadljivosti.
51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
Evo otajstvo vam kazujem: svi doduše nećemo usnuti, ali svi ćemo se izmijeniti.
52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
Odjednom, u tren oka, na posljednju trublju - jer zatrubit će - i mrtvi će uskrsnuti neraspadljivi i mi ćemo se izmijeniti.
53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
Jer ovo raspadljivo treba da se obuče u neraspadljivost i ovo smrtno da se obuče u besmrtnost.
54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
A kad se ovo raspadljivo obuče u neraspadljivost i ovo smrtno obuče u besmrtnost, tada će se obistiniti riječ napisana: Pobjeda iskapi smrt.
55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs )
Gdje je, smrti, pobjeda tvoja? Gdje je, smrti, žalac tvoj? (Hadēs )
56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
Žalac je smrti grijeh, snaga je grijeha Zakon.
57 Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
A hvala Bogu koji nam daje pobjedu po Gospodinu našem Isusu Kristu!
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.
Tako, braćo moja ljubljena, budite postojani, nepokolebljivi, i obilujte svagda u djelu Gospodnjem znajući da trud vaš nije neplodan u Gospodinu.