< 1 Nyakati 11 >

1 Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
Zebrał się tedy wszystek Izrael do Dawida do Hebronu, mówiąc: Otośmy kość twoja i ciało twoje!
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Jako i przedtem, gdy jeszcze był Saul królem, też wywodził i wwodził Izraela. Tak Pan, Bóg twój, rzekł tobie: Ty będziesz pasł lud mój Izraelski, a ty będziesz wodzem nad ludem moim Izraelskim.
3 Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
A tak przyszli wszyscy starsi Izraelscy do króla do Hebronu, i uczynił Dawid z nimi przymierze w Hebronie przed Panem, i pomazali Dawida za króla nad Izraelem według słowa Pańskiego, które powiedział przez Samuela.
4 Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
Jechał tedy Dawid ze wszystkim Izraelem do Jeruzalemu, które jest Jebus, gdzie byli Jebuzejczycy obywatelami ziemi.
5 wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
I rzekli obywatele Jebuzejscy do Dawida: Nie wnijdziesz sam. Ale Dawid wziął zamek Syoński, który jest miastem Dawidowem.
6 Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
Bo był rzekł Dawid: Ktobykolwiek poraził Jebuzejczzyka najpierwej, ten będzie skiążęciem i hetmanem. Przetoż wstąpił najpierw Joab, syn Sarwii, i został hetmanem.
7 Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
I mieszkał Dawid na onym zamku; dla tego nazwano go miastem Dawidowem.
8 Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
I zbudował miasto w około, od Mello aż w okrąg; a Joab pobudował ostatek miasta.
9 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
A tak Dawid im dalej, tem więcej rozmnażał się, i rosł; albowiem Pan zastępów był z nim.
10 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
A cić są najorzedniejsi rycerze, których miał Dawid, którzy się mężnie starali z nim o królestwo jego ze wszystkim Izraelem, aby go królem uczynili według słowa Pańskiego nad Izraelem.
11 Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
A tenci jest poczet rycerzy, których miał Dawid: Jasobam, syn Chachmonowy, przedniejszy między trzydziestoma; ten podniósłszy oszczep swój na trzystu, jednym razem ich zabił.
12 Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
A po nim Elezar, syn Dodonowy, Achochytczyk; ten był jednym między trzema mocarzami.
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
Ten był z Dawidem w Pasdamim, gdzie się zebrali byli Filistynowie ku bitwie; a była ona część pola pełna jęczmienia, a lud był uciekł przed Filistynami.
14 Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
I stanęli w pośród onego pola, i obronili go, a porazili Filistynów: i wybawił Pan lud wybawieniem wielkiem.
15 Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Ci także trzej ze trzydziestu przedniejszych wstąpili na skałę do Dawida do jaskini Odollam, gdyż wojsko Filistyńskie leżało obozem w dolinie Rafaim;
16 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
Albowiem Dawid natenczas mieszkał na zamku, a stanowisko Filistyńskie było natenczas w Betlehem.
17 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
Pragnęł tedy Dawid: Oby mi się kto dał napić wody z studni Betlehemskiej, która jest u bramy!
18 Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Przetoż przebiwszy się ci trzej przez wojsko Filistyńskie, naczerpali wody z studni Betlehemskiej, która jest u bramy, a wziąwszy przynieśli do Dawida. Lecz jej nie chciał Dawid pić, ale ją wylał na ofiarę Panu.
19 Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
I rzekł: Nie daj mi tego, Boże mój, abym to uczynić miał! Izali krew tych mężów pić będą, którzy odważyli żywot swój? albowiem z odwagą żywota swego przynieśli ją; i nie chciał jej pić. Toć uczynili trzej oni mocarze.
20 Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
A Abisaj, brat Joabowy, był przedniejszy z onych trzech; tenże podniósł włócznię swą na trzysta ludu, które pobił, i otrzymał sławę między onymi trzema.
21 Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
Z tych trzech nad innych dwóch był sławniejszy, a był ich książęciem; jednak onych trzech pierwszych nie doszedł.
22 Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Banajas też, syn Jojady, syn męża dużego, wielkich spraw, z Kabseela, ten zabił dwóch mocarzów Moabskich; ten też zszedłszy zabił lwa w pośród jamy, gdy był śnieg.
23 Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
Ten też zabił męża Egipczanina, męża, którego wzrost był na pięć łokci. A chociaż Egipczanin miał w ręku oszczep jako nawój tkacki, wszkże przyszedł do niego z kijem, i wydarł oszczep z ręki Egipczanina, i zabił go oszczepem jego.
24 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
To uczynił Banajas, syn Jojady, który także sławnym został między onymi trzema mocarzami.
25 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
A choć był między onymi trzydziestoma sławnym, wszakże nie doszedł onych trzech. I postanowił go Dawid nad drabantami swymi.
26 Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
A w wojsku co mocniejsi byli: Asael, brat Joabowy, Elkanan, syn Dodonowy z Betlehem;
27 Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
Sammot Harodczyk, Heles Felonitczyk;
28 Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
Hyra, syn Ikkiesowy, Tekuitczyk, Abiezer Anatotczyk;
29 Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
Sybbechaj Husatczyk, Ilaj Ahohytczyk;
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
Maharaj Netofatczyk, Heled, syn Baamy, Netofatczyk;
31 Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
Itaj, syna Rybajego, z Gabaat synów Benjaminowych, Banajas Faratończyk;
32 Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
Hutaj od potoku Gaas; Abiel Arbatczyk;
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Asmawet Bacharomczyk; Elijachba Salabończyk.
34 wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
Synowie Asema Gisończyka: Jonatan, syn Sagii, Hororczyk;
35 Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
Ahijam, syn Zacharowy, Ararytczyk, Elifal, syn Urowy;
36 Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
Hefer Mecheratczyk, Achijas Felonitczyk;
37 Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
Hesro Karmelczyk, Naaraj, syn Ezbajowy;
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
Joel, brat Natanowy, Michbar, syn Gierego.
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Selek Ammonitczyk, Nacharaj Berotczyk, który nosił broń Koaba, syna Sarwii;
40 Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
Hyra Itrejczyk, Gareb Itrejczyk;
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
Uryjasz Hetejczyk, Zabad, syn Achalajego.
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
Adyna, syn Sysy, Rubenitczyk, książę Rubenitów, a z nim trzydzieści mężów.
43 Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
Hanan, syn Maachy, i Jozafat Mitnitczyk.
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
Uzyjasz Asteratczyk, Sama i Jehijel, synowie Hotamy Aroerytczyka.
45 Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
Jedinael, syn Symry, i Jocha, brat jego, Tysytczyk.
46 Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
Eliel Machawimczyk, i Jerybaj, i Josawijasz, synowie Elnaamowi, i Itma Moabczyk.
47 Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.
Eliel, i Obed, i Jaasyjel z Mezobaj.

< 1 Nyakati 11 >