< Éxodo 6 >
1 Y él Señor dijo a Moisés: Ahora verás lo que voy a hacer a Faraón; porque con una mano fuerte se verá obligado a dejarlos ir, expulsándolos de su tierra a causa de mi brazo extendido.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
2 Y dijo Dios a Moisés: Yo soy el Señor.
Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
3 Me dejé ver por Abraham, Isaac y Jacob, como Dios, el Gobernante de todos; pero ellos no sabían mi nombre Él SEÑOR.
Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
4 Y pacté con ellos, para darles la tierra de Canaán, la tierra de sus andanzas.
Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
5 Y mis oídos están abiertos al clamor de los hijos de Israel, a quienes los egipcios tienen bajo su yugo; y he tenido en cuenta mi pacto.
Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
6 Di, pues, a los hijos de Israel: Yo soy EL SEÑOR, y te sacaré del yugo de los egipcios, y te libraré de su poder, y te libraré con la fuerza de mi brazo después de grandes castigos.
“Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
7 Y te tomaré para que seas mi pueblo y yo seré tu Dios; y estarás seguro de que yo soy el SEÑOR tu Dios, que te saca del yugo de los egipcios.
Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
8 Y seré tu guía en la tierra que juré dar a Abraham, a Isaac y a Jacob; y yo te lo daré por tu herencia: SOY EL SEÑOR.
Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
9 Y Moisés dijo estas palabras a los hijos de Israel, pero ellos no le prestaron atención, por el dolor de su espíritu y el peso cruel de su yugo.
Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
10 Y Él Señor dijo a Moisés:
Ndipo Bwana akamwambia Mose,
11 Entra y di a Faraón, rey de Egipto, que deje ir a los hijos de Israel de su tierra.
“Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
12 Entonces Moisés, respondiendo al SEÑOR, dijo: Mira, los hijos de Israel no me prestarán atención; ¿cómo, pues, me escuchará el Faraón, cuyos labios son inmundos?
Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
13 Y fué palabra de Él Señor a Moisés y á Aarón, y les dio órdenes para los hijos de Israel y de Faraón, rey de Egipto, para sacar á los hijos de Israel de la tierra de Egipto.
Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
14 Estas son las cabezas de las familias de sus padres: los hijos de Rubén, el hijo mayor de Israel: Hanoc, Falú, Hezrón y Carmi; estas son las familias de Rubén.
Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
15 Y los hijos de Simeón: Jemuel, Jamín, Ohad, Jaquín, Zohar, y Saúl, hijo de mujer de Canaán. Estas son las familias de Simeón.
Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
16 Y estos son los nombres de los hijos de Leví en el orden de sus generaciones: Gersón, Coat y Merari; y los años de la vida de Leví fueron ciento treinta y siete.
Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
17 Los hijos de Gersón: Libni y Simei, en el orden de sus familias.
Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
18 Y los hijos de Coat: Amram, e Izhar, y Hebrón, y Uziel; y los años de la vida de Coat, ciento treinta y tres.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
19 Y los hijos de Merari: Mahli y Musi: estas son las familias de los levitas, en el orden de sus generaciones.
Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
20 Y Amram tomó a Jocabed, la hermana de su padre, como esposa; y ella dio a luz a Aarón y a Moisés, y los años de la vida de Amram fueron ciento treinta y siete.
Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
21 Y los hijos de Izhar: Coré, y Nefeg, y Zicri.
Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
22 Y los hijos de Uziel: Misael, Elzafán y Sitri.
Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
23 Y tomó Aarón por mujer a Elisabet, hija de Aminadab, hermana de Naasón; y ella dio a luz a Nadab y Abiú, Eleazar e Itamar.
Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
24 Y los hijos de Coré: Asir, Elcana y Abiasaf: estas son las familias de los Coréitas.
Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
25 Y Eleazar, hijo de Aarón, tomó por esposa a una de las hijas de Futiel; y ella dio a luz a Finees. Estos son los jefes de las familias de los levitas, en el orden de sus familias.
Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
26 Estos son el mismo Aarón y Moisés a quienes el Señor dijo: Saca a los hijos de Israel de la tierra de Egipto de acuerdo a sus ejércitos.
Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
27 Estos son los hombres que ordenaron a Faraón que dejara salir a los hijos de Israel de Egipto: estos son los mismos Moisés y Aarón.
Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
28 Y el día que vino la palabra de Señor a Moisés en la tierra de Egipto,
Bwana aliponena na Mose huko Misri,
29 Dijo el Señor a Moisés: Yo soy el Señor; di a Faraón, rey de Egipto, todo lo que te digo.
akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
30 Y dijo Moisés a él Señor: Mis labios son torpes para hablar; ¿Cómo es posible que Faraón me haga una audiencia?
Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”